Kinachoiponza CHADEMA sasa ni 'uchanga' wa viongozi na wafuasi wake, huishia kutukana badala ya hoja

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
16,003
Hakika ''muda hutupa majibu'' na ''uzoefu ni mwalimu mzuri''. Ukifuatilia kwa kina chanzo cha siasa za upinzani hasa CHADEMA kukosa 'consistency' hii imechngiwa kwa kiasi kikubwa na 'uchanga' wa wafuasi wake ambao wengi wanakuwa wa hujiunga pale wanapomaliza shule au vyuo kwa 'msukumo rika' na kisha baada ya muda hujikuta wameachana na siasa hasa pale wanapoanza maisha ya majukumu ya kifamilia.

Nimejaribu kufuatilia, kutokana na 'uchanga' wengi hawana uvumilivu dhidi ya hoja kinzani na huishia kutukana na kejeli na chuki isiyokuwa na chanzo, yaani unamchukia mtu sababu ana mawazo tofauti na wewe, utasikia ''hujielewi'' nk. Kawaida ya chuki ikizidi hufikia mahala hali ya kukata tamaa huja na hapo ndipo hasa wengi wa vijana hawa hujikuta wameachana na siasa za upinzani na kuwa 'neutral' au kujiunga na CCM. Ni sawa na vijana wa kidato cha pili 'hawaambiliki', wakorofi na wajuaji lakini wakishavuka hujuta na kubadilika.

Sababu kubwa ya kuwa wenye jazba hutokana na ghiliba za viongozi wanaowashawishi kujiunga na chama chao. Mara nyingi huwashawishi kwa kuwatia hasira ''tunaibiwa, mimi nikiingia madarakani nitagawa pesa bila kufanya kazi' nk nk nk..pia siasa za kudanganywa 'huyu ndiye mwizi mkuu, ndiye adui namba moja wa maisha yetu'' kisha baada ya muda viongozi hao hao huishia kumkaribisha na kukanusha waliyoyasema. Kwa muda mfupi hii imevutia wanachama ila kwa muda mrefu binadamu hujiuliza na kugundua ulaghai uliopo na kisha kukata tamaa.

Kwa sasa hata ukifuatilia mitandaoni utagundua wafuasi wakubwa wa upinzani hawajui historia za viongozi wao au washika bendera wao. Hawajui ya kwamba vyama vyao vilipata hadhi baada ya kuwadhalilisha hao ambao sasa wanaitwa 'wafalme' na kupewa kushika bendera za vyama vyao. Ndio maana siku za karibuni kambi nzima ya upinzani imegeuka na kumsifu Raisi mstaafu Jakaya Kikwete angali waliongoza kumkashifu hadi kufikia kuitisha maandamano JK asizidishe hata siku moja Ikulu, Nasema huu ni 'uchanga' na ukosefu wa historia na ndio sababu kuu leo badala ya kujenga na kujibu hoja upizani wa Tanzania umeishia kutukana na kutoa kejeli.

Muwe na Jumamosi njema.
 
Na lingine ni hawana jipya lolote, yaani sio wapinzani ni wapo wapo tu kudakua na sio kutuletea vya kuitetemesha serikali.

Kubwa zaidi wabunge wao wengi hawafanyi lolote majimboni, pesa za maendeleo ya jimbo wanaweka mifukoni...eeeeeh
 
Chadema imebaki kuwa chama cha kutafuta kuonewa huruma badala ya kuwakilisha wananchi.
Huwezi kuwa chama pinzani halafu unaleta dharau kwa serikali iliyopo madarakani..
Wasishangae ikifika 2020 wakapoteza wabunge wengi. Kuna dalili CCM imeanza kusaficha chama ili 2020 wapate wabunge wazuri.
 
Ika wale wanakula Rambirambi za watu na kuweka hadi Viongozi wa dini Mahabusu ndiyo wamekomaa kiakili.

Bowed hebu jiulize kuna Fair ground ya kufanya siasa kwa vyama.vya Upinzani??
Pesa ya Rambirambi wote wayoaji na wapewaji wameishia Mahabusu unataka Chadema wakamrambe miguu Gambo??

Mwambie Magufuli aweke fair ground uone.Hao Viongozi mnawoana ndiyo tunu ya Taifa Gambo, Makonda,Pole pole.

Angalieni hata hizo hoja zenu zimejaa matusi tu.

Wekeni Tume.huru na fair ground halafu uone.

Wenye siasa za Chuki na visasi,Ubaguzi ni UVCCM na Uongozi wake na hii mpaka Mwenyekiti wa CCM ni mwenye chuki,visasi na Ubaguzi mno.Naona Yale mapungufu yenu ndiyo mnayapeleka kwa Wapinzani.

Kwa kawaida Nyani haoni kundule.
 
Mleta mada pamoja na Cocochanel kumbe hua mnawamiss Ukawa wasipofanya siasa??!! . Mbona boss wenu ametaka wafanye siasa pekee yake?! Hamjamuuliza kwa nini anawakatalia ukawa kufanya siasa ?!

Huu uchanga na kukosa uvumilivu unaousema zaidi uko CCM na serikalini , tazama aina ya viongozi wasiona uvumilivu Bashite, Gambo nk
 
Mmi ningelikuwa nambal moja kumwita zito mnafiki kama ningemwona mpaka sasa angali chadema na lowasa aliemkashifu fisadi akiwa pale pale angetumia kauli gani kuniamnisha kama yeye c mnafiki?! Uliesema mwizi ndo unaeishi nao ndani mwako pia kama slaa angekubali kuwa pele ningethubutu kuamini upadre ulipotea njia na kutua mahali co pake Mtu ataniambia nini ili imani yang y chadem inirudie upya kama wakat wa zitto kabwe na Dr slaa?! Matusi yote yale kwa Jk leo wanasimama kumshangilia Hv kwetu cc watanzania kwenda kushot na kulia kunawez kukatokea kwa wakat mmoja!!
 
Bavicha ya sasa haihoji viongozi wao ...yaani kutwa ni kusubiri udaku kutoka kwa ajuza.


Muulize lema jengo la Machinga complex liko wapi usikie matusi
 
Sio Chadema tuu, vyama vyote pinzani Tanzania viko hivyo hivyo. Wanashidwa kutofautisha siasa na utu, unakuta unabishana hoja na mtu, anashidwa hoja anaaza kushambulia binafsi. Elimu ya vyama vingi inahitajika kama tukitaka kurekebisha hili tatizo.
 
Back
Top Bottom