Undava King
JF-Expert Member
- Aug 11, 2017
- 3,205
- 5,333
Ni wazi kuwa imani imeanzishwa mahususi kuwa sera kuu ya kampeni inayofanywa na kikundi cha viumbe tusiowafahamu vizuri iwe kwa ubii, wajihi au maumbile zaidi ya kuamini mapokeo ya kile tulichosimuliwa nakuaminishwa kuwa ni sawa.
Leo hii kila binadamu anajikuta fahamu zake zikiangaika kujua kati ya Mungu na Shetani amchague yupi? Kila binadamu anajitengenezea mazingira ya kufanya matendo yake kumu-impress yeyote kati ya hao viumbe wawili akitegemea thawabu fulani au adhabu fulani kutoka kwao endapo tu akienda kinyume nao.
Inaeleweka Mungu kupitia mafundisho yake ni mtawala wa vyote yaani mbingu na ardhi na ana nguvu kubwa ya ushawishi mbinguni kuliko ilivyo duniani, na Shetani pia ana nguvu kubwa kuzimu kuliko duniani. Japo kwa percentage fulani nguvu ya shetani duniani ni kubwa kuliko ya Mungu, kiasi cha Mungu mwenyewe kukiri kuwa Shetani ndiye mtawala wa dunia.
Mabwana hawa wawili na ugomvi wao nakugawanyika kwa majeshi yao katika makundi ya malaika na majini au mapepo nikiri kuwa binafsi kama binadamu hayanihusu, ni sawa uzaliwe katika familia yenye wazazi waliokorofishana na kutalakiana halafu kila mtu akulazimishe kuchukua upande wake au kumuunga mkono kwa namna yeyote ile, huku wakati wakigombana wao ukuwepo wala kushirikishwa, cha zaidi kama mtoto mwenye akili timamu na maadili mema utaishia kuwachukulia wote kama wazazi.
Kila mmoja anajinadi kwa namna yake akiuza SERA zake kwa wananchi(binadamu) kupitia chombo kinachoitwa IMANI(Katiba) inayofikishwa kwa walengwa kwa njia ya DINI (Chama cha siasa) na jimbo au miliki wanayoiwania ni DUNIA na kwanini ni dunia tu? Wanadai kwa kuwa mmoja wao (Mungu) ameiumba na sisi pia ni mali yake. Pia Shetani alitudanganya tukamuasi Mungu eti nae hivi sasa ni mtawala wa dunia.
Tunaambiwa kuwa Shetani alishathibitika kuwa na makosa na mahakama ya mbinguni ikahamuru atupwe kuzimu na jeshi lake lote baada ya kushindwa vita ila bado Mungu akampa nafasi huyu bwana kuendelea kutawala nakuendesha shughuli zake duniani akishawishi(kulaghai/kusema uongo) binadamu wamuunge katika
kampeni yake na Mungu vilevile akitupa karata zake vyema kwenye mchakato huu kuakikisha nae anajitwalia wafuasi wakutosha.
SHETANI; tunaambiwa kuwa ndiye Baba wa uongo na mfalme wa dunia tunayokaa, kumaanisha kila unachokiona ikiwemo dini zote za dunia hii umwabudu yeye, tawala zote juu ya nchi za dunia hii umwinamia nakufuata muongozo wake, maarifa, uponyaji au uangamizaji, biashara na nguvu za majeshi na sayansi vyote vipo mikononi mwake.
MUNGU; tunaambiwa ndo muumba na mzazi wa kila kilichopo na kisichokuepo, kinachoonekana na kisichoonekana, kiufupi ndiyo owner wa ulimwengu usio na mipaka, sifa yake kuu ni upendo na ukamilifu,
mategemeo yake tuishi kwa haki, mema na furaha, kwa bahati mbaya njia ya kumfikia yeye anavyodai mwenyewe ni nyembamba mno kwa maana wafuasi wa kampeni zake ni wachache tu umtambua nakumfuata, kwani wengi wa wafuasi wake uchanganya madesa nakushindwa kujua yupi ni yeye kati ya yake yeye Mungu na Shetani yupi ni sauti ya Mungu wa kweli kupitia maandiko matakatifu wanayoyaamini.
Inasemekana hata hili pia ni lengo la Shetani huyu huyu kutengeneza confusion kwa kuwa ndiye gwiji katika uongo na kwa uwezo halio nao basi ulimwengu mzima hata sasa uishi nakuamini kupitia uongo wake, swali ni je, kwanini Mungu ameingia kwenye battle hii huku akijua kuwa SIASA ni uongo na katu UKWELI hauwezi kuibuka mshindi juu ya UONGO linapokuja suala la Siasa?
Pengine UONGO ushinda dhidi ya UKWELI linapokuja kwenye SIASA za dunia kwa kuwa Shetani kakita kambi huku lakini katika ulimwengu mwingine ni kinyume chake, Hivyo ningeomba hilo tuwaachie wao maana wanajua kampeni zao zinalengo gani.
Kumbuka siku zote mwanasiasa ufanya matamanio yake yaonekane kama ni matimizo ya shida za wengine. Shetani anafanya yake kwa kutushawishi kwa mali na maarifa yakidunia na Mungu pia utukonvisi kwa namna yake ya kipekee ya uaminifu,huruma na utendaji mema.
Hivyo ni juu yetu walengwa kuamua yupi tumfuate na siyo kuwa sisi ndiyo kuni zitakazotekezwa huko jehanamu kwa kushindwa kuegemea upande wowote kati yao wote.
Binafsi sioni kama ipo haja ya mwanadamu kuendelea kudeal na hizi concept au propaganda ambazo hazimuhusu zaidi ya kuzipotezea, maana cha kwanza zimekaa kufikirika na hata kama ni kweli then bado mwanadamu anaingizwa au kutumika kuprove uhalali wa tawala fulani usiomuhusu.
Pili binadamu nae ana haki na dunia yake na ukizingatia umri wake ni mfupi wa kuishi na kuendeleza kizazi chake, kwanini aendelee kuishi kwa hofu na taabu zakusurvive juu ya uso wa dunia huku akitafakari amchague nani kati ya Mungu au Shetani, hili azawadiwe kile alichoaidiwa wakati wa kampeni kuhusu uzima wa milele na raha tele.
Ebu tutafakari kwa pamoja kama binadamu, kwani tukigomesha kuwafuata hawa viumbe na masharti yao haijalishi yupi tunamchukulia yupo sahihi na yupi hayupo sahihi, natukaamua kuishi maisha yetu kama binadamu pasipo matumaini yeyote kwao.
Tuamue kufuata tamaduni na njia zetu za kuishi kama binadamu tulio huru na atutawaliwi na kiumbe yeyote au nomino dhahania ndani na nje ya sayari yetu, mwahisi tutakufa papo hapo au huo moto utatuchoma tu hata kama hatuwaungi mkono wala kuwafuata wote Mungu na Shetani.
Leo hii kila binadamu anajikuta fahamu zake zikiangaika kujua kati ya Mungu na Shetani amchague yupi? Kila binadamu anajitengenezea mazingira ya kufanya matendo yake kumu-impress yeyote kati ya hao viumbe wawili akitegemea thawabu fulani au adhabu fulani kutoka kwao endapo tu akienda kinyume nao.
Inaeleweka Mungu kupitia mafundisho yake ni mtawala wa vyote yaani mbingu na ardhi na ana nguvu kubwa ya ushawishi mbinguni kuliko ilivyo duniani, na Shetani pia ana nguvu kubwa kuzimu kuliko duniani. Japo kwa percentage fulani nguvu ya shetani duniani ni kubwa kuliko ya Mungu, kiasi cha Mungu mwenyewe kukiri kuwa Shetani ndiye mtawala wa dunia.
Mabwana hawa wawili na ugomvi wao nakugawanyika kwa majeshi yao katika makundi ya malaika na majini au mapepo nikiri kuwa binafsi kama binadamu hayanihusu, ni sawa uzaliwe katika familia yenye wazazi waliokorofishana na kutalakiana halafu kila mtu akulazimishe kuchukua upande wake au kumuunga mkono kwa namna yeyote ile, huku wakati wakigombana wao ukuwepo wala kushirikishwa, cha zaidi kama mtoto mwenye akili timamu na maadili mema utaishia kuwachukulia wote kama wazazi.
Kila mmoja anajinadi kwa namna yake akiuza SERA zake kwa wananchi(binadamu) kupitia chombo kinachoitwa IMANI(Katiba) inayofikishwa kwa walengwa kwa njia ya DINI (Chama cha siasa) na jimbo au miliki wanayoiwania ni DUNIA na kwanini ni dunia tu? Wanadai kwa kuwa mmoja wao (Mungu) ameiumba na sisi pia ni mali yake. Pia Shetani alitudanganya tukamuasi Mungu eti nae hivi sasa ni mtawala wa dunia.
Tunaambiwa kuwa Shetani alishathibitika kuwa na makosa na mahakama ya mbinguni ikahamuru atupwe kuzimu na jeshi lake lote baada ya kushindwa vita ila bado Mungu akampa nafasi huyu bwana kuendelea kutawala nakuendesha shughuli zake duniani akishawishi(kulaghai/kusema uongo) binadamu wamuunge katika
kampeni yake na Mungu vilevile akitupa karata zake vyema kwenye mchakato huu kuakikisha nae anajitwalia wafuasi wakutosha.
SHETANI; tunaambiwa kuwa ndiye Baba wa uongo na mfalme wa dunia tunayokaa, kumaanisha kila unachokiona ikiwemo dini zote za dunia hii umwabudu yeye, tawala zote juu ya nchi za dunia hii umwinamia nakufuata muongozo wake, maarifa, uponyaji au uangamizaji, biashara na nguvu za majeshi na sayansi vyote vipo mikononi mwake.
MUNGU; tunaambiwa ndo muumba na mzazi wa kila kilichopo na kisichokuepo, kinachoonekana na kisichoonekana, kiufupi ndiyo owner wa ulimwengu usio na mipaka, sifa yake kuu ni upendo na ukamilifu,
mategemeo yake tuishi kwa haki, mema na furaha, kwa bahati mbaya njia ya kumfikia yeye anavyodai mwenyewe ni nyembamba mno kwa maana wafuasi wa kampeni zake ni wachache tu umtambua nakumfuata, kwani wengi wa wafuasi wake uchanganya madesa nakushindwa kujua yupi ni yeye kati ya yake yeye Mungu na Shetani yupi ni sauti ya Mungu wa kweli kupitia maandiko matakatifu wanayoyaamini.
Inasemekana hata hili pia ni lengo la Shetani huyu huyu kutengeneza confusion kwa kuwa ndiye gwiji katika uongo na kwa uwezo halio nao basi ulimwengu mzima hata sasa uishi nakuamini kupitia uongo wake, swali ni je, kwanini Mungu ameingia kwenye battle hii huku akijua kuwa SIASA ni uongo na katu UKWELI hauwezi kuibuka mshindi juu ya UONGO linapokuja suala la Siasa?
Pengine UONGO ushinda dhidi ya UKWELI linapokuja kwenye SIASA za dunia kwa kuwa Shetani kakita kambi huku lakini katika ulimwengu mwingine ni kinyume chake, Hivyo ningeomba hilo tuwaachie wao maana wanajua kampeni zao zinalengo gani.
Kumbuka siku zote mwanasiasa ufanya matamanio yake yaonekane kama ni matimizo ya shida za wengine. Shetani anafanya yake kwa kutushawishi kwa mali na maarifa yakidunia na Mungu pia utukonvisi kwa namna yake ya kipekee ya uaminifu,huruma na utendaji mema.
Hivyo ni juu yetu walengwa kuamua yupi tumfuate na siyo kuwa sisi ndiyo kuni zitakazotekezwa huko jehanamu kwa kushindwa kuegemea upande wowote kati yao wote.
Binafsi sioni kama ipo haja ya mwanadamu kuendelea kudeal na hizi concept au propaganda ambazo hazimuhusu zaidi ya kuzipotezea, maana cha kwanza zimekaa kufikirika na hata kama ni kweli then bado mwanadamu anaingizwa au kutumika kuprove uhalali wa tawala fulani usiomuhusu.
Pili binadamu nae ana haki na dunia yake na ukizingatia umri wake ni mfupi wa kuishi na kuendeleza kizazi chake, kwanini aendelee kuishi kwa hofu na taabu zakusurvive juu ya uso wa dunia huku akitafakari amchague nani kati ya Mungu au Shetani, hili azawadiwe kile alichoaidiwa wakati wa kampeni kuhusu uzima wa milele na raha tele.
Ebu tutafakari kwa pamoja kama binadamu, kwani tukigomesha kuwafuata hawa viumbe na masharti yao haijalishi yupi tunamchukulia yupo sahihi na yupi hayupo sahihi, natukaamua kuishi maisha yetu kama binadamu pasipo matumaini yeyote kwao.
Tuamue kufuata tamaduni na njia zetu za kuishi kama binadamu tulio huru na atutawaliwi na kiumbe yeyote au nomino dhahania ndani na nje ya sayari yetu, mwahisi tutakufa papo hapo au huo moto utatuchoma tu hata kama hatuwaungi mkono wala kuwafuata wote Mungu na Shetani.