Mi kura yangu ya mwanzo na mwisho kwa ccm ilikuwa kwa Magu tu. Kabla sikuwahi jua kama nitapigia hiko chama kura. Na kifo cha Magu kimehitimisha kupigia kura green colour.Wataelewa tu.....kura yangu ya mwisho kupiga ilikuwa kwa JPM....kilichobaki ni kuwa ndugu mtazamaji.
Inawezekana kuna mita za viwanda au mashirika makubwa zinalipa zaidi ya bilion kwa mweziKwa wastani ni 625,000 tsh kwa kila mita kwa mwezi
Hizo wiki mbili bado hazijafika au?Waziri wa Nishati January Makamba ametembelea ofisi za Tanesco na kulipongeza shirika hilo kwa kufikisha wateja 3.2 millioni ndani ya miaka 5 iliyopita.
Wanaoliwezesha kukusanya zaidi ya trillioni 2 kwa mwezi na kulifanya kuwa shirika pekee linalokusanya fedha nyingi nchini.
Makamba ametoa wiki mbili kwa shirika hilo kuacha kukata umeme la sivyo ataanza kuwafukuza kazi mameneja wote wazembe wote wanaokata umeme.
--
Waziri wa Nishati, January Makamba ametoa wiki mbili kuhakikisha hakuna tatizo la kukatika umeme nchini Tanzania.
Leo Ijumaa Septemba 17, 2021 Makamba amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) baada ya malalamiko ya wananchi kuongezeka kuhusu kukatika kwa umeme .
Makamba amesema atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake na malalamiko ya kukatika kwa umeme yakiendelea kujitokeza, wahusika wote watachukuliwa hatua.
"Ndani ya wiki mbili sitaki kusikia kukatika kwa umeme nikisikia kuna malalamiko nitachukua hatua Kwa wahusika walioshindwa kutekeleza wajibu wao," alisema Makamba.
Alisema wanahitaji Shirika hilo lijiendeshe kibiashara, kisasa ambapo mabadiliko yenye tija yataongeza ufanisi na mapato yataongezeka.
"Shirika lina wateja wa mita 3.2 milioni wanakusanya zaidi ya Sh2 tirioni na hakuna Shirika lolote hapa nchini linalotengeneza fedha hizo, hivyo wateja wanatakiwa kuongezeka ili Shirika liweze kujiendesha" amesema
Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Uzalishaji wa Umeme, Pakaya Mtimakaya amesema wameyapokea maagizo hayo na watayafanyia kazi.
Chanzo: Waziri Makamba atoa wiki mbili kumaliza tatizo la umeme
Shida ni wahusikaMimi nawalaani wote wanaohusika na kukatika umeme! Mungu awape mwisho mbaya inshaallah!
Mbona enzi za Mwendazake umeme haukuwa ukikatika? Mbona ulaya umeme haukatiki? Shida si miundombinu shida ni wahusika wa ofisi ya nishati na madili yao ya kuuza Solar na Majenereta!
Haya majitu yenye madaraka yanatutesa sana duniani hatuna raha , siku yakifa yatapokewa kuzimu na mashetani, mazombi, mazimwi, vibwengo, ibilisi na mapepo!!
Alimaanisha miaka 20.Nahisi miaka 2 ilikuwa
Ova
Aibu iseee hii nchi uwongo tumefanya uwe sehemu ya maisha..Tanesco kweli ni tamu. Wanakusanya zaidi ya trillion 2 kwa mwezi sawa na zaidi ya shilingi trillion 24 kwa mwaka. Hii ni karibu sawa na bajeti ya mwaka ya nchi ya Tanzania. Yaani tanesco ndiyo Tanzania. Wanavyoitumia pesa yote hiyo wanajua wenyewe. Hata gawio la serikali hawalipi. Mitambo yao ya kuzalisha umeme wananunuliwa na serikali. Kwa mfano huo mradi wa NHPP ambao gharama yake ni trillion 6 tu serikali ilibidi kukopa nje ili kuugharimia.
Hizo wiki mbili za Makamba zimegeuka kuwa miaka. Na bei ya umeme wanapanga kuipandisha mara dufu, yaani wawe wanakusanya trillion 48 kwa mwaka ndipo waache hiyo katakata ya umeme. Yaani hadi waizidi bajeti ya serikali. Bunge la tanesco ambalo ndiyo hupitisha bajeti ni hiyo bodi yao iliyosheheni wafanyabiashara. Makamba ndiyo mkuu wa nchi hiyo inayoitwa tanesco. Wananchi wake wanampendaaa hadi raha.
Kumbe yamuda mrefu ningeshangaaWaziri wa Nishati January Makamba ametembelea ofisi za Tanesco na kulipongeza shirika hilo kwa kufikisha wateja 3.2 millioni ndani ya miaka 5 iliyopita.
Wanaoliwezesha kukusanya zaidi ya trillioni 2 kwa mwezi na kulifanya kuwa shirika pekee linalokusanya fedha nyingi nchini.
Makamba ametoa wiki mbili kwa shirika hilo kuacha kukata umeme la sivyo ataanza kuwafukuza kazi mameneja wote wazembe wote wanaokata umeme.
--
Waziri wa Nishati, January Makamba ametoa wiki mbili kuhakikisha hakuna tatizo la kukatika umeme nchini Tanzania.
Leo Ijumaa Septemba 17, 2021 Makamba amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) baada ya malalamiko ya wananchi kuongezeka kuhusu kukatika kwa umeme .
Makamba amesema atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake na malalamiko ya kukatika kwa umeme yakiendelea kujitokeza, wahusika wote watachukuliwa hatua.
"Ndani ya wiki mbili sitaki kusikia kukatika kwa umeme nikisikia kuna malalamiko nitachukua hatua Kwa wahusika walioshindwa kutekeleza wajibu wao," alisema Makamba.
Alisema wanahitaji Shirika hilo lijiendeshe kibiashara, kisasa ambapo mabadiliko yenye tija yataongeza ufanisi na mapato yataongezeka.
"Shirika lina wateja wa mita 3.2 milioni wanakusanya zaidi ya Sh2 tirioni na hakuna Shirika lolote hapa nchini linalotengeneza fedha hizo, hivyo wateja wanatakiwa kuongezeka ili Shirika liweze kujiendesha" amesema
Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Uzalishaji wa Umeme, Pakaya Mtimakaya amesema wameyapokea maagizo hayo na watayafanyia kazi.
Chanzo: Waziri Makamba atoa wiki mbili kumaliza tatizo la umeme