PreGE2025 Jaji Mkuu Mstaafu Mutunga, Martha Karua na wenzake 4 waiburuza Serikali ya Tanzania Mahakama ya Afrika Mashariki. Wataka fidia na msamaha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
2,439
Reaction score
6,692
Wakuu,

Yaani hakuna kupumzika. Sasa hivi Serikali haipati tu upinzani kutoka ndani lakini hadi nje.

Haya sasa, Martha Karua kaamua kuipeleka Serikali yenu Mahakamani.

================================

Martha Karua na wanaharakati wengine wanne wameiburuza na kuishtaki Serikali ya Tanzania kwenye Mahakama ya Afrika Mashariki kwa madai ya kukamatwa kinyume cha sheria, kukataliwa kuingia Tanzania na kurudishwa Kenya

Pia wanaharakati hao wametaka kuombwa msamaha na Serikali ya Tanzania pamoja na kulipwa fidia kwa walichofanyiwa


Aliyekuwa Jaji Mkuu wa Kenya, Dkt. Willy Mutunga, Wakili Mwandamizi Martha Karua, pamoja na watu wengine wanne, wamefungua kesi katika Mahakama ya Haki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACJ) dhidi ya Serikali ya Tanzania, wakidai kuwekwa kizuizini kinyume cha sheria, kunyimwa kuingia nchini, na kufukuzwa.

Kundi hilo, ambalo pia linajumuisha wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu wanne: Gloria Kimani, Lynn Ngugi, Hussein Khalid, na Hanifa Adan, wamedai kuwa haki zao kama raia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zilikiukwa waziwazi walipozuiwa kuingia Tanzania kushuhudia kesi ya uhaini dhidi ya kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu.

Waombaji wanasema kuwa kati ya Mei 18 hadi 19, 2025, walikamatwa bila maelezo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, pasipoti zao zikachukuliwa, na baadaye wakafukuzwa kurejea Kenya.

Wameeleza kuwa walikuwa nchini Tanzania kama sehemu ya ujumbe wa waangalizi wa kimataifa, kwa lengo la kushiriki na kufuatilia mwenendo wa kesi ya Lissu iliyopangwa kuanza Mei 19.

Katika ombi lao, kundi hilo limeishtaki Tanzania kwa kuvunja vifungu mbalimbali vya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hasa vinavyohusiana na utawala wa sheria, uwazi, uongozi bora, na haki ya uhuru wa kusafiri ndani ya nchi wanachama.

Kesi hiyo pia inadai kuwa kuondolewa kwao kulidhoofisha ushiriki wa kiraia na kuvunja dhana ya haki ya wazi, kwa kuwanyima fursa ya kushuhudia mchakato wa kisheria wa umuhimu wa kikanda.

Kesi hiyo imewasilishwa kwa ushirikiano na mashirika mawili ya kutetea maslahi ya umma: Jumuiya ya Wanasheria Afrika Mashariki (EALS) na Umoja wa Wanasheria wa Afrika (PALU), ikieleza kuwa hatua za Tanzania hazikuzingatia masharti ya Kifungu cha 6(d), 7(2), 76, 104, na 8(1)(c) of the EAC Treaty and the EAC Common Market Protocol of 2009.

Waombaji pia wanataka maelezo ya “kukataliwa kuingia” yafutwe kutoka kwenye pasipoti zao, na mahakama itoe amri ya kuizuia Tanzania kuendelea kukiuka haki ya usafiri huru kwa raia wa Afrika Mashariki.

Kesi hiyo inatarajiwa kuhamishiwa makao makuu ya EAC mjini Arusha, ambako tarehe ya kusikilizwa itapangwa na mahakama katika wiki zijazo.

Uamuzi wa kesi hii unaweza kuweka msingi muhimu wa utekelezaji wa haki za kikanda ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Source: Citizen TV Kenya
 
Huko.lazima Sa100 apigwe za uso maana huyu hapa hayupo huko
 
Ilikulikana mapema. Wasingeweza kutuacha hivi hivi.
 
Hiyo inaweza kuishia kuwa “for the record”. Serikali ya CCM haina utamaduni wa kuheshimu court rulings ambazo haijazipenda!
 
Sikujua kama EA Court ni mahakama mbuzi, kwa hiyo majaji wanaolipwa dollars kule wanapewa bure bila kazi
Nani anajali hata wangelipwa dinar au pound.

Kwani wabunge wa East Afrika hawalipwi? Kwani wanatusaidia nini?

Nchi yetu haihali unalipwa nini na nani inataka kile kinachoifaidisha yenyewe.

Kama hukumu hazitekelezwi hiyo siyo mahakama.

Nakumbuka Magufuli alijitoa huko sijui tulirudi lini.
 
Watuchokoze wao halafu tuwalipe na fidia watasubiiri sana

Hawatujui watanzania hao wakenya waende kokote shenzi type
 
Usipotekeleza hukumu unalazimishwa hata kwa kukamata Mali zako
 
Hiyo ni mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki.
Tanzania ni mwanachama wa jumuiya ya afrika mashariki.
Naomba niambie tulijitoa.lini kwenye jumuiya ya affrika.mashariki na kwenye hiyo mahakama
Magufuli alitangaza kujitoa kwenye mahakama hiyo tafuta utajua ni lini.

Mahakama siyo jumuiya, na kujiunga kwenye jumuiya siyo kwamba imejiunga kwenye kila kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…