GE2025 Kesi ya Lissu: Mahakama Kuu kutoa uamuzi mdogo Septemba 22

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mwizukulu wa Buganda

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2024
Posts
638
Reaction score
1,771
Mahakama Kuu Masjala ndogo ya Dar es Salaam imepanga kutoa uamuzi mdogo kwenye kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu Jumatatu ya tarehe 22 Septemba 2025.

Uamuzi huo unakuja kufuatia Lissu kuweka mapingamizi yaliyokuwa yanahusiana na ubovu wa hati ya mashtaka pamoja na maelezo ya mashahidi (witness statement) kuchukuliwa kinyume cha sheria na pia yapo maelezo ya mashahidi ambao mahakama ilisema utambulisho wao ufichwe wameshindwa kufanya hivyo.

Lissu aliwakilisha mapingamizi hayo mara baada ya kusomewa mashtaka, kufuatia kutupiliwa mbali pingamizi lake la awali juu ya mapungufu ya kisheria yaliokuwa kwenye Committal process, iliyosomwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Pia soma
- GE2025 - Lissu: Naomba Mahakama kesi yangu irushwe mubashara ili kuondoa tatizo la wanachadema kupigwa nje ya Mahakama
 
Utashangaa Majaji kwa sababu ya maagizo kutoka juu watapindisha sheria, huku ukweli ukiwa uko wazi kabisa kuhusu hati ya mashtaka kukosewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…