Kikwete: Ipo misikiti mitatu jijini Dar-es-Salaam ilinisomea itikafu ili nife!

Status
Not open for further replies.
Kama hata walio wako nao wanakukana basi ujue wewe ni tatizo!
Maana ata wakristu wanalalamika na wa upande wako wanakuombea UFE sasa uko upande upi?
 
Kama wanampinga tu kwa udhaifu wake wanaitwa Wadini na wakabila na wenye wivu wa kijinga.
Je wanapanga kumuua wao waitweje?.......

Changanya na Mchuzi wa nazi, usipopata jibu weka maji ya betri.
 
Yaani watu wa humu JF siwaslewi kabisa! Sijui ni mazuzu. Yaani rais akisema kuwa kuna jambo fulani baya wananchi wanamtendea basi wanamwita dhaifu, hivi mnaakili lakini? Kwamba yeye asiseme analolichukia ama linalomuumiza? Ndio lazima awe dhaifu mbele ya wananchi wake walio wengi, nyinyi humu mkifika kwa wake zenu hamuwezi kusema neno, tena unshindwa mbele ya mwanamke. The president is Kind kama kuwa kind ni udhaifu basi bora aendelee kuwa dhaifu! Wengine wanasema si bora angewashuhulikia, wakimaanisha kuwakamata ama kuwapiga, kwa kuwa ni waislam ndo awakumute? Izo chuki zenu ndio zitaipeleka Tz pabaya kwa kutotumia akili zenu.
Pia mkae mkijua tu sio kwamba kila itiqafu itafanya kazi tu, Mungu ni muadilifu, akiona kuwa nichuki tu za kawaida basi itiqafu haitotenda haki. Tujiulize kwanini misikiti mitatu tu? Tanzania kuna misikiti mingapi mikubwa? Je hiyo itiqafu ni makubaliano ya waislam wooooote? Wakiwemo maimamu wakubwa? Pia msisahau kuwa, katika kila sala ya ijumaa basi misikiti inamuombea dua njema rais!
 
kabisa,lazima serikali iache kuwalegezea kamba hawa watu.yaani mtu anatamani kuwa rais hadi anaamua kuvuruga nchi ilimradi walioko madarakani waonekane hawafai,yaani yeye hiyo ndo anaona ni njia ya kujipatia kura nyingi hapo 2015.

Anatumia viongozi wa dini kutoa matamko kila siku kama kile kipindi cha kuelekea general election 2010.

This has to come to an end either kwa hiari au kwa lazima.
 
Hawa wasoma Itiqaf wakamatwe na kuhojiwa mbele ya sheria maana ipo siku wataweza kuingiza mamluki wakigaidi kutoka nje ili wamdhuru rais wetu.
 
Mbona Kova hajawakamata kwa makosa ya ugaidi ya kupanga kumuua Mh Rais ,IGP na yeye mwenyewe?
 
Kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi nimemsikia rais JMT Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisema "Kuna misikiti mitatu ili kaa itikafu ili mimi, kamanda wa polisi Sulemani Kova na Saidi Mwema ili tufe".

Nimemsikitikia sana JK na kumuonea huruma alipokuwa anatoa kauli hii. Kwa kauli ya JK na mambo mengine aliyo yaelezea kuhusu mizozo ya udini napigia mstari kuwa Tanzania ina tatizo kubwa linachemka kuliko wengi wetu tunavyo dhani, kilicho nisikitisha zaidi nikutokuonyesha njia ya kutatua matatizo hayo, nimemuona raisi kama vile naye ana lalamika kama wananchi na waumi wengine wanavyo lalamika.

Tuna safari ndefu yenye milima na mabonde mengi.

Haihitaji elimu yeyote kujua JK is not a doer na sana sana ni Raisi anayekwepa majukumu. Pale ambapo alipaswa kuact yeye anakimbia. Angalia

1. Swala la Buseresere amesema walimalize wenyewe. Anasema mbona kabla ya mwanzo walikuwa wanakaa pamoja? Ukiangalia kwa makini ni kama vile anatoa jibu la maana, kwamba kama walikaa pamoja wanaweza kuyamaliza wenyewe. Ukiangalia mtifuano ulioendelea pale na kauli zilizotolewa na viongozi utagundua kuwa hawawezi wakayamaliza wenyewe.

2. Pamoja na kuona umuhimu wa kukaa na viongozi wa dini, ameamua kumwachia Waziri mkuu akutane na viongozi hao. Anajuwa kuwa kwa sasa haaminiki na wakristo na waislamu. Huyu ni raisi ambaye tukio la juzi la ghorofa limesisimua mpaka amepanga lunch/dinner na timu ya waliokuwa wanabeba vifusi. Huyu ndiye raisi ambaye ni mwepesi wa kuhidhuria vifo vya wasanii na kupiga picha nao ikulu. Lakini kukaa na kuamua jambo la msingi kama la udini ameamua kumwachia PM. Huku ni kukimbia tatizo.

3. Anasema tujiulize nini kimetokea mpaka sasa tumefika hapa wakati tulikuwa tunaishi vizuri? Anakwepa majukumu. Nadhani angejiuliza, mbona toka nimeingia haya yamezidi? Kumbe, angepata jibu tayari
 
Mkuu, mimi nimesoma hiyo hotuba yake sikuamini maneno hayo.

Nilijiuliza hivi waandishi wa habari hawakuona hayo maneno?Nilitarajia wangeyapa uzito.
you are very coreect, jamaa ni mzushi tu hakuna fact yoyote aliyoitoa kimuondolea kasha ya udini. Wote tunaijua mikanda ya kutangaza mauaki ya kidini na imekiwa ikiuzwa tena hadbarani na hatukawahi lusikia aliteandaa mikanda hiyo, SHEIKH ILUNGA alikamatwa lwanini tusiamini kuwa huyu jamaa ni msanii tuu.
 
jk tenga mda uisome dini yako..itakusaidia kufanya yale yatakayokufaa baada ya kutoka duniani...sasa hadi itikaf hujui ni kitu gani...huu si mswiba??
 
Very simple, kwanza Kikwete mwenyewe ni mshiriki, pili hao anaodai kumwombea iti-cuf aliwatumia na aliwaahidi mahakama ya kadhi, nchi kujiunga na OIC pamoja na makandokando mengine ili wampigie kampeni misikitini au hadharani huku wakifanya kampeni chafu dhidi ya CDM, kulitukana kanisa na kumkejeli na kumtusi baba wa taifa Mwl. Nyerere. uchaguzi ukapita Kikwete "akashinda". 2011, mihadhara yenye kibali cha serikali chini ya ulinzi wa jeshi la polisi ikaendelea nchi nzima ikianzia Diamond jubilee chini ya mwamvuli wa kile kinachoitwa jukwaa la katiba la waislam likiongozwa na sheikh Mohamed Issa, Basaleh, Amir Kundecha, Ponda Issa Ponda na masheikh kutoka mikoa yote bara na visiwani, yakatolewa maazimio kadhaa na kauli kali zenye kuogofya kama "KUFA KUPONA TUTAHAKIKISHA UKATOLIKI UNANG'OKA MIZIZI YAKE TANZANIA". Kwa kauli kama hiyo ungetegemea wahusika wangechukuliwa hatua kali na mihadhara ya namna hiyo ingepigwa marufuku, lakini serikali ya CCM chini ya Kikwete iliruhusu mihadhara hiyo ya kashfa kuendelea nchi nzima bila kificho huku polisi wakiilinda! (nilipata bahati ya kuhudhuria miwili).

ILIKUWAJE KIKWETE ASOMEWE ITIKAFU?
Ktk sherehe za Idd el fitri ya mwaka 2011 iliyofanyika Dodoma, Kikwete aliwaambia waislam kuwa, mahakama ya kadhi anzisheni na mgharimie wenyewe. Kauli hiyo iliamsha munkari kwa masheikh waliokuwa wametumika kuhubiri chuki dhidi ya wapinzani wa Kikwete kwenye uchaguzi wa mkuu wa 2010. Sheikh Mohamed Issa alihamaki na kusema " Kikwete wewe kwa hili unatofauti gani na padre Slaa ambaye tulizunguka nchi nzima asiigie ikulu ili wewe ( Kikwete) uendelee kutawala?" aliyasema kwenye msikiti wa Idrisa.( zipo cd zenye hotuba hizo).

Nakubaliana kwa dhati kabisa na wale wanaosema kuwa Kikwete ni ndumila kuwili, wengine wanasema usipange naye dili atakugeuka.
Watanzania tuna bahati mbaya sana kuwa na rais asiyekuwa na msimamo hata kwenye mambo ya msingi, hata hivyo hili liwe ni fundisho, na tujifunze, tusirudie kuwa na rais wa namna hii. Lawama zote kwa CCM kutuletea mtu wa namna hii wakaacha kutuletea mtu makini kama Dr. Salim ambaye alichafuliwa na mtandao wa Kikwete mwaka 2005.
ANGALIZO; Siyo CCM mjidanganye kumsimamisha SAS, 2015, zama zake zimeshapita zamani!.

CCM NA SERIKALI YAKE CHINI YA KIKWETE, MMELIKOROGA KWA MANUFAA HARAMU YA MUDA MFUPI, SIMAMENI KWENYE MAJUKWAA MKIRI MAKOSA YENU, MUWAOMBE RADHI WATANZANIA. WATUMIENI WALEWALE MLIOWATUMIA WAPITE KOTE WALIKOPITA WAJARIBU KUNG'OA MBEGU CHAFU WALIZOPANDA. KAMA MLIWEZA HATA SASA MTAWEZA INGAWA HAMUAMINIKI TENA.
 
Kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi nimemsikia rais JMT Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisema "Kuna misikiti mitatu ili kaa itikafu ili mimi, kamanda wa polisi Sulemani Kova na Saidi Mwema ili tufe".

Nimemsikitikia sana JK na kumuonea huruma alipokuwa anatoa kauli hii. Kwa kauli ya JK na mambo mengine aliyo yaelezea kuhusu mizozo ya udini napigia mstari kuwa Tanzania ina tatizo kubwa linachemka kuliko wengi wetu tunavyo dhani, kilicho nisikitisha zaidi nikutokuonyesha njia ya kutatua matatizo hayo, nimemuona raisi kama vile naye ana lalamika kama wananchi na waumi wengine wanavyo lalamika.

Tuna safari ndefu yenye milima na mabonde mengi.

Mkuu Mohamedi Mtoi
Wala hapaswi kuonewa Huruma kwa Mbegu aliyopipanda Mwenyewe na CCM yake.
Anatgemea kuvuna Pili pili kwa Kupanda Mpunga.
JK ni mnafiki na anatuzuga tu, Mkuu wala hatuna Sfari Ndefu.
2015 ndo mwisho wao
 
Last edited by a moderator:
Aliyeua kwa upanga nae atakufa kwa upange..waliingia kwa gia ya udini, sasa udini unatutafuna.
 
Mbona Kova hajawakamata kwa makosa ya ugaidi ya kupanga kumuua Mh Rais ,IGP na yeye mwenyewe?

Aliyoyasema rais ni fake......anatafuta sympath tu na kuonyesha kwamba hata wenzake hawampendi kiasi kwamba wanataka kumuua.

This is ridiculous!... Jambo aliloliongea ni jambo zito, sio jambo la mchezo. Linahusu rais kuuwawa. Haijalishi ni kwa juju au kwa sala za maruhani au sala kwa mungu.
 
Lakini to the contrary, mimi ningemuuliza swali moja jepesi kuhusu ukristo na upendo.

Kwanini Yesu alipoombwa chakula na yule mama mkananayo alimjibu hivi?

'Siwezi kuchukua chakula cha watoto na kuwapa mbwa' Kweli huo ndio upendo?

Ukipigwa upande wa kushoto geuza na kulia.

Yesu hakumnyima chakula mtu wewe, omba uelezwe utajulijwa. Yeye alitoa mfano sio kwamba aliombwa chakula halisi.

Kwani wewe mwenye upendo sana kwa waislamu na wasio waislamu, chakula cha wanao unawapa mbwa?
 
Haihitaji elimu yeyote kujua JK is not a doer na sana sana ni Raisi anayekwepa majukumu. Pale ambapo alipaswa kuact yeye anakimbia.

3. Anasema tujiulize nini kimetokea mpaka sasa tumefika hapa wakati tulikuwa tunaishi vizuri? Anakwepa majukumu. Nadhani angejiuliza, mbona toka nimeingia haya yamezidi? Kumbe, angepata jibu tayari


Asema tujiulize ni nini kimetokea?!? Eboo, sisi tunajua hatuhitaji kujiuliza. Watanzania walifanya kosa la kutomsikiliza Nyerere na kumchagua kuwa raisi wa nchi hii ndio ndio maana hatuishi vizuri tena. Yaani hilo kwake ni gumu kuliona?
 
Yesu hakumnyima chakula mtu wewe, omba uelezwe utajulijwa. Yeye alitoa mfano sio kwamba aliombwa chakula halisi.

Kwani wewe mwenye upendo sana kwa waislamu na wasio waislamu, chakula cha wanao unawapa mbwa?

Umeingia chaka kijana nenda ukajifunze! Utaijuaje biblia wakati huwa unapangiwa vya kusoma?

Unajua kwa nini Yesu alimfananisha yule mama na mbwa badala ya kumpa tu?

Usitoke mapovu, ukiujua huu -- huu huujuwi!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom