Kama Ilani za Uchaguzi zina maana, hii bomoa bomoa imeelezwa wapi katika Ilani ya CCM?

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,344
Tangu serikali ya awamu ya tano ianze mpango wa kubomoa nyumba za wananchi zilizojengwa mabondeni na sehemu zisizoruhusiwa ilinilazimu kuipitia kwa makini ilani ya uchaguzi ya CCM ili kuona jinsi utekelezaji wa jambo hili ulivyofafanuliwa.

Katika ilani hii ya uchaguzi ya CCM nimegundua kwamba suala la bomoa bomoa halimo na halikuwa kipaumbele cha chama hicho.

Katika pitia pitia yangu ya ilani za uchaguzi za vyama vya siasa vya nchi mbali mbali nimegundua kwamba ilani ya uchaguzi ndiyo mwongozo wa chama kinachoshika dola na wakati wote wa kampeni wagombea huhubiri na hutembea juu ya ilani za uchaguzi za vyama vyao.

Tukichukulia kwa mfano, wakati wa kampeni ya Rais Baraka Obama aliasisi na kuuingiza katika ilani ya uchaguzi wa chama cha Democrats, mpango uliojulikana kama Obama Care uliokuwa wa kutoa huduma bure ya afya kwa watu wa hali ya chini. Ingawa mpango huu haukuwapendeza sana matajiri wa Marekani kwa sababu ndio wachangiaji wakubwa wa mpango huo, Obama aliusimamia tangu wakati wa kampeni mpaka wakati wa kupitishwa kwake kwenye bunge.

Kwetu huku ni kinyume, Magufuli wakati wa kampeni yake hakusema chochote kuhusu bomoa bomoa aliyoianzisha ili wapiga kura wampime na wafanye maamuzi kutegemea na kauli zake. Wakati wa kampeni zake aliahidi mengine lakini sasa anafanya mengine ambayo hakuwahi kuahidi, inaudhi sana.

Katika hili nadhani hawatendei haki watanzania.
 
Tangu serikali ya awamu ya tano ianze mpango wa kubomoa nyumba za wananchi zilizojengwa mabondeni na sehemu zisizoruhusiwa ilinilazimu kuipitia kwa makini ilani ya uchaguzi ya CCM ili kuona jinsi utekelezaji wa jambo hili ulivyofafanuliwa.

Katika ilani hii ya uchaguzi ya CCM nimegundua kwamba suala la bomoa bomoa halimo na halikuwa kipaumbele cha chama hicho.

Katika pitia pitia yangu ya ilani za uchaguzi za vyama vya siasa vya nchi mbali mbali nimegundua kwamba ilani ya uchaguzi ndiyo mwongozo wa chama kinachoshika dola na wakati wote wa kampeni wagombea huhubiri na hutembea juu ya ilani za uchaguzi za vyama vyao.

Tukichukulia kwa mfano, wakati wa kampeni ya Rais Baraka Obama aliasisi na kuuingiza katika ilani ya uchaguzi wa chama cha Democrats, mpango uliojulikana kama Obama Care uliokuwa wa kutoa huduma bure ya afya kwa watu wa hali ya chini. Ingawa mpango huu haukuwapendeza sana matajiri wa Marekani kwa sababu ndio wachangiaji wakubwa wa mpango huo, Obama aliusimamia tangu wakati wa kampeni mpaka wakati wa kupitishwa kwake kwenye bunge.

Kwetu huku ni kinyume, Magufuli wakati wa kampeni yake hakusema chochote kuhusu bomoa bomoa aliyoianzisha ili wapiga kura wampime na wafanye maamuzi kutegemea na kauli zake. Wakati wa kampeni zake aliahidi mengine lakini sasa anafanya mengine ambayo hakuwahi kuahidi, inaudhi sana.

Katika hili nadhani hawatendei haki watanzania.
Vipi kuhusu Guantanamo?
 
Rejea vizuri ahadi za Maghufuli, aliahidi kusimamia sheria za nchi, na watakaokiuka hatua zitachukuliwa. hataonea aibu mtu. Ndiyo maana safari hii hata maghorofa ya vigogo yanang'olewa. alifika mahali akasema waliosababisha ukiukwaji sheria hatawahamisha atawafukuza kazi. na kweli tumeona. Ndugu bomoa bomoa ni eneo dogo ktk uvunjifu Wa sheria ambao upon ktk nyanja nyingi.
 
Anaposema atafata utawala wa sheria maana yake kisheria hutakiwi kujenga usiporuhusiwa.
Anapoahidi kulinda mazingira maana take fukwe na vyanza vya maji nilazima vilindwe na watu wasijenge kwenye vyanzo hivyo
Anaposema atalinda maisha na Mali za watanzania maana yake wanaojenga mabondeni nivema wahamishiwe sehemu salama.
upo hapo au unashupaa!!
tunaitaka serikali sasa iendeshe zoezi kwa busara na kufuata sheria kikamilifu bila kuteleza.
 
Tangu serikali ya awamu ya tano ianze mpango wa kubomoa nyumba za wananchi zilizojengwa mabondeni na sehemu zisizoruhusiwa ilinilazimu kuipitia kwa makini ilani ya uchaguzi ya CCM ili kuona jinsi utekelezaji wa jambo hili ulivyofafanuliwa.

Katika ilani hii ya uchaguzi ya CCM nimegundua kwamba suala la bomoa bomoa halimo na halikuwa kipaumbele cha chama hicho.

Katika pitia pitia yangu ya ilani za uchaguzi za vyama vya siasa vya nchi mbali mbali nimegundua kwamba ilani ya uchaguzi ndiyo mwongozo wa chama kinachoshika dola na wakati wote wa kampeni wagombea huhubiri na hutembea juu ya ilani za uchaguzi za vyama vyao.

Tukichukulia kwa mfano, wakati wa kampeni ya Rais Baraka Obama aliasisi na kuuingiza katika ilani ya uchaguzi wa chama cha Democrats, mpango uliojulikana kama Obama Care uliokuwa wa kutoa huduma bure ya afya kwa watu wa hali ya chini. Ingawa mpango huu haukuwapendeza sana matajiri wa Marekani kwa sababu ndio wachangiaji wakubwa wa mpango huo, Obama aliusimamia tangu wakati wa kampeni mpaka wakati wa kupitishwa kwake kwenye bunge.

Kwetu huku ni kinyume, Magufuli wakati wa kampeni yake hakusema chochote kuhusu bomoa bomoa aliyoianzisha ili wapiga kura wampime na wafanye maamuzi kutegemea na kauli zake. Wakati wa kampeni zake aliahidi mengine lakini sasa anafanya mengine ambayo hakuwahi kuahidi, inaudhi sana.

Katika hili nadhani hawatendei haki watanzania.
lazima kuna mahali wamezungumzia kuhusu makazi bora na mipango miji. basi hapo hapo ndio bomoabomoa inaingia. kama unadhani wangesema watabomoa nyumba ya mtu sahau.
 
Utakuwa hujuisoma ilani ya chama cha mapinduzi wewe. Anyway Tafuta kipengele cha "MAKAZI NA MIPANGO MIJI" kuhakikisha miji imepangiliwa vizuri. Pia issue kuu ni CCM kuhakikisha usalama wa watu wake hivyo kuwataka wahame mabondeni nk

Waandishi wengi wa habari wako buzy na madhara ya BOMOA BOMOA, wana macho lakini hawaoni. Mbona hawazungumzii madhara ya kuishi mabondeni na watu wangapi wamepoteza maisha sababu ya mafuriko na mfumuko wa magonjwa.

MWANDISHI YOYOTE WA HABARI ANAYEZINGATIA UELEDI NA UZALENDO HAWEZI KILA SIKU KUANDIKA HABARI YA UPANDE HUO MMOJA TU WA MADHARA YA BOMOA BOMOA. Naona gazeti la Mwananchi na Nipashe hiyo ndio kick yao front pg kila siku!!!!!!!!!

Queen Esther

Tangu serikali ya awamu ya tano ianze mpango wa kubomoa nyumba za wananchi zilizojengwa mabondeni na sehemu zisizoruhusiwa ilinilazimu kuipitia kwa makini ilani ya uchaguzi ya CCM ili kuona jinsi utekelezaji wa jambo hili ulivyofafanuliwa.

Katika ilani hii ya uchaguzi ya CCM nimegundua kwamba suala la bomoa bomoa halimo na halikuwa kipaumbele cha chama hicho.

Katika pitia pitia yangu ya ilani za uchaguzi za vyama vya siasa vya nchi mbali mbali nimegundua kwamba ilani ya uchaguzi ndiyo mwongozo wa chama kinachoshika dola na wakati wote wa kampeni wagombea huhubiri na hutembea juu ya ilani za uchaguzi za vyama vyao.

Tukichukulia kwa mfano, wakati wa kampeni ya Rais Baraka Obama aliasisi na kuuingiza katika ilani ya uchaguzi wa chama cha Democrats, mpango uliojulikana kama Obama Care uliokuwa wa kutoa huduma bure ya afya kwa watu wa hali ya chini. Ingawa mpango huu haukuwapendeza sana matajiri wa Marekani kwa sababu ndio wachangiaji wakubwa wa mpango huo, Obama aliusimamia tangu wakati wa kampeni mpaka wakati wa kupitishwa kwake kwenye bunge.

Kwetu huku ni kinyume, Magufuli wakati wa kampeni yake hakusema chochote kuhusu bomoa bomoa aliyoianzisha ili wapiga kura wampime na wafanye maamuzi kutegemea na kauli zake. Wakati wa kampeni zake aliahidi mengine lakini sasa anafanya mengine ambayo hakuwahi kuahidi, inaudhi sana.

Katika hili nadhani hawatendei haki watanzania.
Tangu serikali ya awamu ya tano ianze mpango wa kubomoa nyumba za wananchi zilizojengwa mabondeni na sehemu zisizoruhusiwa ilinilazimu kuipitia kwa makini ilani ya uchaguzi ya CCM ili kuona jinsi utekelezaji wa jambo hili ulivyofafanuliwa.

Katika ilani hii ya uchaguzi ya CCM nimegundua kwamba suala la bomoa bomoa halimo na halikuwa kipaumbele cha chama hicho.

Katika pitia pitia yangu ya ilani za uchaguzi za vyama vya siasa vya nchi mbali mbali nimegundua kwamba ilani ya uchaguzi ndiyo mwongozo wa chama kinachoshika dola na wakati wote wa kampeni wagombea huhubiri na hutembea juu ya ilani za uchaguzi za vyama vyao.

Tukichukulia kwa mfano, wakati wa kampeni ya Rais Baraka Obama aliasisi na kuuingiza katika ilani ya uchaguzi wa chama cha Democrats, mpango uliojulikana kama Obama Care uliokuwa wa kutoa huduma bure ya afya kwa watu wa hali ya chini. Ingawa mpango huu haukuwapendeza sana matajiri wa Marekani kwa sababu ndio wachangiaji wakubwa wa mpango huo, Obama aliusimamia tangu wakati wa kampeni mpaka wakati wa kupitishwa kwake kwenye bunge.

Kwetu huku ni kinyume, Magufuli wakati wa kampeni yake hakusema chochote kuhusu bomoa bomoa aliyoianzisha ili wapiga kura wampime na wafanye maamuzi kutegemea na kauli zake. Wakati wa kampeni zake aliahidi mengine lakini sasa anafanya mengine ambayo hakuwahi kuahidi, inaudhi sana.

Katika hili nadhani hawatendei haki watanzania.
 
Weeengi wa hii nchi (I mean viongozi wetu) wanasifa kubwa ya unafiki, Leo wanaahidi hivi na kesho wanatekeleza vile. leo wanalalamikia hili na kesho wanasifia kile kisicho na hata tija kwa mhusika, ama kweli huu ni wakati wa kweli wa kuisoma namba has akwa wale aliokua hawana ufahamu wa kujua ni lipi wanapaswa kufanya kwa mustakbali wa maisha yao.
Taunajua kura za kweli zilikua ni ngapi na matokeo ya KUSTAAJABISHA yalikuja vipi, ila nani ni nani ndani ya hii nchi???? hilo ndo swali la msingi. Leo badoo elimu ya bura ni changamoto kuuubwa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini kwa kua tu hii ilikua ni sehemu ya ilani kamili ya UKAWA NA ccm wakadandia gari kwa mbelebaada ya kuona UKAWA wanapata shangwe kibaaoa kwa ilani hii. Leo watanzania wanavunjiwa bil kuandaliwa pa kuishi, huu utaratibu wa wapi?????? kama si kutafuta laana tu kwa Mwenyezi???? kuna watoto wasiyo na hatia maskini wasiojiweza na watu waliozaliwa na kukulia huko mabondeni hadi wamekua na wana familia tena kuuubwa tu, eti leo gafla bi vuuuuuuuuuuuuuu tingatinga hilooooooooooo linapiga nyumba chini, wakaishi wapi?? wakapike wapi???? hata kama elimu ni bure hao watoto wasome vipi???? JPM, JP, JPM, JAPO TAYARI UPO JUU KWA KADIRI YA ULIVYOWEKWA NA WALIOKUWEKA ila chonde chonde si kila jambo unapaswa kukaza hivi. Wachache wenye maisha nafuu wanakusifia kinafiki wakati weeengi wenye maisha duni wanakulaumu sana bila wewe kufahamu maana si MUNGU uletewe taarifa ya kila jambo.
 
Binafsi naamini kuishi mabondeni si tatizo hata kidogo, ila kwa kulitazama suala hili kwa haraka haraka na kwa akili zetu zilizodumaa tunaliona kama ni tatizo kubwa sana linalohitaji mamilioni ya pesa kulitatua.

Tunaliona suala la kuishi mabondeni kama ya Msimbazi kama ni tatizo kwa sababu tu ya umaskini wetu na serikali kutokuwa na mipango mizuri ya kuwasaidia wananchi wake isipokuwa kuwabomolea eti ndio kuwasaidia kuondokaba na mafuriko.

Badala ya kuwavunjia nyumba watu waishio mabondeni ambao wengi wao ni wananchi wa hali ya chini wasio na uwezo wa kupata viwanja sehemu salama ambazo karibu zote zimeishahodhiwa na viongozi na vigogo, serikali ingeweza kufanya jambo moja; ingeweza kuwahamisha wakazi wachache walio pembezoni mwa mito na ikatengeneza miundo mbinu iliyo imara kwa kujenga kuta na mifereji mipana ya kupitisha maji ya mito kwenda baharini na wanachi wakaachwa.

Ukienda katika nchi kama Netherland, nchi pekee duniani iliyo chini ya usawa wa bahari, utashangaa jinsi wao walivyotengeneza miundo mbinu na walivyodhibiti maji yasiifurikishe nchi.

Naamini serikali yetu ingekuwa bunifu isingekuwa na haja ya kuwavunjia watu wake makazi, wangeandaa mpango mkakati wa muda mrefu wa kuyaboresha mabonde hayo kuwa makazi.

Naamini mabonde haya haya tunayoyaona leo ni hatarishi kwa maisha ya binadamu miaka ya mbeleni na siyo mbele sana yatakuwa ni maeneo hot cake kuishi kutokana na maendeleo ya wakati huo.
 
Katika ilani hii ya uchaguzi ya CCM nimegundua kwamba suala la bomoa bomoa halimo na halikuwa kipaumbele cha chama hicho.

C) Mipango miji
i. Programu ya kurasimisha na kuzuia makazi holela imeandaliwa mwaka 2012.
ii. Elimu ya urasimishaji na kuzuia makazi holela imetolewa katika mikoa mbalimbali;
 
Chadema
4.2.9. Kulipa kipaumbele suala la hifadhi na ulinzi wa mazingira katika mipango yote ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
 
siasa za ccm huwa zinafuata mkumbo au fikra za kiongozi aliyepo madarakani , hakuna cha ilani wala nini , Mwinyi alileta RUKSA ambayo haikuwemo kwenye ilani yao.
 
Back
Top Bottom