Kenya waache utoto, Wasitengeneze kisingizio cha machafuko mengine ya Uchaguzi wa Mwakani

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
6,067
10,936
KENYA WANATENGENEZA KISINGIZIO KWA MACHAFUKO MENGINE YA UCHAGUZI WAO WA MWAKANI

0fgjhs8ebvtb4n8qo.85699cfb.jpg


TUHUMA za Mbunge wa zamani wa Jimbo la Starehe jijini Nairobi Kenya, Maina Kamanda kuwa Rais John Pombe Magufuli na Rais Salva Kiir wa Sudan ya Kusini wanamfadhiri Raila Odinga kuhochea vurugu Kenya ni upuuzi na kichekesho cha karne.

Ni ushauri wa bure kwa ndugu zetu wa Kenya wawe wanachagua viongozi wenye historia. Maina ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP) cha Kenya, alipata kuwa meneja msaidizi wa hoteli jijini Nairobi.

Wakati wanachinjana tangu uchaguzi wao wa 2007 na ule wa March 2013 hadi watu zaidi ya 1,200 wanauawa, Magufuli na Kiir walihusika? Huyu Maina simwelewi kabisa.

Kenya huwa wanachinjana katika kila uchaguzi. Sasa hivi, wanajaribu kutengeneza kisingizio cha machafuko ya uchaguzi wao wa mwakani. Bahati mbaya ni kisingizio cha kitoto.

Huko ICC Kenyatta na Ruto walipelekwa kwa sababu gani? Wakati JK alipokwenda kuwapatanisha baada ya Uchaguzi wao mkuu wa 2007, wakaanza kutwangana, Magufuli alikuwa Rais wa Tanzania?

Waache visingizio vya kitoto. Huo ni usanii mtupu. Watatue matatizo yao wenyewe wasianze ujinga wa kutuingiza kwenye kushindwa kwao. Labda wangekuwa wastaarabu waombe tuwapatanishe.

Mandela aliwahi kusema, "Maadui wako sio lazima wawe maadui wangu." Hii ni mbinu ya kitoto ya kujaribu kufanya Raila Odinga abaguliwe na watu wanaomheshimu. Ni mbinu mbovu isiyozingatia taratibu za kidiplomasia na inayotishia mustakbali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Lakini pia inaweza kuwa hasira zakukosa tenda ya ujenzi wa bomba la mafuta na ujenzi wa reli ya Rwanda kuunganisha na njia ya Tanzania.

MwanaJF.
 
Inawezekana wametumia kigezo cha urafiki wao
Si unakumbuka jamaa alivyokua mapumzikoni chato jamaa alimtembelea na akakaa haswa wakizungumza
 
Mi ni mtanzania lakini ukweli sijui chochote inawezekana ikawa ni kweli ama si kweli so tuweke akiba ya maneno, kama nyie hampendi maandamano tanzania kwanini mnataka kenya yatokee? Kama magu anamsapoti odinga mimi na wewe hatujui wamekutana wamekaa siku tatu unafikiri walikuwa wanaongelea nini? Au unahisi walikuwa wanacheza game la fifa? You never know huyo aliesema ana ushaidi kiasi gani
 
Hayo ni ya wakenya tuwaachie wenyewe, ni kama wagombea wa marekani wanavyoisema China ili kuomba kura kwa wamarekani, kwa hiyo na wakenya huenda wameichagua Tanzania kama punching bag la kupatia ushindi hivyo sisi tukae kimya kama china
 
Kumekuwa na tetesi kwamba Tanzania inaingilia mchakato wa uchaguzi wa Kenya. Hii imehusishwa na ziara za mmoja wa wanasiasa wa Kenya ambaye inadaiwa anazunguka kutafuta pesa na uungwaji mkono.

Uchaguzi huu unafuatiliwa kwa Karibu na mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai na ni wazi hata makachero wa ICC na wa Kenya pia watakuwa wanafuatilia nyendo za mwanasiasa huyo ambaye Mugabe alimtuhumu moja kwa moja.
Tayari kuna viashiria vya machafuko Kenya, na endapo mkono wa Tanzania ukionekana,bila shaka ICC itatoa tamko au hata kuchukua hatua..

Chonde chonde tuwaache wakenya waamue watakacho
 
Mbona hukutoa tamko kama hilo kuwa Kenya isiingilie uchaguzi wa Tanzania uliopita????!!!!!
 
Kumekuwa na tetesi kwamba Tanzania inaingilia mchakato wa uchaguzi wa Kenya. Hii imehusishwa na ziara za mmoja wa wanasiasa wa Kenya ambaye inadaiwa anazunguka kutafuta pesa na uungwaji mkono.

Uchaguzi huu unafuatiliwa kwa Karibu na mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai na ni wazi hata makachero wa ICC na wa Kenya pia watakuwa wanafuatilia nyendo za mwanasiasa huyo ambaye Mugabe alimtuhumu moja kwa moja.
Tayari kuna viashiria vya machafuko Kenya, na endapo mkono wa Tanzania ukionekana,bila shaka ICC itatoa tamko au hata kuchukua hatua..

Chonde chonde tuwaache wakenya waamue watakacho
Hivi mwanasiasa apewe pesa ambazo ni kodi zetu halafu atatulipa nini? Au alitukopesha?
 
  1. ICC watakula kichwa
Wakenya wenyewe hawaitaki ICC wao na bunge lao na wananchi wao.Hawana mpango na ICC na ndio wanafanya kampeni kubwa nchi zote za Africa zijitoe ICC unaota!!!!

ICC haina meno kwa maswala ya kenya
 
Back
Top Bottom