Wabunge wanaodhani posho ni ndogo na hawawezi kutimiza wajibu wao wajiuzulu! Kwani nafasi ya Ubunge ni nafasi ya uwakilishi na si biashara ambayo madhumuni yake kupata income kubwa au faida kama wanavyotaka ndugu zetu hawa!
Kuna watu kibao ambao wanaweza kutuwakilisha kwa moyo thabiti na kwa nguvu zao zote bila hata kudai kulipwa pesa lukuki kama ilivyo hivi sasa!
Kwa mwenendo wao wa sasa tumewafaham kwamba hawana nia thabit na wala kuguswa na matatizo halisi ya raia wa kawaida na ndio maana hata kwenye tatizo hili kubwa la watu kupoteza maisha kutokana na mgomo wa madaktari, kutoonyesha kuguswa kwa kuwa wao ni wana Appollo na si watu wanaofanana na sisi.
Tunawaomba waachie ngazi ili wakafanye biashara zitakazowalipa Returns kubwa na kuacha hizi nafasi za uwakilishi kwa watu wataoshirikiana na wananchi wa kawaida bila kudai ujira usifanana na shughuri zao!