January Makamba ni Obama ajaye?

BICHWA KOMWE -

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2022
Posts
7,996
Reaction score
20,079
Sijui mmegundua? Huyu jamaa ana mikogo na miondoko kama ya Barrack Obama.

Ukiachana na ile "nadharia" kwamba yeye mwenyewe mara zote hudhani ana sifa za kuwa Rais, nimebaini pia hata mwonekano wake ni wa ki-obama obama.

Zile tambo zake za kuongea kwa nukta na madoido pamoja na aina ya uvaaji wake, kwa hakika huyu ndiye.

Siku hizi naona anakunja mashati kama Obama.

Nimepekua mafaili yake, inasemekana alipokuwa High School (Galanos) alipata dosari ya kitaaluma kutokana na uvujifu wa mitihani na udanganyifu.

Kwa hilo, nafikiri hiyo ndiyo tofauti pekee aliyonayo dhidi ya Obama. —Obama ni msomi, wakati January ndio vile tena tia maji tia maji.

Mengine yote nafikiri wanafanana sana na Obama. Hasa ule ukunjaji wa mashati unanikoga sana.

Tumpe huyu. Ni Obama wetu wa kitanzania.
View attachment 2323174
 
Kwenye uzungumzaji ni kweli, wote ni wazungumzaji wazuri ila kwenye upande wa kutenda sijui kama wanashabihiana

Labda kama atakuwa na record nzuri ya kufanya vitu kwa ajili ya public welfare zaidi..
 
Kwa hii nchi ya Marehemu hilo linawezekana, Tanzania hata Mwijaku anaweza ongoza nchi kwa.kifupi hata wewe mlera post unaweza ongoza hii nchi.
 
Kwenye kuzungumza sina uhakika.

Lakini kwenye ukunjaji wa mashati hapo swadakta. Kopi right.

Nilishawahi kuhudhuria mkutano flani na alipoanza kuzungumza Tu, kila mtu alimsifia..

Ila ameshawahi fanya kazi za uandishi na mawasiliano kwa hiyo si kitu cha kustaajabisha sana
 
Acha kumfananisha Obama na Mambo ya ajabu.
 
Jamaa ana nyota inayong'aa sana; lipo kundi limejipanga kwa hali na mali kumchafua lakini ni suala la muda tu kabla hajawa-outshine kimasihara tu......hawatoamini!!
 
Hamsogeli hata Ruto wa hapo Kibera, Obama wapi na wapi? Ndiyo za mchana
 
Namkubali Sana ila kama tuu CCM wata ignore ule utaratibu wao usio rasmi wa kufuata mbadilishano wa dini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…