Ishi leo kwanza.

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,745
Reaction score
4,941
WAKATI MWINGINE JARIBU KUACHA KUWEKEZA KWENYE MALENGO BADALA YAKE WEKEZA KWENYE MCHAKATO.
"Sometimes we must stop being goal oriented and shift to process oriented"
........................................................................................................................ ..
Kuendelea kujiwekea malengo na kujisahaulisha kuwekeza kwenye mchakato ni kujilisha upepo. Kumbuka tunaishi leo, jiulize leo unafanya nini hata kutamani kesho?. Malengo ni kesho na kwa hakika ni matokeo ya unachofanya leo ...."Unafanya nini leo?."

Kuna mambo ya ajabu sana katika ulimwengu huu, embu tafakari juu ya hili. Lengo la mwisho la maisha yetu ni kifo, je tunapokimbilia malengo tunakimbilia wapi?.Mchakto ndiyo maisha yako ya leo haswa na ndiyo unaweza kusukuma matokeo "consequences".

Haiwezekani kuishi Duniani kabla ya kuzaliwa, kuzaliwa ni mchakato unaotangulia kuishi. Lengo kinapaswa kutokana na mchakato. Ishi leo kwanza kabla ya kesho. Tatizo letu tunatamani sana kuishi kesho kabla ya kuishi leo.
...........................................................................................................................
 
Ni kweli..we should trust the process..hii kubwa sana,unajua kwanini? Kuna mtu muda huu kalala "anasikilizia" mchongo sehemu..anasema no hurry in africa..anaamini mambo yatakaa.
 
Kwahiyo nianze kuishi leo, then kesho itajisumbukia sindio...??🙄
 
No, usumbufu wa leo ndiyo msingi wa kesho. SUMBUKA SANA LEO.
Njoo Mang'ombe leo tuishi Mkuu kama upo Mbogwe
Mang'ombe haieleweki. Nimepita huko jumamosi Hadi lulyu nilifika. Labda mwakitolyo natafakari kuweka mwalo.
 
Umeandika mambo magumu.

But huwezi kaa tu bila kuwaza kesho yako.

Leo niko shop hapa ila nawaza kesho kuwa na shop la dawa za binadamu.

Lazima tuishughulishe sana akili.
 
Yote tisa, kumi tusisahau kufanya mapenzi.
 
Umeandika mambo magumu.

But huwezi kaa tu bila kuwaza kesho yako.

Leo niko shop hapa ila nawaza kesho kuwa na shop la dawa za binadamu.

Lazima tuishughulishe sana akili.
Sijamaanisha tuache kuwaza, la hasha!.. ila tuutendee haki mchakato wa mawazo yetu leo.
 

HAHA Nakweli​

Mathayo 6:34​

Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Maovu ya siku yanaitosha siku hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…