Kikwete awakopa wananchi chakula.

chankaka

Member
Joined
Mar 14, 2013
Posts
16
Reaction score
12
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Rais kikwete amekiri kuwakopa wanchi hasa wa wilaya ya Ludewa mazao yao ya chakula ( mahindi) na kuahidi waendelee kusubiri kwani serikali haina fedha za kuweza kulipa deni hilo. Mpaka sasa serikali inadaiwa Tshs. bilioni 27 za mazao hayo. na ameahidi kulipa sh. 10 bilioni tu. Hii inadhihirisha kauli ya Mnyika ya mwezi april ya udhaifu wa Rais Kikwete kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake.
 

yaani wewe Chankaka jinsi unavyoshindwa kushirikisha akili yako? nakushangaa sana. hivi kwa akili yako Ludewa pekee wana uwezo wa kuzalisha mahindi na kuwakopesha serikali ya bilioni 27?
 
halafu hujatuambia kama hayo mahindi amekopa kama JK au serikali ndo imekopa. na baada ya kukopa, hayo mahindi yamepelekwa wapi? yaani nimekudharau kupita kiasi.
 
halafu ukiona unaanzisha udaku hata wenzako hawakuungi mkono basi jua kuwa unaandika upuuzi
 
wenzako wanahangaika kuimarisha chama, wewe unahangaika na JK. yaani una tabu sana ndugu. basi uwe unapost vitu vyenye tija kwa chama chako na si uongo, uzushi, uzandiki na fitina
 
Ni aibu kwa mwanaume kupenda kusutwa daima
 

Hayo maneno ya Rais yana uhusiano gani na matusi ya MNYIKA kama siyo kudhihirisha MNYIKA kama kiongozi asivyo na busara wala hekima.
 

Ulitaka akane badala ya kikiri? JK siyo dikteta wewe, issue ya Serikali kudaiwa na wananchi wake wala siyo kwa Tanzania pekee labda kama upeo wako unaishia Tanzania pekee. Mbali na serikali kukosa pesa ikumbukkwe pia kuwa malipo ya fedha za serikali yana taratibu zake.
 

Wewe utakuwa Michael AWEDA, chapa kazi kaka uchaguzi wa chama unakaribia labda utaambulia kitu.
 
Yaani anakopa hadi msosi, si angeomba wampe msaada tu!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…