ITV inaihujumu ACT Wazalendo?

mkalamo

JF-Expert Member
Sep 7, 2013
340
359
Wadau naomba tujadili pasipo jazba, katika siku za hivi karibuni nimekuwa nikifuatilia taarifa mbali mbali zinazorushwa na ITV ikikihusu Chama cha ACT wazalendo. Nilichobaini ni ama kwa makusudi au kwa kutokujua chombo hicho cha habari kimekuwa kikikihujumu Chama hicho, na nitatolea mifano michache juu ya hayo

Mwaka huu wakati chama hicho kilipokuwa kinafanya sherehe yao ya maadhimisho ya miaka miwili kule Zanzibar licha ya ACT kutoa msimamo wao wa kutoutambua uchaguzi wa marudio wa machi 20 mwaka huu, chombo hicho kilimtafuta mmoja wa viongozi na kuongea nae kuwa wanaitambua serikali hiyo

Pia katika siku za hivi karibuni Chombo hicho kimekuwa kikichukua taarifa za ACT na kuzichanganya na taarifa za vyama vingine kwa ajili ya kutafuta uhalali wa kuificha taarifa hiyo. Na jana katika hali ya kushangaza nimeshuhudia katika kituo hicho wakimtambulisha mtu anayeitwa Sabini kuwa ndiye katibu wa Itikadi na mawasiliano wa ACT Taifa badala ya Ado Shaibu na kisha mtu huyo akatoa tamko lisiloeleweka

Katika hili Chombo hicho ni wazi kina mkakati wa makusudi wa kuwahujumu wenzao kwa maslahi wanayoyajua
 
Vipi na TBC wanarusha pia habari za ITV?

ITV ndo channel inayobalance vipindi sijaona tv station inayoizidi ITV. nakusihi fuatilia na Tv station nyingne uone kama na wao wanarusha habari ya ACT kama ilivyo ITV
 
Mbona hiyo siyo habari na ipo wazi. Tungeshangaa kama ITV kama chombo rasmi cha CHADEMA kwa kuwa mmiliki wake ni mwanachama wa kificho kingeitangaza vizuri ACT
 
....kwani ACT wana habari gani ya kuuza gazeti mjomba?, au kuwekwa kwenye taarifa ya habari?

binafsi nimewasikia ACT juzi tu wakitoa tamko bosi wao alivyofukuzwa bungeni!, hicho chama chenu bado kichanga msijidanganye mtapasuka msamba!
 
Wadau naomba tujadili pasipo jazba, katika siku za hivi karibuni nimekuwa nikifuatilia taarifa mbali mbali zinazorushwa na ITV ikikihusu Chama cha ACT wazalendo

Nilichobaini ni ama kwa makusudi au kwa kutokujua chombo hicho cha habari kimekuwa kikikihujumu Chama hicho, na nitatolea mifano michache juu ya hayo

Mwaka huu wakati chama hicho kilipokuwa kinafanya sherehe yao ya maadhimisho ya miaka miwili kule Zanzibar licha ya ACT kutoa msimamo wao wa kutoutambua uchaguzi wa marudio wa machi 20 mwaka huu, chombo hicho kilimtafuta mmoja wa viongozi na kuongea nae kuwa wanaitambua serikali hiyo

Pia katika siku za hivi karibuni Chombo hicho kimekuwa kikichukua taarifa za ACT na kuzichanganya na taarifa za vyama vingine kwa ajili ya kutafuta uhalali wa kuificha taarifa hiyo

Na jana katika hali ya kushangaza nimeshuhudia katika kituo hicho wakimtambulisha mtu anayeitwa Sabini kuwa ndiye katibu wa Itikadi na mawasiliano wa ACT Taifa badala ya Ado Shaibu na kisha mtu huyo akatoa tamko lisilo eleweka

KATIKA HIli Chombo hicho ni wazi kina mkakati wa makusudi wa kuwahujumu wenzao kwa maslahi wanayoyajua
Kafanyeni siasa za majukwaani mjenge chama
 
Sawa kabisa km alivyosema mjumbe mmoja hapo juu kwamba ACT bado ni kichanga sana. Hakijafikia level ya habari zake kuuzia gazeti au kuvutia watazamaji! Hivyo mara nyingi vyombo vya habari havitazipa uzito! Vyombo vya habari vinafanya biashara sio kuuza sura!
 
....kwani ACT wana habari gani ya kuuza gazeti mjomba?, au kuwekwa kwenye taarifa ya habari?

binafsi nimewasikia ACT juzi tu wakitoa tamko bosi wao alivyofukuzwa bungeni!, hicho chama chenu bado kichanga msijidanganye mtapasuka msamba!
Ivi ACT ina Wabunge wangapi??
 
ACT mnagubu utafikiri vibibi vya kizaramo, Ivi mnafkir mtapendwa kwasababu ya kulalamika? Embu peleken upuuz wenu kigoma, au kama vp Burund si kuna vituo ving vya Tv tumieni vile coz mpo karbu nao sana makao makuu yenu kigoma
 
Chama chenyewe hakieleweki, sasa kuna ulazima gani kwa chombo cha habari kueleweka na wakati wahusika wenyewe hawajielewi?

Mfano, kipindi cha uchaguzi Zanzibar ACT walitoa tamko la kutoshiriki Marudio lakini cha ajabu uchaguzi walishiriki na wakapeleka mpaka na Mawakala, sasa vyombo vya habari hapo vitaandikaje sasa?

Let's be realistic
 
Baadhi ya wachangiaji mmeshaambiwa na mtoa post msiwe na mihemko katika kuchangia badala yake angalieni kama kuna hoja ndiyo mjibu

mtoa posti amesema kuna baadhi ya upotoshaji unafanywa na chombo hicho na akatolea mfano wa mtu asiyekuwa kiongozi wa Chama hicho kupewa cheo cha katibu wa uenezi na mawasiliano katika taarifa yao ilihali wanajua cheo hicho anacho nani

vivile mtoa Post ameuliza sababu ya baadhi ya habari za ACT zinazojitegemea kutafutiwa uhalali wa kuchanganya na habari za vyama vingine hata kama havitkufanya mkutano siku hiyo ina lenga nini?
 
Back
Top Bottom