Kampeni ya kutunza uume

Mtumsafi

Member
Jun 1, 2012
90
64
Nimeikopi mahala.tafadhali ewe mwanaume.jifunze kitu.



TUNZA UUME UHESHIMIKE

Uume imara ni heshima kwa mwanume na furaha ya mwanamke, bila uume huwi mwanaume. Uume ndio kiungo muhimu katika mwili wa mwanaume. Ndio mana mtoto akizaliwa mama na manesi kwa haraka huchungulia kuona ni wa kike au wa kiume? Uume hutambulisha nasaba za ndani zilizopo ndani ya mwili wa mwanaume.
Lakini tangu zama za Adamu hasa baada ya gharika kuu wakati wa Sodama na Gomora mwanaume amekuwa anatumia uume wake vibaya hadi kupelekea uume kuwa goigoi na legelege na hatimaye kushindwa kutimiza majukumu yake ya awali. Tangu awali uume uliundwa na Mungu ili uyatimize kikamilifu mambo yafuatayo.
(1) kutumika katika kuzalisha (reproduction)
(2) kustarehesha
(3) kusafisha mwili na uchafu (chumvi na sumu mbalimbali) na pia
(4) kutumika kama utambulisho (identity)

Uume bora ni ule wenye uwezo wa kufanya shughuli zote yani kuzalisha, kuondoa sumu mwilini na kustarehesha bila usumbufu wala maumivu. Uume bora huwa imara ukiwa katika majukumu yake na kuweza kutimiza malengo yaliyokusudiwa. Chakula bora, afya bora, saikolojia sahihi na mzunguko mzuri wa damu katika uume ni muhimu sana kwa afya ya uume bora.

Katika mada iliyopita nilikuelezea kwa uchache maadui wa uke katika ile mada ya “tunza uke ukutunze” leo ningependa pia tujikumbushe maadui 18 wa uume katika mada mpya ya “tunza uume uheshimike”
Sasa kila unapoona jambo la tofauti linajitokeza kuhusu uume wako kwa mwonekano, utendaji kazi na utuliaji (pozi) basi tambua ya kwamba kuna jambo linalofanyika ndani ya mwili wako au ndani ya uume wako ambalo wewe huwezi kulijua mpaka umwone daktari. Ni muhimu kujenga tabia ya kuonana na madaktari mara kwa mara ili kujua afya ya uume wako
Kwa ujumla ubora wa uume unaathiriwa na vitu vingi sana lakini viko katika makundi yafuatayo

(1) UOGA na WASIWASI, UVIVU wa kujifunza na uvivu wa kufanya MAZOEZI.
(2) Ulaji mbaya wa CHAKULA, unywaji wa vileo badala ya maji na utumiaji wa madawa makali.
(3) TABIA MBYA kama vile kutokuoga angalau mara 2 kwa siku, kutojisafisha mara ukojoapo na kwenda haja kubwa, kuwa mchepukaji, punyeto, uangaliaji wa picha chafu za ngomo, ufanyaji wa ngono kinyume na maumbile, uvutaji wa sigara, ulaji wa mirungi, uvutaji wa bangi, utumiaji wa madawa ya kulevya na uchafu wa roho na moya kama kuwaza ngono tu siku nzima unajichosha.
(4) KUTOKUMJALI MKE/MPENZI wako na pia kutokuujali uke wake
(5) MAGONJWA HASA SUGU ambayo mara nyingi yanatokana na vipengere 1-4 hapo juu
(6) Kukaa na uume usiyo na TOHARA. Hii sitaielezea kwa leo.

Dalili za uume wako kushambuliwa na MAADUI ni kama zifuatazo.
1. Kupata maupele, michubuko, miwasho na vidonda sehemu za siri
2. Uume kushindwa kusimama au kuwa imara
3. kushindwa kufanya tendo la ndoa kwa ufasaha
4. kuwa na magonjwa mbalimbali kama tezi dume na bawasiri, kukojoa mkojo kwa shida na maumivu, kuwa na STDs nakadhalika.
5. kupata mshindo mwepesi au kufika kileleni kwa haraka au kwa shida
6. Kupungua kwa mbegu za kiume na kuwa mgumba
7. Mwanaume kukose kuutumia uume kama kitambulisho, I mean mwanaume anaishi na mwanaume mwenzie (sasa haijulikani mwanaume na mwanamke ni yupi)
Sasa ni vizuri ukajua pia kuwa unapokuwa na dalili hizi lazima uangalie nini hasa chanzo chake ndio upate tiba kamilifu itakayokuweka huru.

Maadui hawa mimi huwafananisha na KAA (crab) kwa sababu ni maadui wanaosambaa mwilini haraka sana bila hata ya wewe kupenda. Kumbuka hawa wanaitwa maadui kwa sababu tu wanasababisha uume usifanye kazi zile zilizokusudiwa tangu awali. Kumbuka pia ya kwamba maadui hawa wengine ni dalili tu ya jambo flani linaloendelea mwilini ambalo sio rahisi kulijua mpaka uingie kiundani au uende kupima hospitalini.

ADUI WA #01. MAGONJWA

Magonjwa ni adui namba 1 wa uume wako. Magonjwa ya sehemu za siri, magonjwa ya mwili kwa ujumla, na magonjwa ya wanaume kama -tezi dume ni adui wa uume wako. Ugonjwa kama kisukari na presha, figo na ini kutokufanya kazi vizuri LAZIMA uume uwe dhaifu. Kuna magonjwa mengine pia kama viupele vya ajabu ajabu huko magogoni pamoja na ugonjwa wa bawasiri. MAGONJWA HAYA LAZIMA YATIBIWE HARAKA. Kumbuka chakula ndio dawa pekee ambayo Mwenyezi Mungu alitupatia wanadamu. Magonjwa ya zinaa hata kukojoa mkojainakuwa ngumu, mtu mwenye tezi dume kwa mfano anakojoa mkojo unaunguza kama anakojoa maji ya moto, bawasiri inaumiza mgongo ile mbaya. Je uume utakuwa imara hapo?
ACTION: KULA CHAKULA BORA NA EPUKA UZITO NA KITAMBI

ADUI WA #02. ULEVI NA SIGARA - Ulevi ndio, Na ulevi haufai kabisa kwa afya ya uume wako. Ulevi unakufanya uwe mlaji wa nyama hasa nyekundu, unakuwa sio mwepesi wa kunywa maziwa na kula matunda, unakuwa mzembe wa majukumu yako ya ndani, unapata vitambi, unaharibu balansi ya homoni >> unaelekea upotevuni” Kunywa maji ya kutosha, maji fresh ili kuuburudisha mwili na kuondoa msongo wa mawazo.
DRINK WATER NOT ALCOHOL & SODA

ADUI WA #03. PUNYETU NA MICHEPUKO

Watu walionishuhudia ambao walifungwa katika minyororo ya kufanya punyetu hadi mara 6 kwa siku, waliokuwa wanafanya hadi vyoo za ofisi na wengine kujificha hata majumbani wake zao wakiwa wamelala au hawapo. Vijana wa boarding school na vyuo, mabachela na wengineo wanatoa shuhuda zinazotisha. Punyeto imekuwa utumwa. Wanashuhudia kupata majipu, michubuko, msongo wa mawazo, kushuka kwa kujiamini, wengine wameshuhudia kufika kiwango cha juu cha kutokuvutiwa na wanawake kabisa. Kwa kifupi punyeto huharibu vipokezi (receivers) vya hisia mwilini na saikolojia yako ya mapenzi kwa ujumla, kuharibu mishipa na nerve za ufahamu katika uume na kukukosesha mawasiliano sahihi kati ya uume na akili yako. Unaporudi kufanya tendo la ndoa kawaida (na mwanamke) unakuwa tayari umeathirika na inakuwa kama upo ulimwengu wa nje ya mapenzi. Wengine wanasema haina madhara na pia kutoa namna nzuri ya kufanya ili usipate madhara, lakini kila waathirika wanasema haifai….KINGA NI BORA KULIKO TIBA
ACTION: ANZA PROGRAM YA KUACHA PUNYETU HARAKA ONA KAMA HUO NI UGONJWA KAMA MAGONJWA MENGINE.

ADUI WA #04. MADAWA

Hapa kuna madawa ya kulevya na madawa ya kawaida, pia madawa makali ya presha na kisukari ni hatari kwa afya ya uume wako. Madawa yanayowekwa katika baadhi ya makopo ya vyakula vilivyosindikwa na mengine yanayonyunyiziwa mashambanin wakati mimea inakuwa katika ukuaji wake ni hatari tupu. Madawa ya kulevya nadhani wote tunayajua yalivyonoma. Unalegea mwili mzima, uume unajifia tu kama bamia.
ACTION: JENGA TABIA YA KUTUMIA CHAKULA CHA ASILI KAMA DAWA ILI MAGONJWA YA TABIA YASIKUPATE

ADUI WA #05. UCHAFU WA MWILI, NGUO NA NGUO ZA MBANO

Nguo chafu, za mbano na zisizo za pamba zinasababisha magonjwa ya ngozi. Pia uume unatakiwa upate free range yaani ubembee na sio kutulia kama jiwe. Hii inaufanya uume kuwa active na kuwa tayari kwa kushughulika. Pia wanaume wengi ni mabingwa wa kuvaa suruali si chini ya siku 3 hadi 7. Wengine wanavaa jinsi kauka nikuvae - huo ni uchafu na ni hatari uchafu kuingia ikulu. Oga mara kwa mara fua nguo zako hata kama wife hafanyi fanya mwenyewe, vaa boxer chupi sio zile za chupi za V kama za wanawake. Ukikojoa na kwenda haja kubwa jitawaze vizuri. Kuwa msafi mwili na roho, Sasa wengine wanafuga rasta maeneo ya Ikulu. … OK decide yourself kama ni usafi huo au uchafu, unavaa jinsi week nzima!!!!
ACTION: ACHANA NA SKINI JEANS, CHUPI ZINAZOBANA NA TAITI UNAZOVAA SIKU NZIMA, KUWA MSAFI MUDA WOTE SIO SIKU YA KWENDA UKWENI NDIO UNAOGA NA KUVAA SUTI

ADUI WA #06. BAADHI YA CHAKULA

Hapa lazima tuambiane ukweli ivi mwanaume unakula chips na soda 24/7 unataka uwe nini kama sio kituko, vyakula vyepesi vyepesi visivyokuwa na nguvu vinavyokuongezea sukari na presha mwilini achana navyo. Mwambie waifu kabisa aachane na mapishi ya ugali uliokobolewa. Vyakula vya kukujaza gesi tumboni havifai, vyakula vinavonenepesha tumbo achana navyo kabisa. Wengine wanapiga pombe kali eti zinaongeza nguvu, at least kwa leo au kesho “energy drinks is not a long lasting solution”. Mara moja moja penda kutumia asali na mdalasini, tende, matunda kwa wingi hasa yale yenye zink kama tikiti maji, avocado, uyoga na pia machungwa. Hakikisha unakula matunda dakika kadhaa kabla au baada ya chakula. Usichanganye matunda yenye acid na alkali mara moja na ukala yaani mtindo wa cocktail, mfano chungwa lina acid, parachichi ni alkaline (haya usiyale yote mara moja).
ACTION: BADO NASISITIZA KULA CHAKULA BORA NA PIA KULA MATUNDA SAHIHI KIUSAHIHI.

ADUI WA #07. HOMONI KUVURUGWA

Hapa ndugu zangu pana uhusiano sana na namba 4 hapo juu. Vyakula na madawa tunayotumia pamoja na madawa yaliyotumika na wakulima ndio yanaleteleza hormoni katika mwili wako kuwa na balansi ya tofauti. Matokeo yake hormoni zinazohitajika kuamsha vichocheo vya kuufanya uume ufanye kazi vema zinashindwa kuwa katika balansi nzuri na hatimaye kuufanya uume kushindwa kufanya kazi zake kwa ufasaha.
ACTION: KULA CHAKULA BORA NA EPUKA UZITO NA KITAMBI

ADUI WA #08. UMRI

Kadri umri wako unavozidi kwenda mbele ndivyo uwezo wa kiafya wa uume wako unavyozidi kupungua ingawa wanasema "old wine gets better" Magonjwa pia ni rahisi kukuingia, magonjwa kama tezi dume, kansa ya uume, ubovu wa kibofu cha mkojo na pia kukosekana kwa damu katika sehemu zako za siri.
ACTION: BADO NASISITIZA KULA CHAKULA BORA, KAMA UNAWASIWSI PATA VIRUTUBISHO VYA KUONDOA SUMU KUIMARISHA MIFUPA NA AKILI

ADUI WA #09. KUONGEZA UREFU NA UJAZO WA UUME NA PIA KUUCHORA UUME KWA KUTOBOA AU KUPAKA RANGI

Wanaume wengine hujichora katika uume wao na kuweka alama mbalimbali au majina mbalimbali. Kwa kuwa kazi hizi katika mazingira ya kiafrica hufanywa kwa siri basi vitogeo huwa dhaifu na huenda vikaambukiza magonjwa, lakini pia ukisha chora uume wako kwa kutoboa ngozi ni rahisi kwa magonjwa kukuingia wakati ukiwa katika harakati zako za kinyumba. Kuongeza saizi na ujazo wa uume pia ni adui wako wa baadae (future enemy) ingawa huwezi jua mara moja. Baada ya muda kupita utabaini mapungufu makubwa ya uume wako kutokana na kuongeza urefu au ujazo wake. Watu wengi wapo na wanalalamika, uume umelala pamoja na kuwa mnene na mrefu. Njia za asili ni zile zinaongeza mzunguko wa damu uumeni na kuzuia magonjwa sugu kama kisukari, presha, matatizo ya ini na figo pia kufanya mazoezi ya viungo vya mwili na misuli.
ACTION: ACHA KABISA HIZO TABIA, UACHE UWE KAMA MUNGU ALIVYOUUMBA. JIZOEZE NA JIFUNZE MBINU MABALIMBALI ZA KUWA NA UUME UNAOFANYA KAZI ZAKE VIZURI BILA KUUJAZA AU KUUREFUSHA

ADUI WA #10. ACROBATIC AND ATHLETIC SEX

Hawa pia ni maadui wakubwa, kuna baadhi ya wanandoa hufanya mapenzi kwa kutumia staili za tofauti tofauti na zingine huufanya uume kupenya kwa shida au kukunjana na hivyo kusababisha michubuko na uvimbe katika kichwa na shingo ya uume. Na pia wengine hufanya mapenzi muda mrefu sana kama vile wako mashindanoni - Jiulize unabakia salama? Starehe isiwe kero. Pima faida ya starehe na hasara yake.
ACTION: ENJOY SEX OTHERWISE YOU GET SEXUAL INJURY

ADUI WA #11. MSONGO WA MAWAZO

Au stress huyu ni adui endapo utashindwa kumdhibiti kwa kuwa stress husababisha milango ya fahamu kuziba na pia kuunyima uume damu na oxygen ya kutosha na hivyo uume kushindwa kufanya kazi yake vizuri. Ikiwa utashindwa kuusimamisha uume huenda ukashindwa mara nyingine tena kwa kuwa swala hilo linaweza kuathiri saikolojia yako ya mapenzi na hivyo kujikuta kila wakati unashindwa wakati ki-ukweli upo fiti. Jifunze kuwa nje ya stress kama vile kupangilia mambo yako vizuri ya kijamii, kiofis na kipesa (kwa sababu stress au msongo hutokea wakati matokeo halisi yamekuwa madogo kuliko matokeo tarajiwa na inaonekana hamna namna ya kufanya na muda umekwisha) – Siku zote panga siku yako vizuri na yaangalie mambo yote kwa kutumia akili chanya. Katika kila ubaya kuna uzuri, fuata uzuri.
ACTION: KULA CHAKULA BORA NA SAHIHI, JIPANGE, JIACHIE NA PIGA MAZOEZI YA KUTOSHA.

ADUI WA #12. NGONO KINYUME CHA MAUMBILE, VIDOLE NA MIDOLI

Ufanyaji ngono kinyume na maumbile ni hatari kwa afya ya uume wako, iwe unafanya au unafanywa yote yanapelekea kuwa na hali ya sintofahamu mara uume unapokutana na uke. Sio mazoea yake na sio utaratibu wa dini zetu hata wapagani wanakataa wala sio uhalisia. Wengine wana vimidoli vyao na vitu vinavyofanana na hivyo. Unasinyaisha uume wako…. STOOOOP & BE A MAN.
ACTION: KWA WENYE WATOTO: ANGALIA MTOTO ANAPOKUWA NA TABIA ZA AJABU AJABU MKAGUE, NA ONGEA NAYE MARA KWA MARA. SIO KILA SIKU UNARUDI UNAKUTA WAMELALA – yasijewatokea ya Moshi (Mbaya sana).

ADUI WA #13. WASIWASI WOGA NA UVIVU WAKATI NA KABLA YA TENDO LA NDOA.

Hapa ndugu zangu hakuna maelezo mengi sana ila kumbuka tu ya kwamba kuwa na wasiwasi na woga kunaondoa uwezo wa damu kufika maeneo ya uumeni hivyo kuukosesha uume malighafi muhimu ya damu na oxygeni ili uume ufanye kazi vizuri. Pia wewe mwenyewe mwanaume unakosa focus (target) ya jambo unalolifanya. Kuwa mwanume jiamini unaweza; YOU CAN DO IT EVEN BETTER

ADUI WA #14. UPUNGUFU WA TESTESTORENE

Testosterone ndio homoni ya kiume inayohusika na uundaji wa viungo vya kiume wakati mtoto akiwa tumboni hajazaliwa na kisha kuanza kujenga mwili wa kiume wakati kabla ya kubalehesha na kumtayarisha kijana wa kiume kuwa baba akisha balehe. Na baada ya hapo homoni hii huhusika na matendo mabalimbali ya kimapenzi na mvutano kati ya mwanamke na mwanaume. Pia huhusika na uzalishaji na ukomazaji wa mbegu za kiume. Homoni hii ikipungua uwezo wa uume kufanya kazi vizuri hupungua. Uzuri ni kwamba unaweza kuongezwa homini hii katika mahospitali lakini pia kuna vyakula unavyoweza kula na kuiongeza taratibu.
Action:IJUE TESTOSTERONE.

ADUI WA #15. PICHA CHAFU, ROHO CHAFU NA AKILI CHAFU

Uangaliaji wa picha chafu za ngono ni hatari kwa ujumla wa saikolojia yako. Mwili wako unauwezo wa kubadili tabia na vionjo kama utafanya hivyo ndani ya siku 15 hadi 21. Ikiwa utazoea kuangalia picha za ngono ambazo wataalamu wengi wa holywood wanasema si za kweli basi unajikuta upo katika ulimwengu ambao sio halisia. Ukija kuonana na mkeo halisi unajikuta mwili wako wa hisia bado upo Holywood. Akili yako imetekwa. Huwezi fanya vizuri tena, wengine wanasema wanatafuta apetite, lakini kumbuka apetite hii sio ya asili baada ya muda unazoea unakuwa sugu na huwezi tena kuwa boosted na hizo picha. Best apetizer ni mkeo.
ACHA KABISA PICHA CHAFU, UKIJIZOESHA NDANI YA SIKU 15 HADI 21 UNAACHA KABISA. MPENDE MKEO TU

ADUI WA #16. MWANAMKE MWENYE DHARAU NA MATUSI

Tabia za baadhi ya wanawake zimekuwa kero kabisa kwa uimara wa uume. Mwanamke anakuwa mchafu kupindukia. Wengine ni kutoa matusi mfululizo kama vile hawajaenda jandoni, wengine ni dharau zisizokuwa na mpango hadi wakati wa tendo la ndoa. Wanawake wengine hawachangamki hata mwanaume ajitahidi vipi yaani wapo wapo tu as if ni magogo. Hii ni hatari sana. Mwanamke ni ufunguo mzuri sana kwa afya ya mwanaume hasa kama mwanamke ameutunza vizuri uke wake na pia kama mwanaume hajaathirika na uoga, wasiwasi na mashaka, magonjwa na tabia zile mbaya kama punyeto, michepuko, ulevi na madawa ya kulevya. Wewe mwanume unatakiwa utengeneze mazingira ya mkeo kuwa msafi na mwema kwako, anayejituma na ambaye ni mkweli daima. Love your wife she will pay you back 100%.
ACTION: Mwanamke ndio kiongozi wa Ndoa, mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake mwenyewe. Kuwa kiongozi wa mumeo mara tu anapoingia chumbani, Ubos wake auache nje ya mlango wa chumbani.

ADUI WA #17: UZITO, KITAMBI NA KIRIBA TUMBO CHA MWANAMKE

Wanwake wengi siku hizi wana vitambi, owk unaweza sema hii inakujaje hapa? Ukweli ni kwamba baadhi ya shughuli za msingi za uume zinashindikana kufanyika kwa sababu ya kitambi cha mwanamke, ofcourse hata kitambi cha mwanaume ni adui lakini adui namba moja ni kitambi cha mwanamke na pili ni kitambi cha mwanaume. Wanawake wengi wanaoshindwa kufika kileleni wanavitambi au uzito mkubwa. Hii inauletea uume shida sana ya kutimiza majukumu ya kinyumba.
ACTION: Anzeni program za kutoa uzito, vitambi na viriba tumbo kwa kutumia chakula asili tu, mazoezi ukipenda pia dieting ukipenda.

ADUI WA #18: UKE USIOTUNZWA, uume unakuwa bora ikiwa uke pia ni bora.
ACTION: Mwanaume lazima ujiunge na mkeo kumweka vizuri

ADUI WA #19: KUKOSA USINGIZI

Kuangalia mpira kuanzia saa11 mpaka saa7 usiku, wengine wanaangalia movie huku wanakula mirungi nab ado asubuhi unawahi kazini. My friend unaharibu mwili wako na uume wako unapata stress. Ukilala mwili unapata muda wa kurekebisha misuli, kuweka balansi nzuri ya homoni na kurudisha hamu za mwili za kawaida pia kuboresha kinga ya mwili. LALA USINGIZI WA KUTOSHA UPUMZIKE UBONGO UJIPANGE, MISULI ITULIE SELI ZA MWILI ZIZALIANE.

ADUI WA #20: TOO MUCH SEX IS HARMFUL.

Ukifanya sana ngono unahatari ya kupata madhara yafuatayo uume kuvunjika (hauvunjiki kama kijiti ila misuli inaumia), kuishiwa maji mwilini, UTI, kuumiza nerve za uume, kupunguza nguvu ya misuli na kushindwa au kuuma misuli ya mwili. AMUA NI KIASI GANI KINAFAA

Kwa ujumla utakuwa umegundua ya kwamba chakula ndio suluhisho la kudumu la kupambana na maadui hawa, ingawa pia utalazimika kuwa mwenye tabia nzuri. Endapo wakati mwingine inakuwa ngumu kwa chakula kufanya kazi na kuleta matokea ya haraka itakulazimu kupata ushauri wa kitabibu kama kupata dawa za hospitalini (kemikali) au virutubisho. Ikiwa utapata dawa au vitutubisho hivi na ukapona huna budi kuendelea kutumia chakula bora na pia kuwa na tabia njema kwa ajili ya kupata matokeo ya kudumu, yenye furaha na amani.

Basi ndugu yangu wa kiume (hata wa kike), hii ndio mada yetu moto ya leo na nadhani itakuwa msaada kwako sana.

Ili kulipia mada hi unatikiwa U~ LIKE page ya “health point.” na kushare na magroup mbalimbali kadri utakavyoweza. Asante sana na ubakie na afya njema. Chakula ni Dawa.

healthpoint|+255-755-693-692|Arusha|Tanzania
 
Du...hiyo yote niisome wakati kesho nina test....labda kama kuna summary
 
Ni kweli ukitaka kumficha mwafrika weka ujumbe kwenye vitabu, ndo Tabia zetu sisi waafrika,kuna wengine wamesoma kichwa cha habar tu wakaanza kukoment,bora Mimi nimemaliza kabisa japo macho yanawasha,ndo hivo mtu msafi
 
Duh!tunakaa nayo tu MIPINI bila kujua ulinzi wake!yote kwa yote ila hilo la umri sidhani kama linastahili kuwa katika orodha ya maadui coz halikwepeki unabaki kusikia wazee wanasema enzi zangu mie so la umri limekaa kimajuto.
 
Back
Top Bottom