Je, CCM itabaki salama?

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,242
34,903
Nilifanya mazungumzo na kada na kiongozi fulani (jina kapuni) wa CCM kuhusiana na mwenendo wa siasa nchini, aliniambia jambo moja tu kwamba; wanachama wa CCM wamechoshwa na namna chama chao kinavyodumazwa na mtu mmoja anayedhani chama ni Mali yake na kusahau kwamba chama ni cha watu, na kinatakiwa kiongozwe na watu.

Kada huyo mkongwe amesema hata Mwl. Nyerere hakuwahi kukifanya chama hiki kama Mali yake, amedai miaka hii watanzania wana ulimbukeni na u...levi wa madaraka. Aliongeza kwa kusema kuwa miaka yote ya CCM, sasa hivi chama kimepata kiongozi mzigo, asiyejua hata kesho ya chama chake, anayedhani yeye ni wa maana sana kuliko chama, akamalizia kwa kusema kwamba, muda utasema na siku sio nyingi watu watajipiga vifua kwa hasira na kutoa ya moyoni.
 
Huyo kanena yake ya moyoni lakini hata mimi namuunga mkono kwa hilo, kikubwa watanzania tutunze vichinjio vyetu ili visje kuwa butu 2020 vikashindwa kukata huu mti unaobunguliwa leo naimani utakuwa hauna uimara tena wa kuhimili vishindo vyetu kwa pamoja.
 
Mkuu, acha uongo wako. CCM wako pamoja sana. Ni nafuu punda (Nchi yako unayoipenda sana) afe lakini mzigo wa hao jamaa (kubaki madarakani) ufike salama. Don't be fooled, and don't try to fool others...
 
kwa tume ipi ya uchaguzi wapinzani watashinnda ? Kwa katiba na tume hii tutaendelea kusubiri embe chini ya mnazi!!!
 
Mwenyekiti wa awamu hii ana ajenda ya kuiua ccm. Huwezi kukomalia kufukuza wanachama kisa eti waligawanyika wakawa na makundi wakati wa uchaguzi. Makundi kipindi cha uchaguzi ni jambo la kawaida.

Tulitarajia mwenyekiti arudishe umoja ndani ya chama na kukipa nguvu chama ktk ngazi zote. Sasa hv huwezi kuona mwanaccm anatembea kifua mbele mahala popote. Wanadai mdudu kakaribishwa kwenye kokwa la embe ili ajihifadhi badala yake analiguguna.

Kwa mwenyekiti huyu ccm kwisha! Kwisha kabisa!
 
Nilifanya mazungumzo na kada na kiongozi fulani (jina kapuni) wa CCM kuhusiana na mwenendo wa siasa nchini, aliniambia jambo moja tu kwamba; wanachama wa CCM wamechoshwa na namna chama chao kinavyodumazwa na mtu mmoja anayedhani chama ni Mali yake na kusahau kwamba chama ni cha watu, na kinatakiwa kiongozwe na watu.

Kada huyo mkongwe amesema hata Mwl. Nyerere hakuwahi kukifanya chama hiki kama Mali yake, amedai miaka hii watanzania wana ulimbukeni na u...levi wa madaraka. Aliongeza kwa kusema kuwa miaka yote ya CCM, sasa hivi chama kimepata kiongozi mzigo, asiyejua hata kesho ya chama chake, anayedhani yeye ni wa maana sana kuliko chama, akamalizia kwa kusema kwamba, muda utasema na siku sio nyingi watu watajipiga vifua kwa hasira na kutoa ya moyoni.

Ni maoni yake na ana uhuru wa kuongea ila JPM anapiga kazi mbele kwa mbele hamna kurudi nyuma
 
Nilifanya mazungumzo na kada na kiongozi fulani (jina kapuni) wa CCM kuhusiana na mwenendo wa siasa nchini, aliniambia jambo moja tu kwamba; wanachama wa CCM wamechoshwa na namna chama chao kinavyodumazwa na mtu mmoja anayedhani chama ni Mali yake na kusahau kwamba chama ni cha watu, na kinatakiwa kiongozwe na watu.

Kada huyo mkongwe amesema hata Mwl. Nyerere hakuwahi kukifanya chama hiki kama Mali yake, amedai miaka hii watanzania wana ulimbukeni na u...levi wa madaraka. Aliongeza kwa kusema kuwa miaka yote ya CCM, sasa hivi chama kimepata kiongozi mzigo, asiyejua hata kesho ya chama chake, anayedhani yeye ni wa maana sana kuliko chama, akamalizia kwa kusema kwamba, muda utasema na siku sio nyingi watu watajipiga vifua kwa hasira na kutoa ya moyoni.
Propaganda nyepesi sana hizi.Katafute nyingine we kanjanja tu
 
Wanaccm hawajamstukia huyu mwenyekiti, anataka kuanzisha ccm yake huyu. Hamuoni anawafukuzia mbali na kuwatetemesha watu wenye mchango mkubwa kwenye chama? Ili aingize wa kwake watakaomwabudu. Kuna ccm tena hapo? Kama ipo hiyo ni ccm B
 
Ile CCM ya kubebana ni kweli imekufa kabisa hilo halina ubishi,sasa hivi tuna CCM inayotawala. Kama kodi lipa tu,kama vyeti fake utatoka tu,kama kazi hufanyi utatumbuliwa tu.Haina ushemeji haina wanja wa kijani wala manjano.
 
Back
Top Bottom