Nimejaribu kuichunguza kiufundi ili kujiridhisha kuwa tatizo halipo upande wa mteja. Kwangu mimi, ITV signal status inaonyesha kuwa Signal Strength ni 64% na Signal Quality ni 69%. Hivi ni viwango vya kuridhisha kabisa na tafsiri yake ni kwamba wateja tunapokea signal kwa kiwango cha juu karibu sawa na iliyosafirishwa. Sasa kama iliyosafirishwa inakuja na pixels (mabox box yanayokwama), basi ina maana aliyesafirisha signal ndio amesafirisha signal mbaya. Kwa mfumo wa sasa wa digital kwa watumiaji wa antenna, Star Times ndio wanaosafirisha signal ya contents za ITV, kwa hiyo wameamua kutuletea good but corrupted signal