Konyagi ya kupima Italimaliza Taifa- ni heri Kiroba kilichopigwa matufuku

MR.NOMA

JF-Expert Member
Feb 1, 2014
338
502
Wananzengo Habari za Jumapili! Natoa wito kwa Serikali hasa mamlaka husika kwa kuangalia viwango vya vinywaji na vyakula kutoa tamko haraka na kupiga marufuku kabisa biashara ya Konyagi ya kupima/ k va t ya kupima, maana hi kitu tayari watu wameanza kunyweshwa gongo na uchafu mwingine bila kujijua.Nimeshakutana na watu kadhaa wakilalamika juu ya Hilo lkn hamna mtu anayechukua hatua.Kuna jamaa alinisimulia alipimiwa toti ya Konyagi kwenye baa moja eneo la Mbezi Mwisho Baada ya kuinywa alisikia harufu ya mafuta ya taa mdomoni na baada ya dkk chache Tumbo lilianza kukatakata ilibidi awahi maziwa.Tafafhali Serikali wahusika mtusaidia kupiga marufuku biashara hii ya toti ya Konyagi/ k vant ili tuokoe nguvukazi ya taifa letu na Kama itawezekana makampuni ya vinywaji hivi yajiongeze yaje na vichupa vidogo zaidi vya ujazo mdogo Kama kiroba ili wasipoteze wateja.Point yangu ni afya za watu zipo hatarini,maana kuna wauzaji wenye tamaa,wanajaza vinywaji haram kwenye chupa za Konyagi/ K vant.Nawasilisha.
 
Uko sahihi mkuu. Kwa mstakabali wa wa taifa letu.. Kama wanataka watengeneze vichupa. Vidogo vidogo hata vya ml30 mil 50 na nk kuliko kupima wafanya biashara wengine sio waminifu watawauzia na gongo kwa kuipaki kwenye chupa za k vant, konyagi ama chupa zingine nianzofanana na hizo.
Wananzengo Habari za Jumapili! Natoa wito kwa Serikali hasa mamlaka husika kwa kuangalia viwango vya vinywaji na vyakula kutoa tamko haraka na kupiga marufuku kabisa biashara ya Konyagi ya kupima/ k va t ya kupima, maana hi kitu tayari watu wameanza kunyweshwa gongo na uchafu mwingine bila kujijua.Nimeshakutana na watu kadhaa wakilalamika juu ya Hilo lkn hamna mtu anayechukua hatua.Kuna jamaa alinisimulia alipimiwa toti ya Konyagi kwenye baa moja eneo la Mbezi Mwisho Baada ya kuinywa alisikia harufu ya mafuta ya taa mdomoni na baada ya dkk chache Tumbo lilianza kukatakata ilibidi awahi maziwa.Tafafhali Serikali wahusika mtusaidia kupiga marufuku biashara hii ya toti ya Konyagi/ k vant ili tuokoe nguvukazi ya taifa letu na Kama itawezekana makampuni ya vinywaji hivi yajiongeze yaje na vichupa vidogo zaidi vya ujazo mdogo Kama kiroba ili wasipoteze wateja.Point yangu ni afya za watu zipo hatarini,maana kuna wauzaji wenye tamaa,wanajaza vinywaji haram kwenye chupa za Konyagi/ K vant.Nawasilisha.
 
Viroba mvifungie.... mifuko ya rambo mfungie.... mnataka maskini waishije sasa ? Acha watu wale vitu bana
 
Inalipa sana sana hiyo biashara ,,ukipata location ya stand ,wapiga debe wote unawapata
 
kweli kabisa,unakuta konyagi ndogo inauzwa kwa kupimiwa hata watu wanne,sasa muuzaji si anaweza kumix na gongo@au chang'aa,tunaomba sana viroba virejeshwa kwani viroba ni salama zaidi kuliko pombe ya kupimiwa
 
Hii inaitwa Tatu Mzuka, inauzwa kwenye viosks vyote vya barabarani
Hata Magenge ya Nyanya siku hizi yanauza 3 Mzuka
Uwezekano wa kumix hizo K-vant au Konyagi na mavitu mengine ni mkubwa sana
Aidha kudhibiti nayo ni kitu kigumu labda cha kufanya ni watu wa Government waitane na Wazalishaji wa hizo products waangalie jinsi gani wanaweza kuendelea na udhibiti wa Quality at affordable prices and convenience
 
Uko sahihi mkuu. Kwa mstakabali wa wa taifa letu.. Kama wanataka watengeneze vichupa. Vidogo vidogo hata vya ml30 mil 50 na nk kuliko kupima wafanya biashara wengine sio waminifu watawauzia na gongo kwa kuipaki kwenye chupa za k vant, konyagi ama chupa zingine nianzofanana na hizo.
Watengeneze vichupa?
Unakumbuka lengo la marufuku ya viroba?
Haya ni maamuzi ya hovyo tu yalifanyika kwamba walioamua kusitisha viroba wamefeli sana

Ungesema warudishe tu viroba
 
Hivi wewe hujaona watu kwenye hoteli au bar maarufu wanakunywa pombe kama grants,whisky,black label etc za kupima
Hiyo konyagi wanazopimiwa watu ni shots tu
Acha ulimbukeni

Ova
Nimgeshangaa katibu usingejibu hoja hii...
 
Uko sahihi mkuu. Kwa mstakabali wa wa taifa letu.. Kama wanataka watengeneze vichupa. Vidogo vidogo hata vya ml30 mil 50 na nk kuliko kupima wafanya biashara wengine sio waminifu watawauzia na gongo kwa kuipaki kwenye chupa za k vant, konyagi ama chupa zingine nianzofanana na hizo.
Ina maana harufu ya gongo huijui mpaka ukajikuta kuinywa
 
Wakuu naomba niweke sawa kuwa,najua wazi Kuna pombe Kali nyingi zinauzwa kwa tots kwenye bar kubwa na mahotelini. Lkn kuhusu konyagi na K vant zinavyouzwa ovyo kila Kona na uchochoro,unaweza kuta hata kwenye genge la nyanya unauziwa shot ya konyagy Tena Ni Jero tu,sasa, Kuna Mambo mengi Sana yanatulazima imma turudi kwenye Kiroba tu au tufunge ujazo wa Kiroba kwenye kichupa.Ukiachilia mbali suala la Afya za wanywaji kuwa hatarini Kuna sababu nyingine Kama kiwanda/ wazalishaji wa pombe hizo kupata hasara kwa biashara yao kudorora kwa kuwa watu wanatumia chupa zao wanajaza mf. gongo,jick,spirit na nk wanachamganya na Konyagi na wanawapimia watu ili wapate faida zaidi, pia serikali inapata hasara kwa kushindwa kukusanya kodi kwa kila kishort Cha jero/ buku Cha konyagi.hivyo naendelea kutoa wito serikali wachukue hatua ktk hili
 
serikali haiendekezi walevi mbona husemi wavuta unga au gundi hatuna mda na upuuzi huo
 
Back
Top Bottom