Israel yashambulia tena Syria stoo ya silaha yateketezwa

Duduwasha

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
5,703
3,653
Kwa Mara nyingine tena vyombo vya habari vya kiarabu vimesema milipuko mikubwa mitano ilitikisa jiji zima na miale mikubwa ya moto kuonekana kila kona ya mji mashuhuda wamasema waliona moto na vishindo vya sauti ya milipuko njia ya luelekea uwanja Wa ndege Wa kimataifa Wa Damascus majira ya alfajiri. 3:25AM Thursday 27th April 2017.

Report zinasema ghara la kuhifadhia silaha na tank la mafuta yameharibiwa kabisa hilo ghala yawezekana kulikuwemo na vitu vya kulipuka vinavyodhaniwa ni silaha nzito. Milipuko imetokea baada ya lisaa limoja kipita ndege kutoka Iran ilipotua. Na kawaida huleta silaha kwa ajili ya kundi la lebanon Hezbollah.

Israel imesema haiwezi kusema chochote kuhusu iwe kukubali au kukanusha kuhusika ila imeendelea kusisitiza kuwa msimamo wao upo vile vile kuhusu usalama wao. Na hawatoacha kuzuia kuona Hezbollah wakisaidiwa silaha.

Raisi Putin aliomba chonde chonde nchi jirani ziache uchokozi kwani zitazidi kuchochea hali isitulie nchini Syria haijajulikana Kama Israel aliwataarifu Russia kabla ya kushambulia ila Israel na Russia wanamikataba yao kutokuingiliana angani na kufahamishana kwa kila jambo.

Syria imesisitiza kuwa mashambulizi hayo ni ya ndege kutoka Israel.
 
Israel anawasaidia ISIS wake,maana wao ndio wanawafund na USA so baada ya kuzidiwa na Urusi,wameingia kwa gia ya Hezbollah ila lengo kuwapiga tafu vibaraka wao!!
Acheni kila kitu kulaumu Israel... Huyo Syria anayataka mwenyewe kwa kusafirisha silaha kwenda kwa Hezbollah unategemea Israel wakae tu wkt wanajua wapo hatarini
 
Umeona wana wa Israel wanavyokinukisha mbona huyu Vladimir Putin awatetei, ivi ndivyo itakavyowakuta North Korea
 
Angalau kodogo leo kumejadiliwa vitu japo vichache ila nafuu kuliko mtu flan kila uzi lazima aweke mambo ya kiimani

huwa inakera mno hyooo.
 
Israel anawasaidia ISIS wake,maana wao ndio wanawafund na USA so baada ya kuzidiwa na Urusi,wameingia kwa gia ya Hezbollah ila lengo kuwapiga tafu vibaraka wao!!
Mkuu silaha za Hezbollah's zilianza kuteketezwa kitambo kabla ya vita vya Syria tatizo Hezbollah hawatambui kuwa mawasiliano yao na Iran hapo live maspy Wa israel wananasa kila kitu huko Sudan kiwanda kililipuliwa na ndege za Israel zilizisafiri chini kwa chini zikapiga zikarejea salama waliduwaa nchi zote ndege zilizipita. Ndio Iran akaanza kuitumia Syria. Pamoja na vitisho vyote na kumtumia Russia Kama kinga wanatunguliwa tu.
 
Mkuu kwani kujibu tu kilichoulizwa inakuwa tabu?
Maana naona kama ulichokiandika hapa aidha umeandikiwa au umetokosa (out of reference point).
Nakushauri " wacha porojo, weka majibu".


Mkuu hili sio jukwaa la watoto... Juma mupe toto ball achezee..
Matamshi ya kihindi ukipewa dushe uchezee usishangae...
 
Back
Top Bottom