Karatu itunukiwe tuzo maalum ya ujasiri, uthubutu na demokrasia iliyotukuka

Noncommited

JF-Expert Member
Jun 22, 2012
1,125
369
KARATU ITUNUKIWE TUZO MAALUMU YA UJASIRI, UTHUBUTU NA DEMOKRASIA ILIYOTUKUKA TOKA KWA CHADEMA

Chadema Waitangaze Karatu Kama Jimbo La Kiini Cha Mabadiliko Ya Kweli Na Kupewa Zawadi Maalumu

Kumbukumbu zinaonyesha Karatu ni moja ya Majimbo Vinara kwa Demokrasia nchini Tanzania hasa hasa Tanganyika. Toka 1995 Karatu haijawai kuongozwa na chama cha Mapinduzi.

Historia inaonyesha kwa mara ya kwanza ndani ya Mfumo wa Vyama vingi Jimbo la Karatu likaenda Upinzani TENA CHINI YA Chama kidogo sana kwa wakati huo kiitwacho CHADEMA, Kumbuka vyama vikubwa kwa wakati huoo vilikuwa NCCR, UDP NA CUF.

Karatu ikaongowa na Mbunge wa upinzani Dr.Slaa kwa vipindi Vitatu mfululizo 1995-2010 huku CHADEMA ikiiongoza Halmashauri ya Karatu toka mwaka 2000-2015 bila kupoteza hata muhula mmoja. Kwa CHADEMA kushika halmashauri kuliambatana na Ubunifu wa kuwajali wananchi kwa kuwaondolea Kero za Kodi na michango isiyo na Tija kama vile kodi za baiskeli na michango ya mwenge, vitu vote hivyo kufutwa kwake kulianzia Karatu.

Karatu ikakumbwa na Misukosuko miwili mikubwa iliyosomba wabunge wengi wa Upinzani na uuaji wa vyama vya upinzani: Msukosuko wa kwanza ilikuwa kuhimili Mfagio wa Rais mstaafu JK MWAKA 2005 ambapo alifagia wapinzani wengi sana kwa Nyota yake, Msukusuko wa pili mkubwa ni kitendo cha Dr.Slaa kukikacha CHADEMA na kuipaka matope kibao, wengi wa wachambuzi wakajua CHADEMA watalikosa Jimbo hilo mwaka 2015 kwa kuzingatia Dr.Slaa ndiye aliyeijenga CHADEMA kule Karatu na kuweka Ngome yake lakini matokeo yakawa sivyo, tumeshuhudi Lowasa akiiongoza KURA za urais na CHADEMA kushinda Ubunge mpaka Halmashauri. Hakika msemo wa Fuateni Maneno yangu na siyo matendo yangu muda mwingine una mantiki sana-kwa maana kwamba wana Karatu walifuata maneno na Dr.Slaa aliposema CCM ni mbaya lakini hawajafuta matendo ya Dr.Slaa kuikacha CHADEMA na kuinanga.

Lengo Kuu la Hii Thread ni kuwaomba Viongozi wa CHADEMA walilimulike Jimbo hili na kulipa heshima ya Kutosha kwa kuboresha Huduma za Kijamii kupitia pesa za Ruzuku na kufanya HARAMBEE MOJA KUBWA ya kuchangia jimbo la KARATU ili watu wa uko waweze kufaidi matunda yao ya kuichagua CHADEMA kwa kipindi chote hicho maana siamini kwamba CHADEMA walikuwa na wagombea bora sana kushinda CCM kwa vipindi vyote hivyo bali IMANI NA MAPENZI YA DHATI YA WANA KARATU KWA CHADEMA.

Kitendo cha kuwaandalia TUZO MAALUMU na shukrani kwa wana KARATU kitaleta tija sana kwa Majimbo mengine kujifunza na kuwa na ARI ya kuwa kama KARATU kupitia uwakilishi wa CHADEMA.

MUNGU IBARIKI CHADEMA, MUNGU IBARIKI UKAWA, MUNGU IBARIKI KARATU, MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA.
 
Mpaka sasahivi sijui UKAWA wanafanya nini Kinondoni na Ilala...yes wameshinda..So what?

Mkuu mameya wa UKAWA wa Ilala na Kinondoni wanachofanya ni kuzurura na majoho ya umeya kwenye vijiwe vya UKAWA kujitambulisha kuwa wao ndio mameya kwa Tiketi ya UKAWA.Wanazurura badala ya kuzoa uchafu na kuzibua mivyoo ya maji machafu yaliyozagaa kila kona dar NA KUTENGENEZA BARABARA ZILIZOJAA MAHANDAKI.Ona hata machinjio yalivyo machafu wenyewe wamekula jiwe.
Wanapenda vyeo kuliko kazi.Hawaelewi kuwa cheo ni kazi sio CHEO.

Umeya kwao ni kuvaa majoho na kuzurura vijiwe vya UKAWA.
 
Mkuu mameya wa UKAWA wa Ilala na Kinondoni wanachofanya ni kuzurura na majoho ya umeya kwenye vijiwe vya UKAWA kujitambulisha kuwa wao ndio mameya kwa Tiketi ya UKAWA.Wanazurura badala ya kuzoa uchafu na kuzibua mivyoo ya maji machafu yaliyozagaa kila kona dar NA KUTENGENEZA BARABARA ZILIZOJAA MAHANDAKI.Ona hata machinjio yalivyo machafu wenyewe wamekula jiwe.
Wanapenda vyeo kuliko kazi.Hawaelewi kuwa cheo ni kazi sio CHEO.

Umeya kwao ni kuvaa majoho na kuzurura vijiwe vya UKAWA.
Acha nao wafaidi mbona hao wengine wamekaa miaka hamsini na matakataka mitaani kibao?
 
Mkuu mameya wa UKAWA wa Ilala na Kinondoni wanachofanya ni kuzurura na majoho ya umeya kwenye vijiwe vya UKAWA kujitambulisha kuwa wao ndio mameya kwa Tiketi ya UKAWA.Wanazurura badala ya kuzoa uchafu na kuzibua mivyoo ya maji machafu yaliyozagaa kila kona dar NA KUTENGENEZA BARABARA ZILIZOJAA MAHANDAKI.Ona hata machinjio yalivyo machafu wenyewe wamekula jiwe.
Wanapenda vyeo kuliko kazi.Hawaelewi kuwa cheo ni kazi sio CHEO.

Umeya kwao ni kuvaa majoho na kuzurura vijiwe vya UKAWA.
umeya sio kazi ya kuzibua mitaro
 
Karatu niliwaheshimu sana kuwa watu wasioyumbishwa, wakweli na wasio waoga. Heshima hii kwa kiasi kikubwa ilitokana na misimamo thabiti ya Dr. Slaa. Ni umakini wa Dr. ndiyo uliowapa heshima wana Karatu na wilaya yao. Ni ukweli usiopingika kuwa Karatu wana deni kubwa kwa Dr. Slaa.

Heshima yangu kwa Karatu ilifutika ghafla pale nilipobaini wamempa kura nyingi za urais el kuzidi wagombea wengine. Nikatambua sifa ambazo niliona wanazo, hawana. Nikajiuliza, iwapo el angegombea urais kupitia ccm, wangemchagua? Kumbe wanachagua chama bila kuangalia sifa ya mgombea? Kumbe gia iliyobadilishwa angani na DJ Mbowe iliwasomba Karatu pia? Kumbe Slaa anao mashujaa wachache waliokuwa wakimwelewa? Ghafla nilipata picha ya nyumbu wa Serengeti.....

Ok, peaneni tuzo na cdm yenu, ila binafsi kisiasa nimewadharau sana. Sivyo nilivyowafikiria. Hamna msimamo, si wakweli na mwaweza yumbishwa.
 
SIJAULIZA KUHusu Magufuli...UKAWA wanatakiwa wtende zaidi ya CCM sio kujilinganisha na CCM

Ikiwa serikali kuu bado haijaanza kufanya kazi, hata chini hawawezi acha nao watumbue majipu ya mabango rais akimaliza kutumbua na meya atamaliza kutumbua presha za MA DC zitashuka hapo kazi itafanyika.
 
huelewi unachokisema...serikali kuu ya ccm isipomaliza na nyie mnasubiri au sio? basi bora msingechaguliwa tu

Baraza la madiwani halihitaji chochote kutoka kwa DC

Ikiwa serikali kuu bado haijaanza kufanya kazi, hata chini hawawezi acha nao watumbue majipu ya mabango rais akimaliza kutumbua na meya atamaliza kutumbua presha za MA DC zitashuka hapo kazi itafanyika.
 
SIJAULIZA KUHusu Magufuli...UKAWA wanatakiwa wtende zaidi ya CCM sio kujilinganisha na CCM
Una hoja ila tuwape muda kidogo wakusanye kodi.Bila bajeti huwezi ona kazi ya meya.
Mameya sio executives.
Ila tunawatarajia wafanye zaidi ya wale wa CCM.
 
Tuambie mmefaidi nini kikubwa kwa kuichagua chadema ili wengine nao waichague sio kutaka tuzo. Sasa tuzo yanini Kama watu bado maskini? Ingefaa
ninyi ndio muishkuru chadema Kama imefanya vizuri katika kuwaongoza na sio chama kiwashkuru ninyi!!
 
Karatu niliwaheshimu sana kuwa watu wasioyumbishwa, wakweli na wasio waoga. Heshima hii kwa kiasi kikubwa ilitokana na misimamo thabiti ya Dr. Slaa. Ni umakini wa Dr. ndiyo uliowapa heshima wana Karatu na wilaya yao. Ni ukweli usiopingika kuwa Karatu wana deni kubwa kwa Dr. Slaa.

Heshima yangu kwa Karatu ilifutika ghafla pale nilipobaini wamempa kura nyingi za urais el kuzidi wagombea wengine. Nikatambua sifa ambazo niliona wanazo, hawana. Nikajiuliza, iwapo el angegombea urais kupitia ccm, wangemchagua? Kumbe wanachagua chama bila kuangalia sifa ya mgombea? Kumbe gia iliyobadilishwa angani na DJ Mbowe iliwasomba Karatu pia? Kumbe Slaa anao mashujaa wachache waliokuwa wakimwelewa? Ghafla nilipata picha ya nyumbu wa Serengeti.....

Ok, peaneni tuzo na cdm yenu, ila binafsi kisiasa nimewadharau sana. Sivyo nilivyowafikiria. Hamna msimamo, si wakweli na mwaweza yumbishwa.
Karatu niliwaheshimu sana kuwa watu wasioyumbishwa, wakweli na wasio waoga. Heshima hii kwa kiasi kikubwa ilitokana na misimamo thabiti ya Dr. Slaa. Ni umakini wa Dr. ndiyo uliowapa heshima wana Karatu na wilaya yao. Ni ukweli usiopingika kuwa Karatu wana deni kubwa kwa Dr. Slaa.

Heshima yangu kwa Karatu ilifutika ghafla pale nilipobaini wamempa kura nyingi za urais el kuzidi wagombea wengine. Nikatambua sifa ambazo niliona wanazo, hawana. Nikajiuliza, iwapo el angegombea urais kupitia ccm, wangemchagua? Kumbe wanachagua chama bila kuangalia sifa ya mgombea? Kumbe gia iliyobadilishwa angani na DJ Mbowe iliwasomba Karatu pia? Kumbe Slaa anao mashujaa wachache waliokuwa wakimwelewa? Ghafla nilipata picha ya nyumbu wa Serengeti.....

Ok, peaneni tuzo na cdm yenu, ila binafsi kisiasa nimewadharau sana. Sivyo nilivyowafikiria. Hamna msimamo, si wakweli na mwaweza yumbishwa.

Mimi ni mpiga kura toka jimbo la Karatu since 2000, tunachagua mfumo sio mtu.. tungetegemea sana mtu basi tuwe tunafanya booking kwa Mungu atushushie tunayemtaka.. Steve Jobs alifariki mwaka 2011 lakini Kampuni ya Apple imebaki kuwa imara.. hatununui ipads, iphones kwa sababu zimetengenezwa na Steve Jobs tunanunua kwasababu ni bidhaa imara zinazotengenezwa na Apple Electronic Company!
 
Heshima yangu kwa Karatu ilifutika ghafla pale nilipobaini wamempa kura nyingi za urais el kuzidi wagombea wengine. Nikatambua sifa ambazo niliona wanazo, hawana. Nikajiuliza, iwapo el angegombea urais kupitia ccm, wangemchagua? Kumbe wanachagua chama bila kuangalia sifa ya mgombea? Kumbe gia iliyobadilishwa angani na DJ Mbowe iliwasomba Karatu pia? Kumbe Slaa anao mashujaa wachache waliokuwa wakimwelewa? Ghafla nilipata picha ya nyumbu wa Serengeti.....

Ok, peaneni tuzo na cdm yenu, ila binafsi kisiasa nimewadharau sana. Sivyo nilivyowafikiria. Hamna msimamo, si wakweli na mwaweza yumbishwa.
Si kweli Mkuu wana KARATU wamesimamia kwenye Ukweli kwamba ccm ndio chanzo cha matatizo yote hayo na si chama kingine
 
Lengo Kuu la Hii Thread ni kuwaomba Viongozi wa CHADEMA walilimulike Jimbo hili na kulipa heshima ya Kutosha kwa kuboresha Huduma za Kijamii kupitia pesa za Ruzuku na kufanya HARAMBEE MOJA KUBWA ya kuchangia jimbo la KARATU ili watu wa uko waweze kufaidi matunda yao ya kuichagua CHADEMA kwa kipindi chote hicho maana siamini kwamba CHADEMA walikuwa na wagombea bora sana kushinda CCM kwa vipindi vyote hivyo bali IMANI NA MAPENZI YA DHATI YA WANA KARATU KWA CHADEMA

Tz wapinzani wa kweli wanaopigania mabadiliko makubwa ya mifumo ya utawala au ya uendeshaji wa nchi na serikali ni wachache sana, walio wengi (majority) ni wafuasi wa watu, maanake mtu wake akishaondoka kwenye mrengo fulani naye huunga reli. Watu wa Karatu hawana tofauti sana na watu wa Mbulu, mantiki yake ni kuwa siyo kweli kuwa wana mapenzi na CDM. Kwa miaka yote 25 ya upinzani CDM wameongoza Karatu lakini Mbulu ni kwa miaka 5 tu. Why? Sababu kubwa ni wagombea. 1995 Dr Slaa alishinda kwa CCM wakampora, akahamia CDM, mantiki yake toka mwanzoni hakuwa mwanamageuzi wa kweli. Akaeendelea kushinda kwa ushawishi wake siyo wa chama, 2010 akamleta Natse naye akashinda kwa ushawishi wa Dr Slaa. 2015 Qambalo ameshinda kwa ushawishi wake na siyo chama na angeshinda hata angekuwa CCM, sababu kubwa ni kazi yake ya mratibu wa maendeleo ya jimbo katoliki la Mbulu ampapo amesimamia miradi ya maji kwa vijiji vyote vya wilaya ya karatu. Kwa kifupi: Dr Slaa, Mchg Natse na Qambalo wote ni viongozi wa makanisa makubwa, katoliki na kilutheri, ukishaelewa ushawishi wa haya makanisa utaelewa kuwa siyo mapenzi kwa CDM.

Kwa kukuelimisha kidogo, nchi au wilaya haijengwi kwa ruzuku, harambe na au misaada, hujengwa au kuendelezwa kwa kodi ya wananchi na kwa sasa anayekusanya kodi hiyo ni ccm maana ndo wanaendesha serikali. Kwa hiyo km wewe ni mwanamageuzi kwa kweli au km unaelewa tunapigania nini ktk nchi hii basi ulipaswa kuishauri CDM ipeleke ruzuku kwenye shughuli kuelimisha umma maeneo mengi ya Tz ili 2020 tuchukue dola kisha itekeleze ilani yake.
 
Demokrasia siyo lazima kuchagua upinzani, wananchi wachague kiongozi mwenye mawazo chanya kwa maendeleo ya eneo lao bila kuangalia chama!
Hata hivyo, ni muhimu kuwa makini hasa pale chama tawala kinapokuwa kimeshindwa kutetea maslahi ya walio wengi!
 
Back
Top Bottom