IGP SIRRO , KWELI?

Joined
Mar 3, 2018
Posts
75
Reaction score
800
Hii inawezekana kama kuna nyumba jirani,ama hotel zipo karibu na hiyo round about,Mambosasa na Sirro wangeomba kushirikiana na wamiliki wa nyumba hizo na hotel ili wawape hizo videos.

Lakini nilichoona na kwa nature ya hiyo round about hakuna CCTV cameras ambazo zipo karibu na hapo anapopataja Sirro.
Na hata ingekuwepo nyumba au Hotel yenye CCTV camera IGP Sirro angewambia wana habari na Watanzania kwamba wamepata msaada huo na angetupatia picha pia za hapo round about zikiwa zinaonyesha muda wa gari ilipopita hapo!

Sirro ametaka kutumia ushamba wa Watanzania wa kutojua CCTV cameras akasahau kuwa na yeye hajui namna CCTV cameras zinavyooperate maana yeye amesomea Bunduki na mabomu tu!!

Lakini pia yeye mwenyewe amesema dunia imekua kama kijiji na akasema tena wamepambana na uharifu mwingi bila kuomba msaada!

Sirro amesahau kama teknolojia hiyo inayofanya sisi tuione dunia kuwa kama kijiji,nchi yetu inaburuza mkia hivyo kwenye mambo ya kiteknolojia huwezi kulitaja jeshi letu la aina yoyote ile!!

Mambo ambayo nimeyachukua ya msingi kwa Sirro ni;

Moja. Kuna umuhimu miji mikubwa nchi hii ifungiwe CCTV cameras japo matukio yakitekelezwa na magaidi wao wanajua namna ya kuziingilia hizo CCTV cameras hasa ambazo ni wireless.

Lakini pia tukio likitekelezwa na vigogo wa serikali,itakua ngumu kupata ushirikiano wa CCTV cameras ( kumbukeni AREA D pale Dodoma)

2. IGP Sirro anafunika kombe mwana haramu apite maana hana namna.

3. Lakini pia kwakua inaonekana CCTV camera jeshi letu linazitumia,basi lile tukio la Lissu tuanze na waliozichomoa baada ya tukio na hapo ndipo tutajua nani alihusika kumpiga Lissu.

Hizo picha alizokuja nazo Sirro za CCTV alitakiwa aje nazo vile vile hata kwenye tukio la Lissu japo zinachekesha kweli kweli.

Note; Leo Rais amekutana na wachezaji wa Taifa stars muda sawa na ule ambao IGP alikuwa anaongea na Watanzania. Hili tukio siyo la bahati mbaya.
Nadhani Yericko Nyerere anaweza kutusaidia maana yake lakini kwa uelewa wangu ilikuwa ni kupunguza idadi inayoshughurika na Sirro,kwa tafsiri ya mtaani ni kwamba Rais na Sirro leo wametugawana Watanzania kimkakati!!

Jamani karibuni Gwarama,

Elia F Michael.
Mbunge nje ya Bunge.
Mwenyekiti wa madiwani Kanda ya Magharibi.
19/Oktoba/2018.
 
Hivi Bunge halina uwezo wa kuamuru uchunguzi maalumu kutoka nje?

I mean Bunge kama Bunge!

Please anyone can educate me about this!
Mkuu huo ni ushauri mzuri...lkn kumbuka wabunge wengi ni wa chama tawala ambacho serikali yake haitupi majibu ya kuridhisha kwa mauaji,utekwaji,upoteaji na hata mambo mengi yananayoigusa jamii ambayo ni kunyume na katiba ya URT...hawawezi kupitisha mswada huo!
 
Kadri muda unavyozidi kwenda ndivyo tunayokaribia kuivisha, tukae makao wa kula.
 
Jamani kuna tofauti kubwa kati ya CCTV na SISITIVII sasa mkilinganisha mnakosea.Tekenolojia ya polis wetu ni ya juu sana kumbukeni ile mambosasa law of motion kama risasa ilipinda kona mara tatu itakuwa hii sisitivii!!?Mtuelewe tu tuko kwenye uchunguzi mzito wa wale wazungu wawili tujue walikula mboga gani kabla ya kumteka mooo.Mengine mtajihangaisha tu na vioo tumesha funga subirini madongo ya crazy rock muisome
 
wale wazungu wanaongea kizulu ,kikhoikhoi,au kiafricaan !!!
 
Kamanda zirro bwana alisema sisi tv limeiona gari kawe hahaha hii chai kabisa Tena Haina sukari
 
System imeoza, inacheza maigizo ya darasa la pili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…