Ipo wapi thamani ya JOHO la kuhitimu kama zamani?


Wabongo utawaweza?

Badala ya kujiuliza ubora wa elimu yetu ukoje watu wanajikita kwenye majoho.

Halafu hata kama mtu unajikita kwenye majoho, kukataza watoto kuvaa majoho ni habari zile zile za "watoto ni taifa la kesho" wakati watu wanaishi leo.

Kama joho ni kitu kizuri, basi ni kitu kizuri kwa wakubwa na watoto.

Hizi ndizo zile habari za kufanya elimu kuwa ngumu na kufikiri ndio kufanya elimu kuwa bora.

Linchi limekaa miaka kibao chuo kikuu kimoja tu, mwalimu anayefelisha sana ndiye anaonekana mzuri.

Unnecessary exclusivity.

Tuongelee elimu, joho hata vibaka wanaweza kufoji.
 
Binti yangu ka graduate chekechea juzi kavaa joho na cheti juuu, ni shidaa hata hawaelewi maana ya hilo joho na cheti.

Na wewe pia Una Mtoto duh, kweli Dunia imefika mwisho au Ulimuiba Hosptalini?

 
Hahahhhhh elimu ishakua biashara inapimwa kwa amount of money
 
Chekechea wameharibu hii makitu.
Kwisha habari yake
 


Joho la ukweli ambalo nilivaa mimi lilikuwa na vipandevitatu = mortarboard (bonnet for PhD) or hat, gown, and hood. Bila utatu huujoho halina hadhi ya academic excellence katika levels za juu. Hata kwenyeKipaimara watoto wanavaa majoho lakini hayana utatu au chungu bila mafigamatatu hakifanyi kazi. Tuondoe wasiwasi ila siku wasiohusika na academicexcellence in a higher level, inabidi kuandamana!


Natia shaka na degree yako kama ulivaa joho bila kuwa criticalna ku-question maana ya vile vipande vitatu na utofauti wake katika rangi hasahood, na kwa nini wale wa PhD wanapigiwa na ala za brass band!!!!

 
Tuondoe wasiwasi ila siku wasiohusika na academicexcellence in a higher level wakipiga utatu huu, inabidikuandamana!
Halafu inakuaje graduate unashindwa kuona tofauti ya johoulilovaa na la mwanao aliyemaliza vidudu??!! Umemaliza Hope University nini?!

 

In a course of 100 graduates, ni 10 pekee ndio wanadeserve hiyo degree. Wengi wamekariri tu na ukija kwenye real life ndipo utakapowaonea huruma. Hadi yule aliyesoma Bachelor ya Small Business and Entrepreneurship anatafuta kazi ya kuajiriwa..
 
In a course of 100 graduates, ni 10 pekee ndio wanadeserve hiyo degree. Wengi wamekariri tu na ukija kwenye real life ndipo utakapowaonea huruma. Hadi yule aliyesoma Bachelor ya Small Business and Entrepreneurship anatafuta kazi ya kuajiriwa..

Wacha wasote na majoho si tusote na mahela, chuo ilikua zamani saaana sio enzi hizi za BRN wadau muelewe
Unamaliza chuo hata chembe la utofauti na mtu aliyehitim ngazi ya cheti hamna,
Unadai hadhi ya joho nawakati hadhi yako kwenye life skils hatuioni?
Umevaa joho kwa ajili unahitm mfano biashara na ujasiriamali unazunguka na bahasha kumwomba kazi nani ? Na wakati wewe ndo inabidi uombwe?
 

wewe sio mbongo ??
 

Hiyo ndio shida ya mfumo wa elimu wa kitanzania,mitihani migumu ndio kudhani kwamba wanafanya elimu ionekane bora. mwalimu anakuja darasani anajigamba semista hii lazima nishike watu 200 kwenye somo langu kweli anafanya hivyo.

Nakumbuka miaka kadhaaa iliyopita nikiwa darasa la saba mwalimu wa hesabu alileta maswali ya Quadratic equation ya kutumia general formula wakati hayo mambo yanafundishwa kidato cha pili,wote tukapata sifuri,mwl akafanya watu waiogope hesabu na kuichukia.

Huo ni utamaduni wa elimu ya kitanzania,mwalimu anaetunga mtihani mgumu tena wa kufelisha watu ndio mzuri,niliwahi kufundisha shule moja ya taasisi ya dini kwa muda, mwisho wa mhula nikatunga mtihani wa hesabu na geografia watoto wakafaulu sana,nikaitwa na mwl mkuu,mwl wa taaluma na mkuu wa idara kuhojiwa kwa nini nimetunga mtihani rahisi wakati haukua rahisi ila nilijikita kwenye mambo niliowafundisha.

Mwisho wakanitimua kazi eti natunga mitihani rahisi,yani niwatungie tu kitu ambacho sijawahi kufundisha au hakiko katika mtaala wao ili wasifaulu sana.
 

Matatizo sana mkuu.

Pole ku deal na watu primitive.
 

Kadiri siku zinavyokwenda hakutakuwa na tofauti baina ya majoho na hata chekechea pia watapigiwa tu brass band. Usiwa na shaka na degree yangu. MUHAS hawatoi degree za kubabaisha, sijui labda vyuo vingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…