Karo juu shule ya Trust St. Patrick Arusha


Acheni Ujinga hizo JPM aboreshe shule za UMMA ndio muarobaini wa shule binafsi na si kuziingilia kidikteta. shule za binafsi hazitaweza kutoza ADA bei kubwa kama serikali itaboresha shule zake. Kudhibiti ADA kwenye shule binafsi kutaathiri watanzania wengi wanao fanya kazi huko kama walimu, walinzi, wafagizi, wapishi, madereva na wengineo. Wafanyakazi wengi watapunguzwa kazini na kupunguziwa mishahara. Serikali iboreshe na kusimamia shule zake na si kukimbia majukumu yake na kwenye kumdhibiti mshindani wake.
 
Siyo St Patrick tu wanachaji karo ya juu, ziko shule nyingi za namna hiyo ndo maana nimeomba serikali itoe bei elekezi. watu wengine sijui vipi, wabinafsi kwelikweli eti kwasababu yeye ana uwezo basi hafikirii watanzania wengine ambao hawana uwezo. watu hao ni sawa na wale wanaoishi na maskini na barabara za kufika maskani mwao ni mbovu, sasa badala ya kujitolea atengeneze barabara anaamua kwenda kununua gari ya juu ya miguu minne, huyo ni ubinafsi
 
Wewe ni mbulula kweli kwani lazima mtoto wako asome hapo? Siuwapishe wenye hela zao? Kwa hiyo unataka mtoto wako ale chips kuku, uji wa nido, aoge maji ya moto, atibiwe, apelekwe study tour kajado kenya kwa laki moja? Pumbavu zako. Ujue hao wenye shule zao wameboresha huduma zao kuanzia walimu mpaka chakula sasa kama mnataka ada yao ishuke mnatakiwa mlalamikie serikali yenu iboreshe huduma zote ili hao wakose bei. Mjue kabisa hao wenye shule zao wanapambana na ushindani wa shule zingine
 

Muhamishe mwanao kwenye shule zisizolipa ada kubwa.
 

Wewe unafurahisha kama siyo kusikitisha .... Umwmtoapi mtoto wako shule za Serikali ANZA kata ukampeleka huko kwa hiari yako... Sasa unalalamika nini..?!! Si umwondoe mwanao mpeleke shule unayomudu kulipia. Hujalazimishwa kuacha mtoto wako hapo... Unang'ang'ania kunywa soda Kempiski kwa bei ya mgahawani...!!!!
 

hapo penya "unang'ang'ania kunywa soda kempiski kwa bei ya mgahawani/uswazi ndo penyewe.
 
hahaa muziki huwezi kuucheza toka tuachie wenzio tuucheze....kuna arusha sec pia usiaahau na shule ya msingi meru..kwa nn usimpeleke huko?
 
sijaelewa, umelazimishwa kupeleka mtoto wako pale? kuna shule za kata unalipa alfu 20 tu, mpeleke huko.
 

Kwani ni lazima upeleke mtoto wako hapo? Mbona magufuli ameamua kulipia hadi uji ni wewe tu na mwanao Nenda kwa magu bana kha!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…