talentbrain
JF-Expert Member
- Oct 5, 2009
- 1,187
- 760
Habari za mapumziko marefu ya sikukuu za Muungano na Maulid ya kuzaliwa Mtume Mohammad (S.A.W). Tumerudi tena katika harakati zetu za maisha ya kila siku kama ilivyoada. Sitapenda kuwachosha ngoja niende kwenye hoja moja kwa moja.
Mwaka 2015 kutakuwa na uchaguzi mkuu kwa Tanzania yetu na kama tunavyofahamu kuwa chama chochote kinaweza shinda. Kushindwa kwa upinzani huwa hakuna matatizo makubwa zaidi ya kupinga na maandamano madogomadogo. Ila ninapojaribu kupiga picha jinsi CCM itavyochukulia kushindwa kwake napata wasiwasi.
CCM imeshawekeza sana katika utawala huu kiasi kwamba wanadhani wanahati milki ya kuitawala Tanzania milele. Siwaoni wakijiandaa kuweka misingi ya yeyote anayeshinda kukabidhiwa madaraka bila tatizo. Sasa nikipiga picha naona vurugu zinazoweza kupelekea machafuko kama watanzania wataamua kuwapatia madaraka upinzani.
Najaribu kukumbuka vurugu kadhaa huko Mwanza na Arusha pale ilipobainika wazi kuwa wamepokonywa ubunge tu. Walijaribu kuweka kila hila na hatimaye vurugu zikatokea. Je, urais??? Je, wamejiandaa kuwa chama cha upinzani???Kila nikitafakari na kuona jinsi wanavyofanya maovu kwa nchi hii wakitegemea kulindwa na serikali yao, ndipo naamini hawa jamaa hawataachia madaraka bila fujo.
Hivi wanaoliibia taifa mabilioni ya fedha, wanaomaliza Tembo na Faru wetu?? Je, wanaofaidika na biashara za madawa ya kulevya kwakuwa wanalindwa na utawala huu!!! Nikitazama jinsi watu wanavyotumia CCM katika kuishi isivyo halali nabaki kuamini kwamba watu hao hawatakaa waache madaraka kirahisi tu.
Je, tunasababu ya kuwaacha CCM watawale daima ili kuepusha vurugu za kuachia madaraka???
Hapana na haiwezekani kuogopa kuwaondoa wahalifu kwakuwa tu tunataka amani ya woga. Tusipowaondoa sasa watajaondolewa baadae tena wakiwa wamewekeza zaidi katika nguvu za kuleta vurugu. Wamelitendea mabaya mengi taifa na hawavumiliki tena.
Hii ni picha kubwa nimeyopiga!!!!
Mwaka 2015 kutakuwa na uchaguzi mkuu kwa Tanzania yetu na kama tunavyofahamu kuwa chama chochote kinaweza shinda. Kushindwa kwa upinzani huwa hakuna matatizo makubwa zaidi ya kupinga na maandamano madogomadogo. Ila ninapojaribu kupiga picha jinsi CCM itavyochukulia kushindwa kwake napata wasiwasi.
CCM imeshawekeza sana katika utawala huu kiasi kwamba wanadhani wanahati milki ya kuitawala Tanzania milele. Siwaoni wakijiandaa kuweka misingi ya yeyote anayeshinda kukabidhiwa madaraka bila tatizo. Sasa nikipiga picha naona vurugu zinazoweza kupelekea machafuko kama watanzania wataamua kuwapatia madaraka upinzani.
Najaribu kukumbuka vurugu kadhaa huko Mwanza na Arusha pale ilipobainika wazi kuwa wamepokonywa ubunge tu. Walijaribu kuweka kila hila na hatimaye vurugu zikatokea. Je, urais??? Je, wamejiandaa kuwa chama cha upinzani???Kila nikitafakari na kuona jinsi wanavyofanya maovu kwa nchi hii wakitegemea kulindwa na serikali yao, ndipo naamini hawa jamaa hawataachia madaraka bila fujo.
Hivi wanaoliibia taifa mabilioni ya fedha, wanaomaliza Tembo na Faru wetu?? Je, wanaofaidika na biashara za madawa ya kulevya kwakuwa wanalindwa na utawala huu!!! Nikitazama jinsi watu wanavyotumia CCM katika kuishi isivyo halali nabaki kuamini kwamba watu hao hawatakaa waache madaraka kirahisi tu.
Je, tunasababu ya kuwaacha CCM watawale daima ili kuepusha vurugu za kuachia madaraka???
Hapana na haiwezekani kuogopa kuwaondoa wahalifu kwakuwa tu tunataka amani ya woga. Tusipowaondoa sasa watajaondolewa baadae tena wakiwa wamewekeza zaidi katika nguvu za kuleta vurugu. Wamelitendea mabaya mengi taifa na hawavumiliki tena.
Hii ni picha kubwa nimeyopiga!!!!