Kaseja awapa Yanga masharti mawili

Kaseja awapa Yanga masharti mawili

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,685
kaseja.jpg


DAR ES SALAAM.

KIPA Juma Kaseja yuko tayari Mkataba wake Yanga SC uvunjwe iwapo klabu hiyo haitatekeleza mambo mawili, moja kuanza kumpa nafasi za kudaka katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Kupitia Meneja wake, Abdulfatah Salim, Kaseja ameipa masharti Yanga SC kama inataka kubaki naye immalizie dau lake la usajili Sh. Milioni 20 na pia kuanza kumpa nafasi ya kudaka.

Kwa sasa, kipa huyo namba moja wa zamani wa Tanzania, hana nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Yanga SC chini ya kocha Mbrazili, Marcio Maximo, tofuti na ilivyokuwa chini ya kocha aliyetangulia, Mholanzi, Hans van der Pluijm alikuwa anadaka kwa zamu na Deo Munishi.

Abdulfatah ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, katika Mkataba wao walioingia na Yanga SC, walikubaliana kukamilishia malipo ya mwisho ya dau la usajili ya (Sh Milioni 20) ifikapo Januari 15, mwaka huu, lakini klabu hiyo hadi sasa haijafanya hivyo.

Amesema wakati wanavumilia hilo, bado mteja wake hana nafasi kwenye kikosi cha kwanza jambo ambalo ni hatari kwa kipaji cha kipa huyo.

Abdulfatah amesema kwamba wanayaingiza masharti hayo yote kwa maandishi na kuyapeleka kwa uongozi wa Yanga SC uyatekeleze, vinginevyo hatua za kuuvunja mkataba zitafuata.

Source: Meneja wa Juma Kaseja; Abdulfatah Salim.


BIN ZUBEIRY BLOG
 
Kocha ndio mtaalamu. Utalazimisha upangwe? Kama hela sawa dai ni haki yako
 
Aende zake kule,kipaji ndo kinadaka si jina,washamba sana hawa ndo maana bora kushabikia ligi daraja la 3 uingereza kuliko ligi kuu bongo
 
huyo kipa hana meneja wala wakala,hivyo hawezi kumsemea mtu aliye ktk mkataba.
 
Kudaka labda mazoezini....!Kuhusu pesa hlo ndio la msingi.
 
Tafadhali MANJI na jopo lako,huyu kaseja mwacheni tu aende... yaani kitendo cha kumsajili ilikuwa ni sawa na kumkaribisha gaidi nyumbani kwako.
 
Hata hilo si la msingi, kama kweli hajalipwa si afanye kama Okwi tu?
Yaaah, aondoke tu mbona mwenzeke okwi tulimstukia wakati amevalishwa jezi nyekundu na hans poppe!!!!
Kipa wa yanga tunaemfahamu ni DIDA hao wengine ni vimeo tu....
 
anafkiri jina linadaka aende zake kwanza tulimsaidia ajira..hata ruvu stars hawakumtaka
 
Atadakaje wakati mbovu au anataka sare za simba zihamie Yanga.
 
Atadakaje wakati mbovu au anataka sare za simba zihamie Yanga.

hivi simba tunamtaka huyu wa nn? kamejaa majungu.after all hatutaki wazee hivyo Kiemba na Kisiga wabaki huko huko LABDA CHANONGO kwa kuwa ni zao letu .Huoni walau tulicheza mpira wa kueleweka!
 
Inasemekana Phiri anamtaka kwa udi na uvumba kama si na manemane! Safari ya Mapunda kurejea Kenya imewadia. Yanga msimlipe hiyo 20m/- aliyochukua inamtosha tena ikibidi airudishe maana hajaifanyia kazi.
 
Back
Top Bottom