plan z
JF-Expert Member
- Jun 10, 2019
- 1,395
- 1,439
SIMU/WHATSAPP: 0768571786
Ilipoishia...
kila meseji niliyotuma WhatsApp aliisoma lakini hakunijibu, sikutaka kukata tamaa kwa sababu nilikua nampenda, niliendelea kumtafuta lakini cha ajabu hata nilipompigia simu hakupokea tena wakati mwingine alikata kabisa.
Songa nayo..
Kweli dunia duara yote yaliyomkuta Lucyra yalinikuta mimi, tena ilikua afadhali ya Lucyra nilikua nikimjibu meseji na kupokea simu zake, mimi simu zangu kwa Leyra hazikupokelewa na meseji hazikujibiwa kabisa ingawa alikua anazisoma. Ilikua ghafla sana sikutegemea kama Leyra angebadilika kiasi kile, kiukweli niliumia sana. Ni kama Lucyra aliniambukiza, maradhi yake yote ya mapenzi yalihamia kwangu, kwa mara ya kwanza nikaonja maumivu makali aliyokua anayapata Lucyra juu yangu hakika akikua anateseka sana.Nilikua nampenda sana Leyra pengine kuliko kitu chochote kile ukimtoa Mungu na wazazi wangu. Yeye ndie alikua mwanamke wangu wa kwanza kumpenda maishani mwangu, mapendo yote ya kipadri niliyofundishwa seminarini Don Bosco kule nchini Kenya yalikua kwake kwa sababu sikua padri, labda baadae yangehamia kwa wagonjwa lakini nilikua mwanafunzi sikua daktari bado.
Nilitamani kumpigia Leyra simu na kumfokea kwa yale aliyokua ananifanyia lakini hata ningepiga simu isingepokelewa, hata kama ingepokelewa ningemfokea kama nani yake maana hatukua wapenzi, tulikua na ukaribu mkubwa lakini hatukukubaliana kua wapenzi sababu ya udomo zege wangu.Ni kama nilikua kuzimu inayotembea duniani, hali hii ilinitesa sana kuliko kitu chochote. Kila nilipoenda nilimuwaza Leyra, iwe kanisani, uwanja wa taifa kutazama mpira au bichi kupunga upepo bado sura yake ilikatiza kwenye mzunguko wangu wa damu, nilishindwa kabisa kumsahau Leyra.
Ile miezi mitano ya likizo kwangu ilikua ni kama miaka mitano, nilitamani sana kuonana na Leyra niliamini labda ingefanya akumbuke tulivyokua. Nilijuta sana kwanini nilishindwa kumwambia Leyra hisia zangu kua ninampenda, ingawa yeye mwenyewe alilijua hilo. Hakuna marefu yasiyokua na mwisho, likizo yetu ilikua ndefu lakini mwisho wa siku iliisha. Wote tulirudi chuoni kwa furaha, kwanza kuingia mwaka wa tatu na kuanza mwaka mwingine wa masomo, pili kukutana tena na marafiki maana ni muda mrefu kidogo ulikua umepita. Chuoni nilipanga kumueleza Leyra hisia zangu kua ninampenda sana, ingawa ilikua ni kama nimechelewa maana Leyra alikua ameanza kubadilika tabia. Mwaka wa tatu ulianza, masomo yalikua magumu sana kuliko mwaka wa kwanza na wa pili. Bila kupoteza muda nilimtafuta Leyra mapema sana kabla masomo hayajawa magumu zaidi. Sikuamini nilichokiona, safari hii ilikua ni bora kuongea na Leyra kwenye simu kuliko ana kwa ana.
Leyra alikua amebadilika sana, hakupenda kuongea na mimi tena kama zamani, achana na kumshika mkono na kubusu mashavu yake muda huu Leyra hakutaka hata nimguse. Leyra alianza kunichukia ghafla, zile fursa zote adimu za kutoka out na kwenda kutembea pamoja sikuzipata tena, sikua nimemkosea lolote wala sikua nimemkubalia Lucyra lakini nashangaa kwanini alibadilika na kuanza kunichukia.
Mwaka huo wa tatu wa masomo ulikua wa mateso mengi kwangu, achana na ugumu wa masomo darasani, kutotakiwa tena na Leyra ilikua ni kama nipo jela. Nilijuta kusoma hapo chuoni Baltimore key health chuoni sio kwa sababu ni chuo kibaya hapana, ni kwa sababu uwepo wangu hapo ulifanya nikutane na Leyra, na kua mtu wa kuteseka kila siku kwa sababu yake.
Nilitamani kuhama chuoni hapo kama Lucyra ili niwe mbali zaidi na Leyra labda ingeweza kunisaidia lakini kwa bahati mbaya nilikua nimechelewa, haikua rahisi kupata uhamisho mwaka wa tatu. Furaha yote niliyokua nayo mwanzo chuoni hapo iligeuka kua huzuni, kwanini Leyra hanipendi tena?, nilijiuliza lakini sikupata majibu hasa ukizingatia sikua nimemkosea hata mara moja. Nilichanganyikiwa sana.
Ukiacha Mungu pia nina amini sana katika sayansi lakini yaliyonikuta yalifanya kwa mara ya kwanza niamini maneno ya wahenga kua ‘Chelewa chelewa utakuta mwana sio wako’. Nilijilaumu sana, msemo wa ‘Kuku wako manati ya nini’ uliniponza, nilijuta sana kwanini sikumwambia Leyra hisia zangu. Kwa mara nyingine tena niligundua ni jinsi gani Lucyra alikua akiumia juu yangu.
Mwaka wa tatu ulikua mwaka wa mwisho kwa Leyra chuoni hapo, yeye alikua anamaliza mwaka huo tofauti na mimi niliyekua nasoma miaka mitano kwa sababu ya kuchukua magonjwa mawili, magonjwa sugu ya wanawake na watoto pamoja na mifupa, wakati Leyra yeye alichukua ugonjwa mmoja tu wa mifupa.Semista ya kwanza mwaka wa tatu iliisha, ilikua maajabu, sikutaka kuamini kama kweli Leyra alikua mjamzito, niliumia sana pengine kuliko nyakati zote maisha yangu. Ujauzito wake ndio ulikua sababu kubwa ya kunichukia, sababu iliyofanya anisahau na kutojishughulisha tena na mimi wala ule ukaribu wetu. Niliumia sana lakini nilijikaza kiume, nililia kimya kimya kila nilipokua peke yangu kila nilipotoka nje nilificha maumivu yangu kwa tabasamu bandia.
Kwa chuki na hasira nyingi nilimpa pongezi na hongera za kua mjamzito, naye bila wasiwasi wowote alizipokea kwa mikono miwili. Aliniambia angefurahi sana kama angejifungua mtoto wa kiume mzuri kama mimi. Sikumjibu kitu, maumivu makubwa kama upanga mkali yaliuchoma moyo wangu, mimba yake ilinitesa kuliko kitu chochote, nilitamani kummeza lakini kila nilipoangalia kosa lake halikuepo maana mimi ndiye nilieshindwa kumueleza hisia zangu.
... Itaendelea .. .
Ilipoishia...
kila meseji niliyotuma WhatsApp aliisoma lakini hakunijibu, sikutaka kukata tamaa kwa sababu nilikua nampenda, niliendelea kumtafuta lakini cha ajabu hata nilipompigia simu hakupokea tena wakati mwingine alikata kabisa.
Songa nayo..
Kweli dunia duara yote yaliyomkuta Lucyra yalinikuta mimi, tena ilikua afadhali ya Lucyra nilikua nikimjibu meseji na kupokea simu zake, mimi simu zangu kwa Leyra hazikupokelewa na meseji hazikujibiwa kabisa ingawa alikua anazisoma. Ilikua ghafla sana sikutegemea kama Leyra angebadilika kiasi kile, kiukweli niliumia sana. Ni kama Lucyra aliniambukiza, maradhi yake yote ya mapenzi yalihamia kwangu, kwa mara ya kwanza nikaonja maumivu makali aliyokua anayapata Lucyra juu yangu hakika akikua anateseka sana.Nilikua nampenda sana Leyra pengine kuliko kitu chochote kile ukimtoa Mungu na wazazi wangu. Yeye ndie alikua mwanamke wangu wa kwanza kumpenda maishani mwangu, mapendo yote ya kipadri niliyofundishwa seminarini Don Bosco kule nchini Kenya yalikua kwake kwa sababu sikua padri, labda baadae yangehamia kwa wagonjwa lakini nilikua mwanafunzi sikua daktari bado.
Nilitamani kumpigia Leyra simu na kumfokea kwa yale aliyokua ananifanyia lakini hata ningepiga simu isingepokelewa, hata kama ingepokelewa ningemfokea kama nani yake maana hatukua wapenzi, tulikua na ukaribu mkubwa lakini hatukukubaliana kua wapenzi sababu ya udomo zege wangu.Ni kama nilikua kuzimu inayotembea duniani, hali hii ilinitesa sana kuliko kitu chochote. Kila nilipoenda nilimuwaza Leyra, iwe kanisani, uwanja wa taifa kutazama mpira au bichi kupunga upepo bado sura yake ilikatiza kwenye mzunguko wangu wa damu, nilishindwa kabisa kumsahau Leyra.
Ile miezi mitano ya likizo kwangu ilikua ni kama miaka mitano, nilitamani sana kuonana na Leyra niliamini labda ingefanya akumbuke tulivyokua. Nilijuta sana kwanini nilishindwa kumwambia Leyra hisia zangu kua ninampenda, ingawa yeye mwenyewe alilijua hilo. Hakuna marefu yasiyokua na mwisho, likizo yetu ilikua ndefu lakini mwisho wa siku iliisha. Wote tulirudi chuoni kwa furaha, kwanza kuingia mwaka wa tatu na kuanza mwaka mwingine wa masomo, pili kukutana tena na marafiki maana ni muda mrefu kidogo ulikua umepita. Chuoni nilipanga kumueleza Leyra hisia zangu kua ninampenda sana, ingawa ilikua ni kama nimechelewa maana Leyra alikua ameanza kubadilika tabia. Mwaka wa tatu ulianza, masomo yalikua magumu sana kuliko mwaka wa kwanza na wa pili. Bila kupoteza muda nilimtafuta Leyra mapema sana kabla masomo hayajawa magumu zaidi. Sikuamini nilichokiona, safari hii ilikua ni bora kuongea na Leyra kwenye simu kuliko ana kwa ana.
Leyra alikua amebadilika sana, hakupenda kuongea na mimi tena kama zamani, achana na kumshika mkono na kubusu mashavu yake muda huu Leyra hakutaka hata nimguse. Leyra alianza kunichukia ghafla, zile fursa zote adimu za kutoka out na kwenda kutembea pamoja sikuzipata tena, sikua nimemkosea lolote wala sikua nimemkubalia Lucyra lakini nashangaa kwanini alibadilika na kuanza kunichukia.
Mwaka huo wa tatu wa masomo ulikua wa mateso mengi kwangu, achana na ugumu wa masomo darasani, kutotakiwa tena na Leyra ilikua ni kama nipo jela. Nilijuta kusoma hapo chuoni Baltimore key health chuoni sio kwa sababu ni chuo kibaya hapana, ni kwa sababu uwepo wangu hapo ulifanya nikutane na Leyra, na kua mtu wa kuteseka kila siku kwa sababu yake.
Nilitamani kuhama chuoni hapo kama Lucyra ili niwe mbali zaidi na Leyra labda ingeweza kunisaidia lakini kwa bahati mbaya nilikua nimechelewa, haikua rahisi kupata uhamisho mwaka wa tatu. Furaha yote niliyokua nayo mwanzo chuoni hapo iligeuka kua huzuni, kwanini Leyra hanipendi tena?, nilijiuliza lakini sikupata majibu hasa ukizingatia sikua nimemkosea hata mara moja. Nilichanganyikiwa sana.
Ukiacha Mungu pia nina amini sana katika sayansi lakini yaliyonikuta yalifanya kwa mara ya kwanza niamini maneno ya wahenga kua ‘Chelewa chelewa utakuta mwana sio wako’. Nilijilaumu sana, msemo wa ‘Kuku wako manati ya nini’ uliniponza, nilijuta sana kwanini sikumwambia Leyra hisia zangu. Kwa mara nyingine tena niligundua ni jinsi gani Lucyra alikua akiumia juu yangu.
Mwaka wa tatu ulikua mwaka wa mwisho kwa Leyra chuoni hapo, yeye alikua anamaliza mwaka huo tofauti na mimi niliyekua nasoma miaka mitano kwa sababu ya kuchukua magonjwa mawili, magonjwa sugu ya wanawake na watoto pamoja na mifupa, wakati Leyra yeye alichukua ugonjwa mmoja tu wa mifupa.Semista ya kwanza mwaka wa tatu iliisha, ilikua maajabu, sikutaka kuamini kama kweli Leyra alikua mjamzito, niliumia sana pengine kuliko nyakati zote maisha yangu. Ujauzito wake ndio ulikua sababu kubwa ya kunichukia, sababu iliyofanya anisahau na kutojishughulisha tena na mimi wala ule ukaribu wetu. Niliumia sana lakini nilijikaza kiume, nililia kimya kimya kila nilipokua peke yangu kila nilipotoka nje nilificha maumivu yangu kwa tabasamu bandia.
Kwa chuki na hasira nyingi nilimpa pongezi na hongera za kua mjamzito, naye bila wasiwasi wowote alizipokea kwa mikono miwili. Aliniambia angefurahi sana kama angejifungua mtoto wa kiume mzuri kama mimi. Sikumjibu kitu, maumivu makubwa kama upanga mkali yaliuchoma moyo wangu, mimba yake ilinitesa kuliko kitu chochote, nilitamani kummeza lakini kila nilipoangalia kosa lake halikuepo maana mimi ndiye nilieshindwa kumueleza hisia zangu.
... Itaendelea .. .