Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,843
SIMULIZI HII IMEKAMILIKA
IMEANDIKWA NA : ZUBERI MARUMA
CHANZO : BURE SERIES
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI
JOHN VERGAN kijana anayemiliki kampuni kubwa na mwenye mafanikio makubwa katika maisha yake anadondokea katika penzi la mtoto mrembo mwenye asili ya kishombeshombe HUSNA ambaye ni jini!
VERGAN akubali kuwa na HUSNA baada ya kugundua si binadamu heka heka,vituko,uzuni vinamuandama je atafanikiwa kuokoka katika kisanga cha jini huyo mpole na mwenye hasira za karibu?
fuatana nami mwanzo mpaka mwisho wa riwaya hii itakayokuburudisha-..,..
TUANZE
1
Ulikuwa ni ukumbi mkubwa ulojaa watu wenye hela zao, kila starehe iliyopo katika dunia hii ilikwepo hapo kasino ilo lilijaa wadachi,waindi,
walokuwa wakijiuza.
mziki mkubwa ulikuwa ukiendelea kuwaburudisha wateja wa club hiyo
kulikuwa kuna walinzi wa kutosha,walokuwa tayari kupambana na kiumbe chochote kitakachotaka kuleta shida
gari aina mbali mbali za kitajiri ziliingia na kutoka na wasichana warembo ni ukumbi ulosifika kwa matanuzi yote uyatakayo
JOHN VERGAN kama mwenyewe alivyopenda kujiita alikuwa counter akitupia pombe yake taratibu!
machangudoa wachache walijipitisha mbele yake lakini ilo wala akulijali wengine awakuishia kujipitisha tu kwani walimfata na kutaka kutoa company
lakin VERGAN hakuwa tayari, mawazo yalitawala kichwa chake aligubia bia kwa fujo aikujulikana kipi kilichomtesa kijana huyo mwenye umbo la wastani
si mrefu sana wala si mfupi sana,maji ya kunde mwenye body sex mwili wa mazoezi alikuwa na kila mvuto wa kimapenzi kwa mwanamke amwangaliaye!
wanawake wengi sana walimmezea mate lakin moyoni mwake alikwepo mwanamke mmoja tu MOURINE
huyu ndo alomfanya VERGAN Agubie ile bia kwa hasira na hisia tele MAPENZI yalimtesa alimpenda mtu asiyempenda tena secretary wake
macho yake makubwa yaliyozungukwa na nyuzi nyembamba nyeusi yalitua mkononi mwake alivaa saa ya dhahabu iliyosomeka ni saa sita na nusu usiku akashusha pumzi taratibu ni wazi alishachoka na usingizi ulishaanza kuyanyemelea macho yake kilevi kilishaanza kumlevya
Akaishika simu yake na kuibonyeza tarakimu kadhaa akaiweka maskioni....
"simu unayopiga haipatikani tafadhali jaribu tena badae"
ndiyo kauli ilojibu upande wa pili JOHN VERGAN akakunja sura kwa hasira,akaachia mguno wa fedheha
Akashika chupa yake na kugubia kile kinywaji alipoishusha chini ilikuwa tupu
Kwa vyovyote muda ule MOURINE asingeweza kuja
Akaamua kujinyanyua zake akiwa anapepesuka taratibu na kuelekea nje kwa hatua fupi aliendea gari yake na kujipakia ndani
toka jioni alikwepo katika hoteli ile mpaka muda ule aliiwasha gari na kuiondoa kwa kasi.
*************
MOURINE msichana mrembo kiumbo na secretary wake VERGAN akiwa ndani ya gari yake jioni hii moyoni mwake alikuwa na raha sana! kitendo cha BOSI wake kumuitaji hotelini kilimpa faraja,ni kweli alimpenda bosi wake yule, na bosi wake alishamwonesha ishara zote za kumpenda,
Hakutaka kumkubali kwa kutopenda kuonekana mrahisi ila siku hii ya leo alijihisi hali flan si ya kawaida alijihisi KUMPENDA na kuitaji kuwa pamoja naye kimapenzi hisia zile zikamfanya aongeze mwendo wa gari lake kumuwai mwanaume yule
Lakini ghafla akiwa katika mwendo mkali akakatisha mwanamke mrembo mbele ya gari,
MOURINE akajaribu kupiga break huku akiachia yowe ns kufumba macho yake ila breki ikakataa na gari likamvaa dada yule
MOURINE akiwa kachanganyikiwa huku alitetemeka baada ya kujiisi kumgonga mtu yule akashuka kwa speed mpaka mbele ya gari lake
AKUKUWA NA MAITI WALA MDADA MOURINE akashtuka!
kwa haraka akarudi garini na kujaribu kuwasha gari GARI LIKAGOMA, akazidi kuchanganyikiwa
Akashika simu yake nayo kwa ajabu ikawa imezima chaji,safari ya MOURINE ikawa imefia hapo.
************
BADO JOHN VERGAN moyo wake ulijaa simanzi ghafla akiwa kwenye mwendo wa wastani mbele yake akamuona msichana mrembo,
msichana alozivuta na kuziamisha HISIA zake akazidi kupunguza mwendo wa gari na alipo mfikia dada yule kabla ajamsemesha dada yule akamuwahi
"kaka naomba lifti"
VERGAN akujibu swali lile kwani akili yake ilikuwa katika umbo zuri la mrembo yule!
umbo namba nane,mwenye asili ya kiindi akika alikuwa na mvuto wa ajabu,
"mimi naita JOHN mwenzangu sijui unaitwa nani?"
dada yule ndani ya gari alikaribishwa na swali
"MIMI NAITWA HUSNAT"....
Macho ya VERGAN yalikuwa katika mapaja mazuri yalokuwa wazi wakati huo,
binti yule aliyejitambulisha kama HUSNAT alivaa kimini kidogo kilicho acha mapaja yake wazi! kutokana na msukumo wa pombe VERGAN alijikuta akishindwa kuzizuhia HISIA zake nzito kwa dada yule!
akamtongoza!
dada yule akuwa na kizuizi VERGAN akimchukulia kama changudoa akaelekea naye katika nyumba yake,
akiwa na mwanamke yule ndani ya gari alipania kulala naye usiku mzima katika jumba lake lile akilifaidi penzi lake!
Akazidi kuongea mwendo kurudi afike haraka!...
LAITI ANGEJUA!?....
**************
Ilikuwa ni nyumba kubwa na ya kifahari gari aliyepanda VERGAN na msichana mrembo HUSNAT iliingia mpaka parking
VERGAN akiwa kamshika mkono binti yule wakatoka na kuelekea sebuleni ambapo awakukaa sana wakaelekea chumbani
wakapanda kitandani kila mmoja akionekana kumuitaji mwenzake zaidi!
VERGAN katu akuziona kwato zilizokuwa katika miguu ya bibie yule!
Pia hakuyaona macho yake ya kung'aa katika giza kwa macho yake ya kawaida aliyaona kawaida!
wakazama penzini!
penzi ambalo katu VERGAN hakuwai kulipata kwa binadamu wa kawaida,
penzi liliyomlevya na kumpa usingizi mzito,baada ya VERGAN kulala jini HUSNAT akuwa na muda wa kupoteza akavaa nguo zake zote akanyoosha mkono wake juu barua ikatokea akaiweka pale kitandani na GHAFLA AKATOWEKA!!!
Ilikuwa ni alfajiri tulivu ilojaa kibaridi VERGAN alipapasa mbele yake hapakuwa na mtu, akafumbua macho yake taratibu kajua cha asubuh kalitokeza kutarifu sasa kumepambazuka,
VERGAN alishtuka na kucheki mlango
"UKUFUNGULIWA"
Akakumbuka juu ya kukutana na HUSNA jana
"au nilikuwa naota?! hapana!"
bado VERGAN alikuwa katika hali za sintofahamu akakurupuka kitandani pale akiita kwa nguvu kama mweu
"HUSNA! HUSNA! HUSNA!" Bado hakukuwa na jibu! akaingia chooni,bafuni ndani kwa ndani bado akukuwa na mtu!,
vergan akiwa kama kachanganyikiwa akafungua mlango na kutoka nje alipomkuta mlinzi wake kipele
"umemuona msichana katoka humu ndani asubuhi hii?" Akauliza kwa wahka
"msichana? msichana yupi bosi?" Kipele akasaili....
"yule nlokuja naye jana usiku!"........
" Jana usiku?!"
Kipele akaoji huku bumbuwazi likimbumbukia usoni pale....
"Ndiyo yule binti nloshuka naye kwenye gari?!"
"No Bo's!,nliona ukishuka mwenyewe hukuja na mtu kaka"
"What?!"
"Ndiyo!,tena ulikuwa full ukipepesuka ukuja na mtu bosi"
"Mfyuuuuu!"
Vergan akaachia msunyo ulosindikizwa na mguno hafifu wa mfadhaiko
Ni wazi alizidi kuchanganyikiwa
!,akaenda sebuleni akajitupa sofani!,mawazo yakaanza kupishana kama mishale ya saa!!!
"uyu binti atakuwa kaenda wapi yarabi?! mbona mlango ukufunguliwa? mlinzi naye anasema sikuingia na mtu jana usiku au nilikuwa naota? hapana hapana hapana nilimpa binti lifti HUSNA alinambia anaitwa HUSNA nikampenda! nkamchukua nkaja naye akanipa penzi tamu ambalo sijawai kulipata alafu! alafu ikawaje? HUSNA! HUSNA! hapana si ndoto kuna kitu"
alijiuliza VERGAN na kujijibu mwenyewe akajinyanyua na kurudi tena chumbani
macho yakadondokea kitandani
Kitanda kilikuwa shaghala baghala kuonesha kwamba usiku kucha kilitumika,hilo likazidi kumpa picha sahihi kwa kile akiwazacho
macho yake yakatua mezani akakuta barua imefungwa vizuri
Akastaajabu!!!...
Kwa hatua fupi fupi akasogea pale kitandani huku mkono ukiwa unatetemeka akaifata barua ile na kuishika ilinukia harufu nzuri!,
harufu ya manukato,alikumbuka manukato hayo ni ya HUSNA
akaichukua ile barua na kuifungua na kuanza kuisoma naaam macho yalimtoka pima
"DEAR SAMAHANI! KWA KUONDOKA BILA KUKUTA HARIFU NILIHITAJIKA HARAKA NYUMBANI NA WAZAZI WANGU WAKWE ZAKO HASUBUHI NJEMA WAKO KIPENZI HUSNA NTARUDI"
ITAENDELEA