Ila CCM, Mungu anawaona

Ila CCM, Mungu anawaona

vis kipo

Senior Member
Joined
Aug 30, 2020
Posts
146
Reaction score
258
Kundi pekee la watu wanaoifaidi DEMOKRASIA ya kweli hapa nchini ni WAJUMBE WA CCM.
Ukiangalia wimbi na Kasi ya wanaowania kugombea katika majimbo mbalimbali hapa nchini, na kwamba wote wanawategemea WAJUMBE wa kuwapitisha katika kura za maoni, ni wazi kwamba Imani na matarajio ya watia nia yapo mikononi mwa WAJUMBE. Na katika kipengele hiki, hakuna mtia Nia anayemchukulia poa MJUMBE, kwa nini?... Kwa sababu anajua hatima yake IPO mikononi mwao.

Dhiki yangu ni hii hapa,
Ikiwa CCM wanaweza kupractice DEMOKRASIA kwa ukamilifu kiasi hicho katika kuwapata wagombea wao (ukamilifu kimaadili silisemei); wanafeli wapi kuwafanya WA Tanzania wote wawe kama WAJUMBE wao wa chama katika kuwapata viongozi wao wanaowataka? Kwamba badala ya watia Nia watano, saba au kumi katika Jimbo Moja, iwe ni CCM, CDM, ACT, CUF, NCCR, nk, nk, katika nchi Moja, na wote wawategemee "wajumbe" ambao ni wanachi, katika mizania huru na ya wazi.

Ingekuwa hivyo, hizi kelele za NRNE, Gwajimanization, Kitimanization, Bagonzanization... (Hivi Mwamakula Bado yupo?, simsikii kama enzi za mwendazake) Zingekuwepo? Ndiyo maana nasema CCM, MUNGU ANAWAONA
 
Back
Top Bottom