Wick
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 8,312
- 12,194
Wapangaji 6 wa nyumba moja mnajichanga na kununua bastola kujihami dhidi ya majambazi. Mnakubaliana kwa kuwa bwana ugoko yuko chumba cha karibu na mlango wa kuingilia basi awe analala na bastola tayari kumkabili yeyote atakayejaribu kuwavamia.
Siku bastola inapowasili toka dukani na kutua mikononi mwa bwana Ugoko, Ugoko anawaamuru wote muweke mikono juu; anawaamuru mgalegale kwenye tope la uani, mruke kichurachura na vitimbi chungu mzima.
Waliowahi kukwaruzana naye huko nyuma na wale anaowadai wanaipata 'fresh'. Halafu, huku mkiwa mmechuchumaa na mikono ikiwa juu, anawasomea marufuku nyingi sana; hairuhusiwi kufungulia radio sauti ikasikika nje, kukaangakaanga ni marufuku na sheria zingine kibao. Akawaapia kuwa yeye si mtu wa mchezo anayetaka na ajaribu aone!.
Baadhi ya majirani wamelalamika chinichini na wengine wamempongeza kuwa Ugoko ni kiboko!.
c&p
Siku bastola inapowasili toka dukani na kutua mikononi mwa bwana Ugoko, Ugoko anawaamuru wote muweke mikono juu; anawaamuru mgalegale kwenye tope la uani, mruke kichurachura na vitimbi chungu mzima.
Waliowahi kukwaruzana naye huko nyuma na wale anaowadai wanaipata 'fresh'. Halafu, huku mkiwa mmechuchumaa na mikono ikiwa juu, anawasomea marufuku nyingi sana; hairuhusiwi kufungulia radio sauti ikasikika nje, kukaangakaanga ni marufuku na sheria zingine kibao. Akawaapia kuwa yeye si mtu wa mchezo anayetaka na ajaribu aone!.
Baadhi ya majirani wamelalamika chinichini na wengine wamempongeza kuwa Ugoko ni kiboko!.
c&p

