Lakini labda swali ndugu ni kuwa ni kwanini wanawake ndio mara nyingi hung'ang'ania kuolewa? Nadhani inategemea na makubariano yenu. Inawezekana kabisa kabisa kuwa mkaanzisha mahusiano yenu kwa lengo la kupatiana starehe tu pale inapohitajika. Kama ni hivyo, basi asiwepo hata mmoja kati yenu atakayezungumzia ndoa. Fanyeni tu starehe zenu na nendeni mkalale kila mmoja kwao. Tatizo la wasichana kulalamika ni kuwa wanaume huwa tunatumia mbinu nyingi kuwapata ikiwemo hiyo ya kuwaoa na kwa vile wengi wao wako-desperate for marriage, inakuwa ni rahisi kuwapata kwa njia hiyo. Hapo ndipo unaanza kulalamikiwa kuwa umemepotezea muda binti wa watu. Naamini kabisa upo uwezekano wa kuwa katika mapenzi na mkapatiana starehe bila shida ya kitu kiitwacho ndoa. Kwakifupi, siyo lazima mapenzi yaishie kwenye ndoa lakini chamsingi ni makubariano yenu ya mwanzo wa mapenzi yenu yanasemaje?