IPTL/PAP: Hatuna kesi na TANESCO

Very right! IPTL hawana kesi na TANESCO popote pale duniani, uamuzi wa kutoa fedha za escrow ulipofikiwa ulizingatia ukweli huu. Hakukuwa na dispute yoyote mahakama yoyote duniani na mgogoro wa capacity charge ulikuwa umemalizwa kwa capacity charge kushushwa kutoka $ 4.2 milioni mpaka $ 2.6 milioni. Hivyo basi fedha za escrow ni mali ya IPTL.
 
Mwaka 2006 serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupitia Wizara ya Nishati na Madini, shirika la IPTL na Benki Kuu ya Tanzania (wakala) kutokana na Mkataba wa kuzalisha na kuuza umeme kutoka IPTL kwenda TANESCO kulianzishwa akaunti ya ESCROW.
MAtakwa ya makubaliano ya kuanzishwa na kutekelezwa kwa mradi wa kujenga, kuendesha na kuzalisha umeme wa kuuza kati ya kampuni binafsi ya IPTL na TANESCO ni kwa serikali kufungua letters of credit au kufungua akaunti ya ESCROW.

Akaunti hiyo siyo fedha za serikali bali ni fedha ambazo ziliwekwa kutokana na matakwa ya mkataba wa kuuza umeme kwa TANESCO kutoka kampuni binafsi. Katika mkataba wa kufungua akaunti ya ESCROW kuna kifungu kinasomeka, “required amount means the amount in Tshs. That the government of Tanzania shall deposit from time to time in the ESCROW account which equals not less than two months estimated tariff payments under the PPA, provided that such amount shall be adjusted annually by IPTL and TANESCO pursuant in the PPA in the article 11 hereof, and government of Tanzania will be entitled will be entitled to review independently, the calculation of the required amount pursuant to this agreement”.
Tafsiri yake kwa Kiswahili ni kwamba “kiasi kinachopaswa kuingizwa na serikali katika akaunti ya ESCROW ni kile ambacho kinalingana na madai ya malipo sawa na miezi miwili ya gharama ya kuuza umeme ambazo IPTL inadai TANESCO, IPTL na TANESCO watafanya marejeo kuhusiana na kiasi cha gharama za umeme kila mwaka. Hayo ni kwa mujibu wa makubaliano ya kuuza na kununua umeme kwa mujibu wa makubaliano ya mkataba wa mauzo ya umeme (Power Purchasing Agreement) au kwa kifupi PPA na kama ilivyobainishwa kwenye kifungu cha 11. Serikali itakuwa huru kufanya tathmimini yake kuhusu gharama halisi za uzalishaji na uuzaji wa umeme kwa mujibu wa mkataba wa PPA.
Wakati akaunti ya ESCROW inafunguliwa serikali na IPTL walikuwa katika mahakama ya usuluhishi ya ICSD ambapo suala la gharama za capacity charge lilikuwa linagombewa. Hivyo serikali ya Tanzania ilikataa madai ya kulipa dola za kimarekani milioni 3.6 kwa ajili ya capacity charge.
Katika Mahakama ya Usuluhishi fedha ambazo zilikubaliwa ni dola za Kimarekani millioni 120 na hivyo gharama za capacity charge kuteremshwa kufikia dola za Kimarekani milioni 2.6. Hivyo mgogoro kati ya serikali na IPTL ukawa umekwisha.
Kumalizika kwa mgogoro huo kunamaliza utata wote wa serikali kuwa na madai katika akaunti ya ESCROW, isipokuwa yale yanayohusu kodi ambazo TRA itakuwa inadai wakati akaunti ya ESCROW itakuwa imefunguliwa kwa wahusika kwa makubaliano ya kutoa fedha au pale fedha kutoka akaunti ya ESCROW zitakuwa zimetolewa na kuwekezwa katika vitega uchumi kama inavyoelezwa katika kifungu cha 3 kinachohusu uwekezaji wa fedha katika akaunti ya ESCROW.
Inaelezwa kwamba shria za Tanzania ndiyo zitatumika katika uthibiti wa fedha za akaunti ya ESCROW. Mtazamo huu wa sheria unazingatia matakwa ya usuluhishi ya Mahakama ya kimataifa ya usuluhishi ICSID ambayo inatamka wazi kwamba wahusika wanakubali kwamba IPTL inathibitiwa na Nationals na hivyo itachukuliwa kuwa shirika la Tanzania kwa madhumuni na matakwa ya makubaliano ya mkataba wa kimataifa. Na wakala wa akaunti ya ESCROW anathibitiwa na serikali ya Tanzania na hivyo anatambuliwa kama taasisi ya kitanzania kwa madhumuni ya mkataba wa ICSID.
Hivyo alipopatikana mnunuzi PAP ambaye alikubaliana kununua hisa za VIP Engineering and Marketing shirika hilo ambalo linamiliki aslimia 30% ya hisa zote, ilikuwa sahihi aondoe kesi ya kutaka IPTL ifunge hughuli zake na wabia wagawane mali. Mahakama Kuu haikukosea kukubaliana na VIP Engineering and Marketing kuondoa kesi na hivyo kufungua milango kwa mmiliki wa hisa zote 100% kuchukua fedha zilizokuwa Benki Kuu kwenye akaunti ya ESCROW.​
 
Singa singa ni mwivi tangu kitambo
 

Attachments

  • 1416386778296.jpg
    52.3 KB · Views: 95
Singa singa ni mwivi tangu kitambo

Alikuibia Mkeo nini? Acha udaku wewe, umetumwa kututoa kwenye topic? IPTL/PAP hawana kesi na TANESCO popote pale duniani, hivyo ni sahihi IPTL/PAP kulipwa fedha za escrow sababu Dispute ilikwaisha.
 
Wamesha elewa. Ripoti inakuja kufunika kabisa, nakuwapoteza wanasiasa uchwara.
Nakaonea huruma katumbili nakumbuka siku zile alipokuwa analilia ubunge wake mpaka kamasi zinamtoka huku akitembea kwa magoti kumfata mbatia amsamehe. Dahhh!

tumbiri alitembea kwa magoti huku akimfata Mbatia, Duuhhh! Hii kali.
 
ivi nyie ni watz kweli...na je mnasimamia haki kweli...?? maana ukweli wa hili swala upo wazi kwa kusoma na kuelewa tuuu...daah. nawasikitikia sana.

PAC wala rushwa tu! PAC wanatumika na mafisadi wakubwa wa nchi hii! PAC wanatumika na SCB-HK! PAC wana ajenda zao za kisiasa!
 

IPTL ndio wamiliki halali wa fedha za escrow na mahakama kuu ndio iliyotoa uamuzi huo wa IPTL/PAP kumilikishwa fedha za akaunti ya escrow.
 

iptl Mungu atawasimamia haki yenu haitaporwa kamwe
 
iptl ndio wamiliki halali wa fedha za escrow na mahakama kuu ndio iliyotoa uamuzi huo wa iptl/pap kumilikishwa fedha za akaunti ya escrow.

mbaya zaidi maamuzi yalitolewa na mahakama zetu wala sio nje ya nchi,tumewanyanyasa iptl vya kutosha
 

hili ndilo la ajabu zaidi kama suala hili lilifuata makubaliano yaliyowekwa wakati wa kuanzisha akaunti hii ya escrow kwanini watu wavumishe ni ufisadi
 
Alikuibia Mkeo nini? Acha udaku wewe, umetumwa kututoa kwenye topic? IPTL/PAP hawana kesi na TANESCO popote pale duniani, hivyo ni sahihi IPTL/PAP kulipwa fedha za escrow sababu Dispute ilikwaisha.

labda singa alikua mkewe hatarin sana
 

tena ni fedha halali za iptl na wanastahili kuombwa radhi kkwa kuchafuliwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…