Je, ni kwamba NSSF wana ubaguzi?

Je, ni kwamba NSSF wana ubaguzi?

akatanyukuile

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2019
Posts
314
Reaction score
308
Kama kichwa cha habari kinavojieleza,

Ninapenda kuomba msaada kwa wenye uelewa wowote ili nipate kujua ni kwamba nilikua nikifuatilia mafao yangu, nilikamilisha taratibu zote wanazozitaka baadae nikaahidiwa kuwekewa pesa zangu baada ya mwezi mmoja, la kushangaza mda ulipofika niliwekewa kiwango kidogo sana tofauti na nilivotarajia, nilipo jaribu kuuliza niliambiwa ndo utaratibu mpya wa malipo yakua unalipwa asilimia 33 kwa mda wa miez 6 tu.

Nilijaribu kuuliza tena inakuaje majibu nimekua nikipata ambayo hayaridhishi, sasa juzi tu rafiki yangu naye ambaye yeye anakaa Ilala mimi nipo kiondoni akaomba kupewa pesa inamaana kaacha kazi, la kushangaza yeye kaliwa pesa zote bila chenji sasa ninajiuliza inakuaje mkoa mmoja sera na kanuni za mifuko ziwe tofauti? Au nimeibiwa? Au nini kilicho nyuma ya pazia ninaomba mwenye uelewa tafadhali nisaidie ili nione kama nitapata haki yangu.

Asante na maandalizi mema ya pasaka.

NINAKUMBUSHA TU KAMA RAIA WA KAWAIDA CORONA IPO NA INAUA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfafanuo ni huu Kama wewe ni professional kuanzia Elimu ya diploma kupanda juu ndio wanakupa 33% idea ikiwa kwamba wewe ni msomi ndani ya miezi sita utakuwa umepata kazi nyingine na kuendelea kuchangia.Ila Ukiwa Elimu yako ni ya chini ndio wanakupa hela yote kwa kigezo kwamba huna Elimu kwa hiyo itakuwa ngumu kupata kazi nyingine. Hii ni Sheria ilipitishwa na bunge kwa hiyo wakulaumiwa wakwanza ni wabunge. Ukiangalia reality is totally opposite watu wa Elimu za chini saivi ni rahisi kupata kazi kuliko wale wa diploma na degree. Hii wamefanya Janja kwasababu wanajua watu wa degree ndio wanachukua mafao makubwa kwa hiyo mifuko itayumba na wao washaifilishi kwa miradi yao ya kifisadi na serekali kuchukua mikopo mikubwa kutoka kwenye mifuko karibia trillion 2.5 ambayo mpaka saivi haijarudishwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom