kambagasa
JF-Expert Member
- Aug 18, 2014
- 2,271
- 1,809
Habari zenu wadau, Katika mkoa Shinyanga Kahama jirani kabisa na Kakola kuna kata ya Bugarama ambayo kwa kila dali awamu hii lazima ichukuliwe na UKAWA. Picha lenyewe liko hivi; Katika uchaguzi uliopita wananchi waliionyesha CCM kuwa wao si mburura tena baada ya kijiji cha Ilogi kutetewa na CHADEMA huku Bugarama CCM na CHADEMA kugawana vitongoji nusu kwa nusu kwa mara ya kwanza tangu vyama vingi.
WATIA NIA WA CCM
Watia nia wa CCM ni kichekesho kwani wengi ni watuhumiwa wa kuifilisi SACCOS kubwa ya IBUKA kabla hawajaitelekeza na kukimbilia kuwania udiwani huku wakielekeza mashambulizi kwa diwani anayemaliza muda wake na huku akiwa ametangaza nia tena huku akiugwa mkono na kijiji anachotokea tu (BUYANGE). Kichekesho kingine ni watia nia kutoka vijiji vya Bugarama,Igwamanoni na Ilogi ambao kama kuna watu wanawaunga mkono basi ni waganga wa jadi na wachawi huku kundi kubwa la vijana ambao wamejiandikisha kwa wingi wengine wakijiandikisha wakitokea Kakola ambayo ni ngome ya UKAWA wakimpigia upatu bwana Izengo wa CHADEMA kama chaguo lao. Kuna kijana mmoja wa CCM ambaye sitamtaja alikuwa ametangaza kugombea kwa kupitia CCM nasikia ameandika barua ya kujitoa katika ulingo kwa kutishiwa kulogwa na hao wazee wanaotaka udiwani kwa tiketi ya CCM. Msiulize nimezipata wapi kwani nilikuwa huko kabla sijarudi kwangu Bariadi.
WATIA NIA WA CCM
Watia nia wa CCM ni kichekesho kwani wengi ni watuhumiwa wa kuifilisi SACCOS kubwa ya IBUKA kabla hawajaitelekeza na kukimbilia kuwania udiwani huku wakielekeza mashambulizi kwa diwani anayemaliza muda wake na huku akiwa ametangaza nia tena huku akiugwa mkono na kijiji anachotokea tu (BUYANGE). Kichekesho kingine ni watia nia kutoka vijiji vya Bugarama,Igwamanoni na Ilogi ambao kama kuna watu wanawaunga mkono basi ni waganga wa jadi na wachawi huku kundi kubwa la vijana ambao wamejiandikisha kwa wingi wengine wakijiandikisha wakitokea Kakola ambayo ni ngome ya UKAWA wakimpigia upatu bwana Izengo wa CHADEMA kama chaguo lao. Kuna kijana mmoja wa CCM ambaye sitamtaja alikuwa ametangaza kugombea kwa kupitia CCM nasikia ameandika barua ya kujitoa katika ulingo kwa kutishiwa kulogwa na hao wazee wanaotaka udiwani kwa tiketi ya CCM. Msiulize nimezipata wapi kwani nilikuwa huko kabla sijarudi kwangu Bariadi.