Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 980
- 3,646
Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu, Jaji Joseph Warioba akitoa maoni katika kongamano la kitaifa kuhusu uchaguzi mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) amesema
Polisi kazi yao ni kulinda usalama wa raia na mali zao, na wanafanya kazi hiyo maana hakuna lawama kubwa katika kufanya kazi zao.
Matatizo yanakuja Polisi wanapoanza kushughulikia siasa. Huko nyuma tulipokuwa tunapata cases hizo za public interest, mahakama ilikuwa inashirikiana na polisi kupanga watu, na wakija wengi wanazungumza nao kwamba sio kuwa tunawazuia msiende kusikiliza kesi, sababu ni kwamba hakuna nafasi ya kutosha. Kwa hiyo wataruhusu watu kiasi fulani wataingia ndani, wengine labda watakaa mahali fulani.
Pia soma > Pre GE2025 - Jaji Warioba: Jeshi la Polisi limeingizwa kwenye Siasa, linatoa matamko ya Kisiasa, liachwe lifanye kazi yake
Hapa sasa inaonekana ni mapambano, siyo kushauriana ni kwenye geti imezuiwa wasiingie, wala kule hujui kama kuna nafasi ama hapana, ni kuzuia tu.
Na walivyokuja, polisi hawakuja kwa njia ya amani maana unakuja unashughulika na hili. Ukiona yaliyotokea Aprili 24 na baadaye 28, utaona walikuja kwa mtindo wa vita, umejiandaa una silaha, una magari na askari wengi sana, unambwa, una farasi, yaani atmosphire ile ni kama uko kwenye uwanja wa vita, na pale ndipo tulifanya kosa la kwanza.
Ingewezekana kabisa kusema hapa kweli hakuna nafasi ya kutosha, watakaoweza kuingia ni hawa hapa, na wengine ama wafanye utaratibu mwingine.
Na teknoloji imeendelea, wangeweza hata kuwa na screen mahali fulani wakasikiliza, lakini badala yake ilionekana kama mapambano.
Kwa hiyo, kwa upande wa Serikali wanaona ni kulinda amani, kwa upande wanaona hii ni kuonea na kila mmoja anashikilia upande wake.
Nadhani hili la kesi hiyo kuna misingi, maaana wakati wote uamuzi huwa ni wa mahakama, lakini hapa inaonekana uamuzi ulikuwa wa Polisi, turudi kwenye taratibu za kawaida
Polisi kazi yao ni kulinda usalama wa raia na mali zao, na wanafanya kazi hiyo maana hakuna lawama kubwa katika kufanya kazi zao.
Matatizo yanakuja Polisi wanapoanza kushughulikia siasa. Huko nyuma tulipokuwa tunapata cases hizo za public interest, mahakama ilikuwa inashirikiana na polisi kupanga watu, na wakija wengi wanazungumza nao kwamba sio kuwa tunawazuia msiende kusikiliza kesi, sababu ni kwamba hakuna nafasi ya kutosha. Kwa hiyo wataruhusu watu kiasi fulani wataingia ndani, wengine labda watakaa mahali fulani.
Pia soma > Pre GE2025 - Jaji Warioba: Jeshi la Polisi limeingizwa kwenye Siasa, linatoa matamko ya Kisiasa, liachwe lifanye kazi yake
Hapa sasa inaonekana ni mapambano, siyo kushauriana ni kwenye geti imezuiwa wasiingie, wala kule hujui kama kuna nafasi ama hapana, ni kuzuia tu.
Na walivyokuja, polisi hawakuja kwa njia ya amani maana unakuja unashughulika na hili. Ukiona yaliyotokea Aprili 24 na baadaye 28, utaona walikuja kwa mtindo wa vita, umejiandaa una silaha, una magari na askari wengi sana, unambwa, una farasi, yaani atmosphire ile ni kama uko kwenye uwanja wa vita, na pale ndipo tulifanya kosa la kwanza.
Ingewezekana kabisa kusema hapa kweli hakuna nafasi ya kutosha, watakaoweza kuingia ni hawa hapa, na wengine ama wafanye utaratibu mwingine.
Na teknoloji imeendelea, wangeweza hata kuwa na screen mahali fulani wakasikiliza, lakini badala yake ilionekana kama mapambano.
Kwa hiyo, kwa upande wa Serikali wanaona ni kulinda amani, kwa upande wanaona hii ni kuonea na kila mmoja anashikilia upande wake.
Nadhani hili la kesi hiyo kuna misingi, maaana wakati wote uamuzi huwa ni wa mahakama, lakini hapa inaonekana uamuzi ulikuwa wa Polisi, turudi kwenye taratibu za kawaida