Kama Nchi, tunafeli sana. Shida ni nini?

Kama Nchi, tunafeli sana. Shida ni nini?

Daisam

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2016
Posts
2,622
Reaction score
3,144
Ndugu zanguni, kila Mtanzania anajua jinsi rasilimali za Nchi yetu zinavyochakazwa na WAHUNI siku hizi.
Kila unapogusa pana upigaji mrefu kabisa. Watu wanakosa huduma za kijamii, na Wapigaji wanaongezeka kila uchao.

Juzi nilisema hapa kuwa, siku hizi vitendo vya WIZI, UFISADI NA RUSHWA vinafanyika waziwazi. Siyo kwa kificho tena. Vinafanyika waziwazi mchana kweupe pee.

Hii ni kwa sababu hakuna mtu anayeweza kuwawajibisha. Viongozi wetu wa Serikali hawana meno.
Vitendo hivi vinafanyika kwa ushirikiano mkubwa sana.

Utakuta ndani yake yupo RC, DC, Mkurugenzi, Mbunge, Waziri anayehusika, TAKUKURU, Hakimu/Jaji, TAKUKURU na wengineo.

Nchi yoyote ile ukiona Rais wa Nchi ni LEGELEGE ujue Watendaji wake wote walio chini yake watakuwa UJI UJI na wanakuwa hawana meno.

Kitakachofuata hapo ni Taifa kuchakaa kabisa na hatimaye kuingia kwenye machafuko.

RIP, OUR BELOVED FATHER, JPM.
 
Umeongea marefu ila hujataja hata kitu kimoja cha upigqji au mtu mmoja aliyekamatwa anapiga. Acha maelezo ya jumla jumla, weka facts kuonesha una uhakika na unachokisema. Wacha kuishi kwa kufata mikumbo vijiweni

Kwanza unasema kipindi hiki, je una uhakika kipindi kilichopita hakukuwa na upigaji? Kuna kipindi kimewahi kuwa bila upigaji Tanzania?
 
Umeongea marefu ila hujataja hata kitu kimoja cha upigqji au mtu mmoja aliyekamatwa anapiga. Acha maelezo ya jumla jumla, weka facts kuonesha una uhakika na unachokisema. Wacha kuishi kwa kufata mikumbo vijiweni

Kwanza unasema kipindi hiki, je una uhakika kipindi kilichopita hakukuwa na upigaji? Kuna kipindi kimewahi kuwa bila upigaji Tanzania?
Nakusamehe tu, yawezekana wewe unaishi Urusi au Ukraine kwa hiyo hujui kinachoendelea hapa Nchini.
 
Nakusamehe tu, yawezekana wewe unaishi Urusi au Ukraine kwa hiyo hujui kinachoendelea hapa Nchini.
Huna haja kunisamehe

Nimekushauri tu weka facts baaaasi. Unisamehe nimekuomba msamaha mimi?

Mbona rahisi tu, we Sema fulani aliiba shilingi fulani na huyu aliiba kiasi kadhaa. Sijakubishia kuhusu upigaji inawezekana upo ila kwakuwa umeamua kulileta hapa maana yake una ushahidi mwenzetu. Tunahitaji tuchangie mada yako. Tupe uwanja wa kuchangia.

Usitataje awamu hii ukaacha hii, awamu zote zinakuwaga na upigaji na pengine hizo zingine ushahidi upo.
 
Ndugu zanguni, kila Mtanzania anajua jinsi rasilimali za Nchi yetu zinavyochakazwa na WAHUNI siku hizi.
Kila unapogusa pana upigaji mrefu kabisa. Watu wanakosa huduma za kijamii, na Wapigaji wanaongezeka kila uchao...
  1. Kupeana uongozi kwa misingi ya undugu, urafiki, ushost, ukanda badala ya creativity na perfomance
  2. Uchawa wa kusifiana sana hata kwa makosa ya waziwazi
  3. Ufuatiliaji hafifu katika utekelezaji wa majukumu kwa waandamizi
  4. Sheria zetu ni butu hasa kwenye kuwachukulia hatua wabadhirifu wa mali za umma
  5. Bunge na Mahakama kuingiliwa na mhimili wenye kitita
  6. Elimu yetu in ualakini, inakosa continuity, kila Waziri huja na mambo yako matokeo ni ku swing kama bembea
  7. Huduma za jamii ni hafifu na hivyo kuathiri kwa kiasi kikubwa uzalishaji mali
  8. Uadilifu siyo sehemu ya maisha yetu, tamaa na ubinafsi umechukua nafasi kubwa kuliko utu kwa walio wengi
  9. Wataalamu waliopo hawapewi nafasi kutuletea mabadiliko badala yake wanatumika kisiasa zaidi
  10. Mentality ya kutegemea misaada imetudumaza
  11. Mawazo mapya yenye tija kuchukuliwa kama threat kwa nafasi za wakubwa
 
Ndugu zanguni, kila Mtanzania anajua jinsi rasilimali za Nchi yetu zinavyochakazwa na WAHUNI siku hizi.
Kila unapogusa pana upigaji mrefu kabisa. Watu wanakosa huduma za kijamii, na Wapigaji wanaongezeka kila uchao...
Hujui Kweli kwa nini Maendeleo ni kikwazo?
Shida ni hii:
= Kuchagua Rais anayetoka Chama cha CCM
= Rais akishindwa kazi fukuza
= Ujue unapopoteza miaka mitano unapoteza muda Katika maisha yako 5 years is almost your entire life on Secondary and High school levels - a planning time for your life
= Usimuonee huruma Rais au kiongozi

We live ONLY ONCE!!! Presidents and other elected leaders are appointed and encouraged by our leniences
 
Ndugu zanguni, kila Mtanzania anajua jinsi rasilimali za Nchi yetu zinavyochakazwa na WAHUNI siku hizi.
Kila unapogusa pana upigaji mrefu kabisa. Watu wanakosa huduma za kijamii, na Wapigaji wanaongezeka kila uchao...
Lucky enough ameshakufa..

Haya tuonyeshe ufisadi japo sekta Moja tuu vinginevyo Ni majungu yanakusumbua.

Mwisho wewe Hadi saizi umefisadi shilingi ngapi?
 
  1. Kupeana uongozi kwa misingi ya undugu, urafiki, ushost, ukanda badala ya creativity na perfomance
  2. Uchawa wa kusifiana sana hata kwa makosa ya waziwazi...
Hakuna popote Duniani ambapo wanaojuana wananyimana uongozi..

Mathalani Trump alimpa mtoto wake Uongozi na hata kama utasema ana uwezo kwani yeye ndio mwenye uwezo pekee?
Rais alitumia nafasi yake kumpa uongozi na hata huku kwetu nafasi za uteuzi ziko hivyo..

Mwisho Jambo kuu la Uadilifu,bahati mbaya jamii kubwa ya Watzn sio waadilifu Sasa unategemea Nini? Ukijifanya muadikifu peke yako utaishia pabaya..
 
Back
Top Bottom