Daniel Mbega
JF-Expert Member
- Mar 20, 2013
- 338
- 180
LENGO la kupunguza nusu ya watu wanaoishi katika umaskini na njaa nchini Tanzania na kuwafanya wawe katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 linaweza kuhatarishwa na ongezeko la idadi ya watu, zaidi katika maeneo ya vijijini.
Hali hiyo, ambayo ni pigo kwa mikakati ya Taifa ya kupunguza umaskini kama inavyoainishwa kwenye Awamu ya Pili ya Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA II) pamoja na Dira ya Taifa ya Maendeleo kuelekea mwaka 2025, inatokana na kasi kubwa ya ongezeko la watu nchini ambayo haiendani na mipango mingine ya maendeleo.
Kwa habari zaidi, soma hapa => Kasi ya uzazi mzigo mkubwa kwa uchumi wa Tanzania | Fikra Pevu