Ni kweli kuwa Chama changu Chadema hakitafilisika kwa kushiriki chaguzi ndogo zitakazotangazwa baada ya Mahakama kutengua ushindi wa Aesh - Sumbawanga Mjini, Godbless Lema - Arusha mjini na Makongoro Mahanga - Segerea kwani mtaji wake ni umma unaokifadhili wakati wa uchaguzi. Hakika kitaendelea kuwa imara siku zote Mungu ibariki Chadema nyosha mkono wako kwa watanzania wanaoteswa na mafisadi tuletee Kiongozi mwenye uchungu na rasli mali za watanzania. Mwana JF tupia mchango wako hapa. Shukrani.