Wanajf, nakiri wazi kuwa mi ni kiongozi wa CHADEMA ngazi ya kata. kwakuwa mi ni kiongozi wa CHADEMA na kwa kuwa chama changu kimepengekeza serikali tatu namimi kama kiongozi ni halali kutetea msimamo wa chama changu kwani ni maamuzi ya vikao halali vya chama hivyo kwenda kinyume ni kukiuka katiba ya chama kwa kudharau maamuzi ya vikao halali vya chama. Vilevile mi kama kiongozi itabidi nitetee maamuzi ya chama mbele ya wananchi. Lakini kwangu binafsi nakubaliana na hoja ya serikali moja ambayo binafsi naona kama ndo chanzo cha kuondoa matatizo ya muungano kabisa na niko tayari kutetea hili kwa nguvu zote na kwa ujasiri wote na kama inashindikana basi si lazima Tanganyika kuungana na Zanzibar hivyo basi kama kuna upande hautaki serikali moja basi kila nchi ijitegemee kama nchi huru. Hapa mtanisaidiaje, je nitetee maamuzi ya chama changu au nitetee dhamira yangu?. Naomba kuchangia kwa nidhamu ili nipate pa kusimamia ndugu zangu.