Jinsi ya kuboresha usomaji vitabu

Jinsi ya kuboresha usomaji vitabu

masimango

Member
Joined
Dec 14, 2014
Posts
26
Reaction score
7
Habari za kazi wadau wa jukwaa hili

Ni matumaini yangu kuwa mnaendelea salama kabisa na juhudi za kulijenga Taifa letu.
Leo naomba tushirikiane kwenye hiyo mada tajwa hapo juu ili tuweze kuboresha usomaji wetu, usomaji huo unaweza kuwa wa vitabu au majarida mbalimbali.
Naomba kujua kwa wale wazoefu wa usomaji vitabu ni mbinu gani ambazo mnazitumia ili kusoma kwa ufanisi, kwa maana ya kusoma kwa kuelewa mantinki na maana ya kitu unachokisoma.

Kwa upande wangu mimi ni mpenzi sana wa kutaka kuwa msomaji vitabu lakini mara nyingi nimekutana na changamoto mbalimbali wakati wa kusoma vitabu. Kwa mfano kupata usingizi baada ya kusoma kurasa chache, kukosa hamu ya kusoma, kurudia kusoma baada ya muda mwingi kupita (nikisoma leo labda nakuja kuendelea kusoma wiki ijayo, hii inapelekea kusahau ulichokisoma nyuma), na mengine mengi.

Kwahiyo nalileta kwenu ili tushirikiane mawazo ni jinsi gani ya kuboresha usomaji vitabu ili tuwe wasomaji wazuri wa vitabu na kuongeza maarifa katika maisha yetu ya kila siku.

Naomba kuwasilisha kwenu mada hii.

Asante
 
Mimi nimejiwekea ratiba ya kusoma kurasa kumi kila siku, naandika kwa ufupi point na kuzitafakar. Na wewe kama utaweza tenga muda was kusoma vitabu kila siku, kwa kuanzia anza na kitabu chenye kuvutia ambacho hautamani kukiacha kusoma kujua nn kitatokea (chenye matukio ya kusisimua)
 
Mimi nimejiwekea ratiba ya kusoma kurasa kumi kila siku, naandika kwa ufupi point na kuzitafakar. Na wewe kama utaweza tenga muda was kusoma vitabu kila siku, kwa kuanzia anza na kitabu chenye kuvutia ambacho hautamani kukiacha kusoma kujua nn kitatokea (chenye matukio ya kusisimua)
ok asante sana kaka kwa ushauri, ntaufanyia kazi
 
Usomaji wa vitabu upo wa aina nyingi kulingana na msomaji na aina za vitabu anavyopenda.

Mm vitabu huwa naviCatagorize:

-Maarifa
-Burudani
-Challenge

Hapo huwa vinaingia vitabu vya aina nyingi, na huwa nasoma kulingana na muda na mood pia,

Nikiwa sijachoka akili wala mwili naweza kusoma aina zote hapo juu..

...nikiwa nimechoka ila nahitaji kusoma kwa ajili ya kitu fulani basi shelf ya "Maarifa" lazima niipitie,

...nikiwa bored naweza kusoma vya "Maarifa na burudani"

...nikiwa safarini napendelea kusoma vya "burudani na challenge" ili akili iwe busy na kitabu,

Kwahiyo ktk usomaji ni mtu tu na jinsi anavyopenda kuoangilia mambo yake, nina tabia ya kurudia vitabu pia....nikimaliza kusoma kitabu huwa naandika ktk list ya vitabu nilivyosoma na kama nimekipenda nitakiHIGHLIGHT na hata kukichambua kwa ufupi zaidi ili nikielewe zaidi.

Usomaji wa vitabu ni mzuri sana hupanua ubongo na kuufanya uwe unaweza kufikiria mambo mapya na magumu zaidi.

Natumai nimeeleweka kidogo.
 
Usomaji wa vitabu upo wa aina nyingi kulingana na msomaji na aina za vitabu anavyopenda.

Mm vitabu huwa naviCatagorize:

-Maarifa
-Burudani
-Challenge

Hapo huwa vinaingia vitabu vya aina nyingi, na huwa nasoma kulingana na muda na mood pia,

Nikiwa sijachoka akili wala mwili naweza kusoma aina zote hapo juu..

...nikiwa nimechoka ila nahitaji kusoma kwa ajili ya kitu fulani basi shelf ya "Maarifa" lazima niipitie,

...nikiwa bored naweza kusoma vya "Maarifa na burudani"

...nikiwa safarini napendelea kusoma vya "burudani na challenge" ili akili iwe busy na kitabu,

Kwahiyo ktk usomaji ni mtu tu na jinsi anavyopenda kuoangilia mambo yake, nina tabia ya kurudia vitabu pia....nikimaliza kusoma kitabu huwa naandika ktk list ya vitabu nilivyosoma na kama nimekipenda nitakiHIGHLIGHT na hata kukichambua kwa ufupi zaidi ili nikielewe zaidi.

Usomaji wa vitabu ni mzuri sana hupanua ubongo na kuufanya uwe unaweza kufikiria mambo mapya na magumu zaidi.

Natumai nimeeleweka kidogo.
Asante sana kaka, nashukuru kwa mchango wako mzuri
 
Usomaji wa vitabu mara nyingi ni hulka ya mtu, unaweka ratiba yako namna ya kusoma, pia kama hua unasafiri safiri basi beba vitabu ,
Binafsi nimesoma vitabu vingi nikiwa safarini
 
Back
Top Bottom