Je, CCM Itatawala Milele Au?

Status
Not open for further replies.

Mkuu Kitila tuanze na elimu ya uraia huko basi manake ndiyo tatizo.I mean tusisubiri mwezi ujao uchaguzi ndiyo tuanze kujitokeza kwa wananchi na kuwaambia kuwa umasikini wao unasababishwa na CCM.Hawawezi wakakuelewa,watajua umeenda kutafuta kura(read kula)tu!Na ndipo balaa inaanza hapo kwa vile walishazoea kupewa elfu mbili ili 'watoe kula' basi lazima na wewe wakuulize vipi unazo hizo 2000?Kama huna anza kuhesabu maumivu!!
Kuna sehemu nyingine Mkuu siyo siri wananchi wamechoka na wabunge wa CCM,isipokuwa hakuna potential alternatives,inafikia wanaona heri wachague yule yule wa CCM.Kuna mkulu mmoja wa NCCR nakumbuka 2005 nilishiriki kampeni yake kwenye jimbo ninakotoka.Sisi vijana tulimsaidia sana tena bila ya kulipwa hata senti tano.Na kizuri ilikuwa yule mgombea wa CCM aliyekuwa kipenzi pale na alishinda kwenye kura za maoni,jina lake likaja kuondolewa.CCM wakaja kutuletea Mbunge yuleyule ambaye tulikuwa hatumtaki.Lakini mkulu wa NCCR pamoja na hii golden chance aligalagazwa sana na yule babu wa CCM.
Sababu kubwa hakujiandaa.Maandalizi yake yalikuwa finyu sana na alichelewa kuonyesha nia yake ya kugombea.
 

Nakuunga mkono kwa pointi yako ilichaandika ni fact tupu. Kuhusu hoja hii CCM haitatawala milele hilo halina ubishi.
 


kabla ya lawama zoe kwa serikali tujiulize tumeifanyia nini nchi ama serikali na si kuuliza serikali imefanya nini
 
is it because we are so kind and good hearted citizen kwa hiyo issue za magomvi kama Kenya hatuziwezi, hivyo hatutaweza kuwapata akina Odinga?
Kote huko tunazunguka tu; tatizo ni hili hapo juu kwetu sisi wa-TZ. Hakuna miujiza wala nini CCM hawaweezi kuachia utamu wa nchi hii kirahisi. La sivyo tutangoja mabadiliko mpaka milele yetu itakapofika.
 
kabla ya lawama zoe kwa serikali tujiulize tumeifanyia nini nchi ama serikali na si kuuliza serikali imefanya nini

- Mkuu wangu tupo pamoja hapo na ndio hasa msingi wa hoja yangu, tunafanya nini serious cha kuwahistusha watawala kwamba tunakerwa na uongozi wao mbovu?

- Na je ni kweli tunawawakilisha wananchi wengi wa Tanzania na vilio vyetu au? Na ni nini we are not going right?

Respect.


FMEs!
 


Mkuu Field Marshall ES aka W. J. Malecela, Le Mutuz.

Ni kwa sababu tuna watu vigeugeu kama wewe, waganga njaa.

Unasemaje kuhusu utapeli uliofanya wakati ule?
 
Last edited by a moderator:
Hivi unakumbuka 1995 kwanini matokeo ya uchauguzi mkuu mkoa wa Dar es Salaam yote yalifutwa?! Hiyo haikuwa shock kwa CCM?!

Hivi unajua 1995 Nyerere alipoiambia ZEC ibadilishe matokeo ya kura za urais wa ZNZ in favour of Dr. Salmin Amour, Bado unasema tu CCM haijawahi kutikishwa na upinzani?.

Hivi unakumbuka 2010 Akina Lut General Abdulahaman Shimbo walivyowatisdhiwa wananchi kwa sababu ya UOGA wa CCM. Bado unakumbuka uchakachuaji wa kura wa Dr. Kikwete 2010?!. Kama hakuogopa kwanini alichakachua matokeo ya kura. Najua ulikuwa US hebu ulizia majimbo ambayo CDM ilitangaza mshindi hali ilikuwaje? Kama sio uoga wa CCM ni nini?

Nakwambia hakuna katika uhai wa CCM/TANU ambapo imetishwa/inatishika kama sasa. Wako madarakani tu kwasababu ya TUME ya UCHAGUZI na vyombo vya dola period.
 
Katika kile kinachoonekana hakuna chama mbadala kinachoweza kuenzi amani iliyopo tz,watz wameamua sasa ccm kiwe chama chao cha maisha,Hili limetokana na vyama vya upinzani nchini kukumbwa na kashfa nzito ambazo zinatishia mustakabali wa taifa hili changa kama ufuatavyo;CHADEMA--Kuna ukabila wa kufa mtu,kama wewe si mchaga hauthaminiwi chamani kama ilivyo kwa zitto,CUF-nyumbani kw waisilamu waliowengi;TLP-ukabila pia ukipingana na mrema tu out!; NCCR-MAGEUZI-ukabila pia,pingana na mbatia uone,muulize classmate wangu kafulila atakwambia;TLP-wasukuma wa kinyantuzu wamejaa,pingana na cheyo uone cha moto! Kwa mambo haya yasiyowapendeza watz hakuna mbadala wa ccm japokuwa watz wamachoka kuongozwa na ccm,wakimbilie wapi sasa?2010 watz walikuwa hawajashtuka subirieni 2015 chadema haifurukuti tena! Ukabila na udini waanza kuitafuna tz hata kwenyeb ajira!
 
Eheeee!Dalili nyingine hii ya CHADEMA kwenda Ikulu
 
…politically..(MTANZANIA).!!! ……watch … you're …. Steps….!!!!! …are …you …moving …back… or …..Forward…..watch your steps….!!!!
 


…
KI..UHALISIA ..(MTANZANIA) .!!! ……watch … you're …. Steps….!!!!! …are …you …moving …back… or …..Forward…..watch your steps….!!!!
 

Mheshimiwa sana wa Nambari one, leo nimepata nafasi tena ya kuwa hapa jamvini. Sasa mkuu, anzisha thread nyingine basi ili tuchangie.!
 
hujui maana ya milele?wewe ngoromiko na kilaza mkubwa kweli! Wasiliana na mwalimu wako wa darasa la tatu akufundishe ndipo uingie jf tena,umewahi sana

Sidhani kama kuna shida katika kuuliza, na kama ungekuwa na jibu dhahiri usingetumia lugha hiyo! Au ungekuwa mtu wa kujiheshimu usingeandika ulichokiandika hapo juu kama una jibu la swali. As a great thinker learn

Pili, Hata kama ningekuwa ni "kilaza" je nisingekuwa na stahili ya kujuzwa?Au ni nani anayekuwa "kilaza zaidi" aliyeuliza akihitaji kupata ufahamu(common ground) au aliyekimbia swali kwa kejeli na matusi?!

Tatu, as a great thinker you should learn to know/understand the motive of every question posed to you! Dont think every question has cheap answer as the question might seem!So having said that, jibu swali au skip it kama hujui/huwezi/ au kama unaona halina relevance!
 
Ikisemwa kuwa CCM itatawala milele maana yake "CCM ni Mungu!"
 

We sijui tukuite vuvuzela la CCM au zezeta
 
kamuzu Banda pamoja na kuitawala Malawi kwa mkono wa chuma hata kufikia kujiita rais wa maisha alikuja kuondolewa kwa sanduku la kura,chama cha KANU pamoja na kuwa mojawapo wa vyama vikongwe barani Afrika kilifutika katika ramani ya siasa kupitia sanduku la kura vivyo hivyo chama cha Rais Kaunda wa Zambia,Rais Obote wa Uganda n.k. na hili linaweza kutokea kwa CCM.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…