Koliflawa na nyama ya kusaga

Pilipilihoho

JF-Expert Member
Jan 29, 2016
202
145
Mahitaji:

Kitunguu maji 1;

Vitunguu saumu 2;

Mafuta ya kula kikombe 4(1);

Nyama ya kusaga 1 2(1);

Vijiko 2 chumvi;

2(1)kijiko cha pilipili manga iliyosagwa vizuri;

Kijiko moja cha unga wa curry;

2(1)kijiko cha cornander iliyosagwa;

2(1)kijiko cha bizari;

4(1)kijiko cha mdalasini;

Karoti moja iliyokata nyembamba;

Viazi mviringo 2 vikatwe vipande vidogo;

Koliflawa 2(1)ikatwe vipande vidogo;

Vikombe 2 vya vitunguu vilivyopondwa;

2(1)kikombe cha maji.

Hatua:

1. Kwenye kikaangio weka mafuta ya kula na acha yapate moto wastani. Ongeza kitunguu maji na koroga kiive. Wakati unakoroga, ongeza vitunguu saumu hadi vyote vianze kugeuka rangi ya udongo iliyopauka. Angalia visiungue.

2. Weka nyama ya kusaga pamoja na viungo vingine vilivyobaki. Koroga na pika nyama hadi iwe na rangi ya udongo.

3. Weka karoti, viazi, koliflawa, nyanya na maji. Weka moto wa wastani kisha funika acha vichemke. Acha viive kwa muda wa dakika 25 hadi viazi view laini.

4. Onja na ongeza chumvi kama haitoshi. Unaweza kuweka pilipili kama unapenda.

5. Andaa wali wako na kula na sauce yako ya koliflawa na nyama ya kusaga.
20160321.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom