IPhone tips

IPhone tips

mzenjiboy

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2010
Posts
907
Reaction score
387
Kwa watumiaji wa iPhone kama unataka kutuma email basi sio lazima kuandika.

Fungua email yako kisha andika address ya mtu unaemkusudia.

Kisha kwenye hiyo alama ya microphone hapo chini binya kisha soma au sema ujumbe wako in ENGLISH na ukimaliza binya Done.

Ukishabinya hiyo Done utaona message yako imejiandika na baada ya hapo unabinya SEND kwa kutuma ujumbe wako.

Hii inafanya kwa iPhone 4S na iPhone 5 ama iPhone nyengine sina hakika.
 
Bado sijakuelewa sehem gani ya microphone ninatumia iPhone 4s
 
Kwa kupitia iPhone yako inawezekana pia kwa watu wengine waliokaa karibu yako kuweza ku-connect na iPhone yako na kuweza kutumia internet.

Hatua za kufanya : Unafungua Settings kisha Personal Hotspot.

Bonyeza Personal Hotspot na itafunguka ukurasa wa pili. Katika ukurasa wa pili utaona tena Personal Hotspot kama iko kwenye Off basi iweke On ili iweze kufanya kazi.

Ukishaiweka On kwa maana hiyo kwa kila alie karibu nawe ikiwa ata-search basi ataipata iPhone yako lakini hatoweza kujiunga na internet yako mpaka umpe password yako.

Na password yako unaiona ipo hapo penye Wi-Fi Password.

Enjoy Your iPhone.
 
Kwenye watsup unaweza kutuma ujumbe wa sauti yako badala ya kuandika.

Fungua watsup yako: sehemu ya kuandika message yako kwa upande wa kulia utaona microphone.

Ili kurikodi sauti yako, weka kidole chako kwenye hiyo microphone na uzuwie, utaona inafunguka.

Ikishafunguka na bila ya kuachia kidole hapo tena utarikodi maneno yako na ukimaliza unaondoa kidole, huwa kazi imeisha, na ujumbe uko tayari kwa kutuma.

Na kabla ya kutuma unaweza kusikiliza kile ulichorikodi.

Enjoy your iPhone 🐠
 
Ni vizuri kujua salio (percentage ) la betri kwenye simu yako. Hii inasaidia kuchukua hadhari katika matumizi endapo huna charger mfukoni au kama upo eneo halina umeme.

Unaanza na Settings kisha General. Kwenye ukurasa wa General tafuta Usage. Binya Usage itafunguka ukurasa mwengine na hapo utaona Battery Percentage. Hapo penye Battery Percentage weka ON na kazi umemaliza.

Mara tu baada ya kuweka ON utaona alama ya betri huongezeka namba kama 80% au namba yoyote kwa kutegemea na salio lako.

Enjoy your iPhone ✈️
 
Kwa yeyote ambaye anakusudia kununua simu aina ya iPhone na ambayo imeshatumika, ikiwa kwa mtu au dukani anatakiwa ahakikishe ya kuwa :

Simu hiyo iko wazi yaani haihitaji pass code au Apple ID.

Pia ili kuhakikisha kama haijawekwa passcode itabidi uizime na kuiwasha mara mbili tatu ili uridhike.

Ama kuhakikisha kama simu haina apple id kwanza itabidi ujiunge na internet ndipo utaweza kujua.

La kufanya jiunge na internet, kama kwa Wi Fi au njia nyengine, kisha nenda kwenye Apple Store.

Ukifika hapo binya Search, hapo sehemu ya juu ya Search andika neno 'jamii forums'. Chagua 'jamiiforums' kisha bonyeza FREE kisha inakuja INSTAL.

Kama umekusudia kuINSTAL hapo ndipo utatakiwa kuweka apple id, na ikiwa hakutakiwi kuweka apple id inamaanisha ya kuwa simu iko wazi.

Kisha jaribu kuINSTAL kitu chengine ili uzidi kuhakikisha ya kuwa unauziwa kitu chenye dhamana.

Ushauri wangu ni bora mtu ukubali kusumbuka japo kidogo ili mradi wako uwe kuliko kuuziwa kitu ambacho huna uhakika nacho. 🌺
 
Back
Top Bottom