Je, siasa za ubabe, jeuri, kiburi ndio vipimo vya utendaji kazi mikoani?

Andrew Mushi

JF-Expert Member
Dec 13, 2016
630
696
Ninaanza kuingia hofu, ya uchapaji kazi wa viongozi wetu hususan viongozi wa kuteuliwa ktk ngazi ya mikoa na wilaya.

Nimegundua kitu kimoja, wengi wenye kutetea uchapaji kazi wa hawa viongozi wetu, ukiwauliza vielelezo vya msingi juu ya uchapaji wa kazi zao, hawakurudii na takwimu au vielelezo vya msingi vya maendeleo ktk sehemu zao za utawala. Kitu ambacho wote tunaweza kukiona.

Bali watakurudia na maneno yao waliyotamka, hususan maneno ya kibabe, ujeuri, vitisho, audio za majigambo, na wengine wameshaanza kuthubutu hata kuwapiga watu vibao, vitisho vya jela n.k

Sasa tukijichunguza, swala la msingi je hayo ndio maendeleo au huo tunaouita uchapaji kazi unatuhudhirishia vitu viwili kushindwa KIUWELEDI wa hao watendaji wa mikoa na wilaya au ama UBUNIFU wa jinsi gani ya kuratibu njia mbadala za uendeshaji wa halmashauri zetu kwa kutumia nyenjo na wataalam tuliokua nao ktk sehemu zao walizopangiwa, au yote mawili kwa pamoja.

Siasa za waliokua madarakani kutumia ubabe ktk majukumu yao, ndio imekua kama sehemu kubwa ya maongezi mitaani, na ni daraja ya kukutoa kisiasa.

Lakini tukija kwa mwananchi, changamoto na huduma za jamii ambazo ndio makusudi maalum ya utendaji wao kikazi, yako vile vile na yamezidi kuwa magumu, au kuna unafuu wowote huko mikoani, na hapa ndipo bado ninatafuta ushahidi.

Je tunahitajia ubabe wa kisiasa kuwa kiongozi safi hususan wilayani au mikoani au ubabe wa kisiasa?

Na je mikoani tunahitajia watendaji wake wawe ni wanasiasa au wawe technocrat zaidi, yaani wenye ufundi zaidi, kujua jinsi gani ya utendaji wao kazi, na siasa tuwaachie wabunge.

Kwa pointi ya mwisho hapo, Muheshimiwa Rais anapoteua Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi au Jaji hategemei akafanye siasa Bali ufanisi na utendaji wake, ndio aweze kuutumia zaidi, yaani technocrat na sio siasa zaidi, kwa majaji wetu naliona hilo kwa asilimia kubwa, kwa wakuu wa mikoa, naona siasa zaidi ya utendaji.


I sincerely hope I will be proven wrong sooner rather than later!
 
Kuna nafasi za kichama kama wakuu wa wilaya na mikoa, hawa ni extended arms ya chama kilichoko madarakani na utendaji wao kazi ni more of pleasing the master (Chama).
Hawa wanapokua na madaraka juu ya watendaji wa serikali nikimaanisha wakurugenzi na walio chini yao, just remember hawa makada wengi wao hawana sifa za utawala zaidi ya kupiga vumbi wakati wa kampeni.
Something need to be done.
 
Kuna nafasi za kichama kama wakuu wa wilaya na mikoa, hawa ni extended arms ya chama kilichoko madarakani na utendaji wao kazi ni more of pleasing the master (Chama).
Hawa wanapokua na madaraka juu ya watendaji wa serikali nikimaanisha wakurugenzi na walio chini yao, just remember hawa makada wengi wao hawana sifa za utawala zaidi ya kupiga vumbi wakati wa kampeni.
Something need to be done.

Nakubaliana na wewe Mkuu, madaraka isiwe ni sehemu ya kudhalilisha watu, kwani chama sio sehemu ya mikono ya dhulma juu ya haki ya wananachi au wale uliopewa dhamana juu yako, weledi huo kwa viongozi wetu kufahamu na kuzingatia hio principle , je wanao..

Na hapo naungana na wewe something has to be done ..
 
0a235b924463d3d9c0b241c513c0915d.jpg
 
Hao watendaji wanafuata style ya utendaji wa baba Sizonje. Ubabe, vitisho,dharau na majigambo ndio dira ya awamu hii
 
mtu anampigaje mtu vibao na kubaki kazin...kweli hii ni Africa.
 

Hapa ndiyo ile dhana ya Nitatokaje au Nitapandaje cheo ,ndipo unapoona huu upumbavu ukitokea.Sasa huyu inasemekana ni Mpwa wa Mkullu,mwache aprove kwa mjomba kwamba anaweza kazi ya Ukuu wa Wilaya.

Wamesahau kama UTAWALA ni dhamana ya muda mfupi sana,na kuna maisha baada ya uongozi
 
Ni kukosa akili na uweledi ndio maana wanatumia ubabe,kiongozi mwenye akili timamu awezi kumpiga mtu makofi.
 
Kuna mkuu wa wilaya huko Njombe anaitwa Ruth Msafiri anapiga watu makofi hadharani na kisha kuamuru aliyepigwa makofi awekwe ndani saa 48. Jana kamtwanga makofi mwenyekiti mmoja wa serikali za mitaa na kuamuru awekwe ndani saa 48. Kisa eti, hastahili na amepoteza sifa za kuwa kiongozi.
 
fb2a428b553151598d7bec73960f755d.jpg


Tumefikia vipi hali ya uzembe na uchoshwaji wa watendaji kazi.

Je unawaweka ndani ? au unapambanua njia iliyobora na kuangalia uwezo wao wa ufanyaji kazi yao hao wakurugenzi wa halmashauri, kama uwezo wao hauendani na vipimo vya weledi wao kama maafisa wa ngazi husika basi pia ina njia za kuwawajibisha.. labda wanewekwa kifeva feva, ndio tunarudi kwenye swali la awali hapo juu..tumefikaje hapa?

Lakini hata hivyo ktk job description ya ukuu wa wilaya sidhani kama kipengele cha kuwaweka watumishi wako rumambe au kuwadhalilisha kwa umma, kwa hio uzembe wao sio sababu ya kigezo cha kuwa judge wa kuwaseka rumande, yaani tunajiweka juu ya sheria na mahakimu juu ya wengine, ijapokua majukumu ya kazi haijaelezea hayo, bila kufuata due process, na hapa hatutetei uzembe, bali misingi ya sheria na haki.

Mzembe wa kazi, rudia disciplinary procedures ziko kule HR office, ikiwa kuwapa warnings au uwafukuze kazi accordingly. Mbona hiki chepesi wanajitoa Ufahamu.
 
Jamani ndo unasikia Mungu mtu ivi viongozi wetu wateule mnatambua kuna maisha baada ya teuzi zenu,ninawasiwasi na weledi wenu wa Kazi, mnatambua wajibu wenu na je mnatambua enzi za mwl viongozi walipewa heshima si kwa sababu nchi haikuwa na wasomi la hasha viongozi waliwaeshimu wananchi, Leo hii nyie hamueshimiwi ila mnalazimisha kuheshimiwa tena kwa nguvu ya dola. Mjitafakari rejeeni enzi za Mwl.
 
Back
Top Bottom