Mwaka 2017 nilikuwa na kinissan x-trail kilikuwa kichefuchefu balaa!, kuna siku nimeenda bar kupata kinywaji nikavuta pisi kali moja nikajilie mema ya nchi ile nimeingia kwenye gar niliwashe tuende lodge flan likagoma kabisa kuwaka wakati huo lilikuja linatembea, hapo sikuwa na namna nikadaka tax chap gari langu nikaliacha hapo, ile narudi nitest tena likagoma tena kuwaka nikampigia fundi akaja ile kuwasha ni jino moja likawaka nikaishia kumlipa pamoja na usumbufu kibao, baada ya miezi kadhaa nikamshikisha jamaa flani likaja mtesa lile gari mpaka leo hatusalimiani na yule jamaa kisa kumwuzia msala, kwakweli stress za gari zisikie tu.