Hahaha! Mbona bado naona means tested?
H
Hahaha! Mbona bado naona means tested?
Swali lako linanifanya niendelee kuamini kuwa To lead Tanzanian is very simple task,And that is what Magu is doing right now.
Kwanini nasema hivi,watanzania tunapenda kuishi kwa matukio,yaani tukio likitokea tunashabikia alafu waziri au kiongozi akitoa tamko tunashabikia bila kufanya critical analysis(utafiti).Then baada ya muda ndio tunagundua madhaifu ya tamko then tunaanza kulalamika.Hii ndio Tanzania
Swala la wanafunzi wachache kutopata mikopo limekuja,watanzania wakapiga kelele means tested iondolewe,Waziri akajitokeza akasema ameiagiza bodi irudishe 8500 kwa wanafunzi wote(Unajiuliza Je waziri alikuwa hajui kuwa means tested ipo?? au wakati bodi wamekuja na huo utaratibu,hawakumwambia waziri?? Je kama siyo wanafunz kulalamika,waziri angetoa tamko lake??)
Lkn kubwa zaidi,Wazir amesema kwenye tamko lake means tested itaondolewa muhula wa kwanza peke yake,then mihula inayofata means tested iko palepale(yaan hapa waziri alitoa temporary solution) badala ya kutoa permanent solution.
Wazir alitoa utatuzi wa muda tuu badala ya kutoa utatuzi wa muda mrefu
Tatizo linakuja sasa,watanzania kama kawaida tuliishia kumpongeza waziri kwa mapambia na nyimbo na vigelegele lukuki
baaba ya muda mfupi,tukigundua kuwa means tested haijaondolewa tunaanza tena kulalamika.Watanzania hatujui kuhoji wala kudadisi tamko likitolewa,sisi kazi yetu ni kusifu tuu.Unasifu na kupiga vigelegele wakati ni wajibu wa serikali kutoa mikopo!Hii ndio Tanzania
Anzeni tena kulalamika,Huenda waziri akasikia na atakuja na Tamko
Ngachoka!