Hao wote ni waongo pasua kichwa tu, hiyo gari ninayo mwaka wa 4 sasa, tangu niagize toka Japan ingawa ni ussed, lakini tangu niichuue haijawahi kuniletea tatizo lolote zaidi ya kubadilisha engine valve moja ilikuwa imepinda. Mpaka leo nasafiria mikoni, mimi nipo Arusha, nilishaenda nayo Nairobi, Dar, Tanga na Mbeya. Safari zote hizo haijawahi kuniharibikia hata siku moja tena ni gari inayotulia sana barabarani,sana sana utabadilisha tairi tu kwa pancha, kitu ambacho ni cha kawaida katika gari. Cha msingi tunza gari yako,kama alivyosema Damin Marijan epuka kuchanganya vituo vya mafuta, jitahidi utumie kituo kimoja tu. Nakutakia kila la kheri.