Kama ntaendelea kuishi 2015

Kama ntaendelea kuishi 2015

Jacaranda

Member
Joined
Oct 23, 2011
Posts
45
Reaction score
20
Watu hujifunza siku hadi siku kuhusu vitu viletavyo fedheha moyoni.Kwa Afrika kipindi cha uchaguzi huwa si mwanana.Kama ntaendelea kuishi zaidi ya 2015,kama moyo wangu utaendelea kudunda na mishipa yangu kutililisha damu nitambeba mtoto wangu na kumrusha juu na kisha kumdaka,nitamnong'oneza kwa sauti yenye hakika na kumwambia hii ndo Tanzania tuliyoitaka


kisha Ntamshika mama yake kiunoni huku nikimtazama machoni kwani ntakua na uhakika sitamuona akilia tena kuhusu hali ngumu ya maisha kwani adui wa maendeleo ccm atakua amezikwa,sanduku la kura litakua limetoa adhabu yake dhidi ya ccm
 
Kwa kiasi fulani, pengine kiasi kidogo CCM ni sababu tosha ya hali ngumu ya maisha, kiasi kikubwa nionavyo mimi ni sisi wananchi. We are not doing enough for ourselves, we cheat too much on almost everything, tunaiba, kuhonga na kuhongwa rushwa katika kila nyanja, kazi hatuifanyi vile ipasavyo, tunalalamikia wengine as if wao wamezaliwa kuishi kwa niaba yetu au tumezaliwa tuishi kwa niaba yao. Wananchi tunaiba na tukipata madaraka tunaiba zaidi, Iwe CCM au chama kingine chochote, vyote viko mikononi mwa watanzania wenzetu wenye hulka hizihizi. Kwa mtazamo wangu, ukombozi tunaohitaji sasa ni kifkra zaidi kuliko ukombozi wa kisiasa. Expectations kubwa sana juu ya vyama mbadala wa CCM ni janga lingine lijalo......as nothing will change much!

mwananchi wa Tanganyika!
 
Umeongea pointi za msingi sana.

Tena hata mimi hiyo siku nijitoa sadaka kwa kujikata na wembe au kisu sehemu yoyote ya mwili na dmu yangu itoke ili kuenzi na kusherehekea ukombozi kwa furaha pamoja na wanachadema na wanamabaliko wote walio tangulia mbele za haki!
 
Back
Top Bottom