Kila Mtu anaweza Kuwa Tajiri akitaka

Kila Mtu anaweza Kuwa Tajiri akitaka

Joined
Feb 7, 2015
Posts
13
Reaction score
5
Mwanadamu ni kiumbe wa ajabu sana kuliko viumbe vyote duniani,mwanadamu ni muoga sana kuliko viumbe wote duniani,mwanadamu huyo huyo akiamua kuwa jasiri, ni jasiri kuliko viumbe vyote duniani, jambo ambalo wengi wetu hatulijui ni kuwa sisi ndo tuna dhamana ya kuamua hatma ya maisha yetu, kwanini nasema hivyo?

Soma mfano huu:Charles alimwambia baba yake wakati huo akiwa na umri wa miaka 10,baba nikiwa mkubwa lazima nitakuwa tajiri na nitakutunza wewe na mama mtaishi maisha mazuri sana hapa duniani,kweli charles hadi anatimiza miaka 45 alikuwa tayari tajiri mkubwa akisaidia ndugu zake wote, Evod alimwambia mama yake kuwa, mama maisha yetu ni dhiki tu kila siku sidhani kama tutakuja kufanikiwa,

kweli hadi sasa Evod ana miaka 49 maisha yake ni dhiki tu,anaishi kwa kuombaomba na kula yake ni ya shida sana,we're the fate of our destiny,kila upangacho lazima kiwe hapa duniani,maneno yetu ndo yanaumba hatma ya maisha yetu,kinywa huumba uzima na mauti,utakalo wewe leo ndo litakutokea kesho,kauli huumba,kila mmoja na aelewe.
 
Asante sana kwa ukweli huu, laiti watu wangejua!
 
Sawa na mtoto umpe jina la Shida. Atakuwa na shida mpaka roho itengane na mwili
 
Baba nikifikisha miaka 40 nitakua Bill Gates mpya wa dunia.. nitasafiri kwenda fukwe za Copa Cabana kila weekend kula maisha, nitasaidia wenye maisha magumu na shida mbalimbali. Nitakinunua chama chote za mafisadi CCM na kukisambaratisha... Amen
 
wengi walisha kua na ndoto za kuja kuwa matajiri lakini mpaka leo ni bila bila maisha ni bahati pamoja na akili ya mtu
 
Hayo maapizo ya utajiri bila usimamizi(utotoni) na kuyaishi na kufuata njia za kuwa tajiri HUTAUONA HUO UTAJIRI KAMWE.
 
wengi walisha kua na ndoto za kuja kuwa matajiri lakini mpaka leo ni bila bila maisha ni bahati pamoja na akili ya mtu
Bado unaamini kwenye bahati mkuu, hata hao unaoona wana bahati ni kutokana na walijaribu kufanya jambo flani kwa ujira mdogo ila kwa kukutana na watu mbalimbali ndipo walipokutana na mambo mazuri ambayo wewe unaita bahati wakati ukweli ni utaratibu tu wa maisha kuelekea kwenye mafanikio.
 
Hakuna linaloshindikana kwake yeye mwenye kuamini...
 
Chochote upandacho ndicho utakacho vuna.

Mauti na Uzima vimo midomoni mwa MTU, imani huona mbali kwa Imani Ibrahim alihesabiwa haki kuwa Baba wa mataifa, kwa imani Henoko hakuonja mauti, Kwa imani Hanna alipata mtoto Samwel, Mdomo huumba maana kinywa hunena yaujazayo moyo,

Ujana umejaa maono na matarajio mengi kijana akiona baba ake ana nyumba ya nyasi yy huona nyumba ya vigae hata kama hakijui kigae kinatengenezwa wap.

Hiyo ndo imani siku zote ukijijengea kushindwa huwezi fanya chochote maana utaogopa kushindwa, kumbuka mkulima hufungia mbegu kwenye tundu la aridhi hata kama ndani hamna chakula maana huamini zitaota na kuzaa sana
 
wengi walisha kua na ndoto za kuja kuwa matajiri lakini mpaka leo ni bila bila maisha ni bahati pamoja na akili ya mtu
Mkuu usiamini katika bahati, kwani tafsiri ya neno bahati kama alivyo tafsiri muigizjaji wa filam Denzel Washington 'Bahati ni mandalizi yanapo kutana na fulsa' Hivyo bahati ni kwa wapambanaji watafutao wavitakavyo.

Pia mwandishi wa vitabu Walph Wado alienda mbali zaidi na kusema Mwanaume jasiri hamimi katika bahati ila hutafuta akitakacho bila kuchoka mpaka anapo kipata.
 
Lakini unayukumbuka maneno yaliyoandikwa kwenye bible, pale Yesu Kristo aliposema kuwa chances za tajiri kuuona ufalme wa mbinguni ziko so slim mithili ya ngamia kupenya kwenye tundu la sindano?

Unakumbuka pia kwenye bible hiyo hiyo, ambapo yule masikini Lazaro alipokufa alikwenda moja kwa moja kwenye ufalme wa mbinguni na yule tajiri alikwenda jehanum?

Alipotoa mfano ule Yesu Kristo na kumwambia yule kijana kuwa kama anataka kuuona ufalme wa mbinguni, kwanza akauze mali zake, halafu mauzo hayo akawagawie masikini, ni kwa kuwa alikuwa anajua kuwa mtu yeyote anapofikia level ya utajiri, anakuwa siku zote hatosheki na mali alizochuma na wakati wote matajiri wanaaim kupata super profit kutokana na biashara wanazozimiliki.
 
Mi naangalia tu hekima za matajiri kuwaona maskini ni wazembe wakati hao matajiri hawataki kuona maskini anainuka. Wapo tayari hata kuua.
 
Back
Top Bottom