Je prof. Muhongo anashughulika na asichokijua?

Je prof. Muhongo anashughulika na asichokijua?

Joined
Sep 28, 2012
Posts
87
Reaction score
32
Kwamba yale maandamanona malumbano ya wana Mtwara na sasa Taifa zima kuingia katika mjadala juu ya uvumbuziwa gas yameungwa mkono na baadhi ya Wanasiasa wa upinzani na hata wachache wa CCM ni kweli. Kwamba Mkoawa Mtwara na mingineyo mingi wana umaskini iliokithiri ukilinganisha na minginenchini ni kweli pia. Hata hivyo, kwamba huyu Muhongo - Mwanadhuoni wa Chuo Kikuukutokuwa na uzoefu katika uchafu wa siasana mienendo ya makucha ya makaburu katika kutawala nchi changa / zinazoendelea;yeye na wengine wengi wataendelea kushughulika na moshi tu maana hawajaweza kugunduani wapi hasa moto umewashwa na kusudi la kuwasha moto huu ni nini?

Naombeni contactshuyu Waziri Mwanasayansi Muhongo ili nimwandikie mwenyewe kwa undani haya ambayo sisi wenye uzoefu tumeyabaini live na mtu yeyote alisilete mzaha katika hiitaarifa ambayo nitawapa Usalama wa Taifa na moja kwa moja kwa Rais Kikwete kama Mkuu wa nchi anayetakiwakuingilia kati kwa kuongea na wananchi huko Mtwara na kuhutubia Bungeni wa uwazizaidi maana madhara na nguvu zilizoko katika hili sakata yako juu sana zaidi yauwezo wa TPDC au Wizara ya Nishati na Madini. Nitaandika bila kuzunguka.

Waingerezawamedhamiria kuendelea kututawala ili mwishoni wao ndio wafaidi hii rasilimaliya gesi asilia iliyovumbuliwa nchini na nchi jirani kusini. Kwa kutumia mfumowao wa siku zote wa divide & rule wameanzakwa kutulisha dhamira ya "tutapigana mpaka kieleweke, maana sisi tumekuwa nyumakuliko wengine; kwanza wenye rasilimali tufaidi kabla ya wengine(Taifa)". Aliyewasha moto ni Balozi wa Uingerezanchini Bibi Diane Corner. Huyu mama aliyepitiakatika Chuo cha Ulinzi cha NATO mwaka 2000 ni mzoefu katika ama miradi ya kuwashamioto au kuizima baada ya vita kwa makubaliano ya kuanza kufaidi rasilimali zanchi changa. Kati ya miradi yake ya hivikaribuni iliyofanikiwa siku za nyuma alipopelekwa na kufanya kazi ni Zimbabwe (Harare)na Sierra Leone. Uzoefu wake umejengwa kwa muda mrefu alipokuwa Katibu mwandamizi katika dawati la mamboya nje katika nchi za Jumuiya ya Madola Afrika - Kati na Kusini.

Kwa kushirikana na makampuni makubwa ya mafuta yenye makaomakuu London, British Gas group & Ophir Energy ambayo yamekuwa yakifanyakazi ya kutafuta na kuzalisha gesi Tanzania na nchi kibao Afrika na katika mabaramatano, wamewasha moto kwa kugawa fedha nyingi kwa Viongozi wachache waupinzani (ving'angánizi wa umaarufu na walafi wa fedha) ambao ni Mgombea Uraisiwa kudumu kupitia tiketi ya CUF Prof. Lipumba na Kinara wa Masalia Msaliti Zitto aliyeomba msamaha wa kebehi bilakusema ambacho anatubu (tactical apology + fauxipology) na H. Murji, Mbunge wa CCMMtwara Mjini. Kwa walioshiriki maandamano wapo wachache waliogawiwa Tsh. 200,000 kila mmoja na wengine wenye ushawishimkubwa dau lao lilikuwa juu kidogo, lakini pia wapo wengi waliounga mkonopasipo kupewa taarifa juu ya huu mgao. Mgao bado uko mkubwa kwa viongozi wavyama ambao ni kati ya US$ 5,000 na 10,000 kutegemeana na umaarufu wa mtu.

Suala la msingi la kupigia mstari ni kuwa mradi wa bibiDiane utaendelea sana kwa kupanda mbegu ya chuki miongoni mwetu KUPITIA WANASIASA NA HATA NGO'S iliyasiwepo maridhiano katika jambo hili ili mwishoni tupigane na watatumiambinu zao kama kawaida hata kupenyeza siraha za moto ili tumalizane mapema. Nibayana kuwa hata ule mgogoro wa mpaka na Malawi si suala tu la mpaka wa nchi balini gesi na fedha ilisha mwagwa huko Malawi ndio maana kila siku Waziri Membe anagongaukuta na kututangazia kusogea hatua nyingine ya mbele ya ‘kukubalikutokubaliana' maana ingekuwa ni sisi wenyewe (Watanzania na Wamalawi) hakunashida lakini kwa kuwa kuna mkono wa fedha haramu za mababeru tunaongozwa kimyakimya kufika kule wenzetu wa Nigeria (Biafra & Niger Delta), Sudan, Sierra Leone,DRC n.k walipofikishwa.

Rais Kikwete chagua kama tunataka kuingia katika "bloody gas"au gesi asilia kwa ajili ya maendeleo yetu bila kuvuruga amani yetu. Wanahabarijiandaeni kutengeneza documentary kama ile ya Drilling & Killing by A.Goodman inayohusu Tz kama tutaziba pamba masikioni.

Kwamba, Tanzania ni moja kati ya nchi chache sana Afrika ambazo zina utajiri wa rasilimali asilia lakini hawajaruhusu kukaliwa na vituovya kijeshi vya Marekani wala Uingereza katika jina la kulinda amani ni jambo linalowakosesha usingizi makaburu wengi! Unataka, tafakari; hutaki acha na usubiri documentary ya
Drilling & Killing in Tanzania.
:fencing:
.
 
Hauna ukweli wowote wewe, sisi hatupigani ila tunasema hatutaki ujenzi wa bomba
 
Acha kutisha watu, kwani gas ikiwaprocessed Mtwara kama wananchi wanavyodai itageuka kuwa mali ya Waingereza?, unataka tuamini rasilimali yeyote iliyopo nje ya Dsm si mali ya Tanzania?
 
Mkuu!

Kwa hiyo wewe unachokijua unafikiri wenzako hawakijui?

Haya ni masuala ya kitaalamu sana na ni hatari na hao wanawadanganya wanamtwara wanafahamu kabisa umuhimu wa wataalamu lakini wanakwepa kuwatumia ama kudharau utaalamu wao sababu tu ama ya njaa zao ama kutafuta umaarufu.
 
Hauna ukweli wowote wewe, sisi hatupigani ila tunasema hatutaki ujenzi wa bomba


MKUU USIWE MKAIDI,UNAPOSEMA HUTAKI UJENZI WA BOMBA UNATAKA NINI HASA?

MBONA WAKAZI WA MWANZA,KAGERA NA MARA HAWAKUANDAMANA KUPINGA SERIKALI KUPELEKA MAJI YA ZIWA VICTORIA MKOANI SHINYANGA?

MBONA WENYEJI WA TANGA,MOROGORO,DODOMA NA MOSHI HAWAKUANDAMANA KUPINGA UPELEKWAJI WA NISHATI YA UMEME SEHEMU MBALIx2 ZA NCHI.?


MKING'ANG'ANIA SANA MTAONEKANA NI WATU WA AJABU SANA,KWANI SULUHISHO LA MWANAMTWARA SI GESI PEKEE BALI ELIMU NA MASUALA YA USTAWI WA JAMII BADO NI KIKWAZO KIKUBWA CHA NDUGU ZETU WALE.

MBONA KIPINDI KILE CHA MZEE MKAPA HAMKUAANDAMANA JUU YA MASUALA MENGINE YA MSINGI?
 
we mleta mada unadhani bado watu wanahadaika na hizo propaganda zako? watu wameamka sasa na wanajitambua, hivyo acha kupoteza muda wako kuandika upuuzi kama huo uliouleta
 
Haya ni mawazo yako, wengine watayakubali, wengine watayakataa, na sisi tunayapuuzia kwa sababu unaonesha huna busara, soma hii paragraph kutoka kwenye habari yako;

"Kwa kushirikana na makampuni makubwa ya mafuta yenye makaomakuu London, British Gas group & Ophir Energy ambayo yamekuwa yakifanyakazi ya kutafuta na kuzalisha gesi Tanzania na nchi kibao Afrika na katika mabaramatano, wamewasha moto kwa kugawa fedha nyingi kwa Viongozi wachache waupinzani (ving'angánizi wa umaarufu na walafi wa fedha) ambao ni Mgombea Uraisiwa kudumu kupitia tiketi ya CUF Prof. Lipumba na Kinara wa Masalia Msaliti Zitto aliyeomba msamaha wa kebehi bilakusema ambacho anatubu (tactical apology + fauxipology) na H. Murji:
 
Mleta mada ni mnafiki mkubwa kwa sababu na akili zako timamu umeona prof lipumba na zito ni waroho"hivi kwa akili yako nani ni mroho kati ya viongozi wanaosema mradi lazima uelekezwe dar au awa wenye ufahamu mkubwa wanaotaka process zifanyike mtwara?

Kama kutawaliwa na wazungu hakutaanzia mtwara wewe!!!!! Unataka tuendelee kuwaachia wanufaike wao tu na familia zao??kama umeliona kwani hukujui anakopatikana rais??au ufahamu hata sehemu zenye ofisi za usalama??

Acha kutuvunja moyo wewe mtwara tuendelee kukomaa mpaka kieleweke kama wamekutuma uwapunguze kasi watu wa jf its better ukaacha mambo yaendelee kuwa hot hivihivi ukitaka kuwe na amani mwambie viongozi wako wawatendee haki raia wote wa tanzania na wawasikilize wananchi wanataka nini.
 
Haya ni mawazo yako, wengine watayakubali, wengine watayakataa, na sisi tunayapuuzia kwa sababu unaonesha huna busara, soma hii paragraph kutoka kwenye habari yako;

Wewe ndiye umeonyesha busara kwa kutoa msamaha kwa msaliti ambaye hataji hata kakokosea nini?
 
Mleta mada ni mnafiki mkubwa kwa sababu na akili zako timamu umeona prof lipumba na zito ni waroho
"

Dunia yote yenye demokrasia ukijaribu mara mbili na kushindwa unawaachia wengine. Halafu kiongozi wa masalia katubu eti kakosea nini ebu nikumbushe na wewe unajifanya great thinker wakati unatoa msamaha kwa kile usichokijua!
 
Hauna ukweli wowote wewe, sisi hatupigani ila tunasema hatutaki ujenzi wa bomba

Kote walipopiganga walianza kwa kusema hatutapigana haya subiri uone kama wewe hutaki kujifunza. Ninachosema ni kuwa mradi wa hao watu si wa kutafuta suluhu toka upande wowote, bado huelewi!! unafikiria mimi naongelea hapa bomba!! Yaani kuna watu leo hii wanafikiri suala la mataifa makubwa kuingilia mafarakano ni nadharia halafu naye anajiita great thinker!
 
Back
Top Bottom