Wakubwa,
Hivi kati ya software developer na software engeneer ni kipi kizuri kusoma na faida zake ni zipi!?
Software Engineer ni software developer, lakini si Kila software developer ni software engineer.
Software Developer ni mtu yeyote yule anaeandika code kwa ajili ya kutengeneza program.
Software Engineer ni mtu anaefuata standards zilizopitishwa Kwa ajili ya kutengeneza mifumo.
Kwa hivyo engineer inahusisha kufuata standards.
Kizuri kusoma ni Software Engineer Kwa sababu utakuwa unatengeneza mfumo ambao unafuata standards.
Nini faida ya kutengeneza mfumo unaofuata standards?
1. kutengeneza mfumo ambao ni rahisi kuuboresha (Maintainability). Kila kukicha mifumo inahitaji maboresha hivyo ni vyema kutengeneza mfumo ambao ni rahisi kuuboresha.
2. Kutengeza mfumo ambao ni rahisi Kwa wengine kuuelewa. unaweza kuwa umeajiliwa na kampuni Fulani lakini kesho haupo hapo. Hivyo ni vyema kuwa na mfumo ambao hata akizisoma code mtu mwingine basi iwe rahisi kuuelewa.
Mfano kwenye mfumo wako umetumia Model View Controller (MVC) ni rahisi mtu kujua package hii itakuwa inafanya kazi Fulani
3. Kutengeneza mifumo imara na yenye efficient kubwa Kwa nguvu kidogo. Mfano mzuri ni google kuanzisha view model kwenye android development. inarahisisha maisha ila pia ni effective.