Ifanye iPhone yako iwe Zaidi ya Simu

Ifanye iPhone yako iwe Zaidi ya Simu

ManiTek TV

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2011
Posts
410
Reaction score
159
[h=2]12/03/2013

Dijit: App itakayobadili iPhone Yako[/h]



Dijit si app mpya kwenye AppStore lakini ni app ambayo itaifanya iPhone, iPad au iPod Touch yako iwe ni zaidi ya simu. Dijit ni app ya rimoti, ambapo hufanya kazi badala ya rimoti zote za gajeti mbali mbali zinazotumia rimoti. Utahitaji kutumia pesa ya ziada japokuwa app hii ni bure, pesa ya ziada inatokana na ukweli kwamba unahitaji kununua kifaa kinachojulikana kama Beacon kilichotengenezwa na kampuni ya Griffin Technology.


Beacon inauzwa kama laki moja hivi, lakini utakaponunua, rimoti zote unafungia kwenye kabati iwapo unatumia gajeti yoyote ya iOS yaani iPad, iPhone au iPod Touch. Gajeti yako ya iOS huunganishwa na Beacon kwa teknolojia ya bluetooth kisha unaweza kuitafuta remoti yako katika database ya Dijit ambayo ina maelfu ya rimoti. Hivyo inafanya matumizi kuwa rahisi kabisa na utaratibu wa kutafuta ni rahisi kwa vile unachotakiwa ni kuingiza jina gajeti yako (brand) aina ya gajeti (TV, DVD, Receiver n.k) kisha unafuata maelekezo kui-programu.



Ikiwa unatumia kifaa cha kichina ambacho hakina hata brand upo uwezekano kuwa hakitakuwepo kwenye database ya Dijit, hata hivyo bado utaweza kuitumia gajeti yako kwa kuisomasha Dijit kifungo kimoja kimoja kwa kutumia rimoti yako ya asili, lakini ukishai-programu mara moja tu huna haja ya kurudia tena kazi hiyo kwa vile inahifadhiwa kwenye kumbu kumbu ya dijit yako. Gharama nyingine ambayo ni ndogo tu ni kwamba Griffin inatumia betri mbili aina ya AA za kawaida tu, lakini ni vyema kuwa na betri za reachargeable kwani griffin humaliza betri haraka kwa uzoefu wetu labda uwe unatoa betri kila baada ya kuitumia.


Tahadari ni kwamba kama rimoti imepotea na kifaa chako hakimo kwenye database ya dijit basi rimoti hii si suluhisho kwa sababu ili ifanye kazi na kifaa (TV, box, DVD n.k) chako ni lazima ama kifaa chako kiwe kwenye database yao au uwe na rimoti original ili u-programme dijit yako angalau mara moja kwenye kila kifaa cha iOS utakachokitumia.



Pia Dijit inakuruhusu kupanga mwenyewe ni gajeti gani unatumia na hivyo kukuunganishia gajeti hizo kwenye rimoti moja katika kile wanachokiita activity. Yaani kwa mfano kama unatazama DVD basi unapanga activity ya DVD na hivyo Dijit inakupa rimoti ambayo inakuwa na DVD, TV pamoja na Home Theatre yako, na kama unataza TV kwa kutumia dishi, basi unaweka activity itakayokuwa na rimoti ya TV na Receiver yako.


Pia unaweza kupanga kwenye chumba fulani kuna vifaa gani na hivyo unapochagua chumba, kama vile chumba cha kulala au sebleni digit inakupa rimoti za chumba kinachohusika tu.


Dijit pia inapatikana kwenye Android lakini mnunuaji awe na tahadhari kwenye suala la Beacon, kwa vile beacon ya iOS haiingiliani na Beacon ya Android. Vile vile kuna app nyingi zinazoweza kuifanya simu yako iwe rimoti kamili, lakini zote huwa lazima ziambatane na gajeti (kifaa) nyingine kama ilivyo Beacon kwa dijit.
Source: Gajetek - Gajet na Teknolojia
Twitter: gajetek




 
Hapo safi sana , nilikuwa sijui kama iPhone na yenyewe kuna namna ya kupata Remote Control japo haina ir port. Nilikuwa nikiitumia sana Psiloc irRemote kwenye nokia yangu ya zamani S60v2 (Nokia 6260) kipindi hicho wazee wanashangaa channel zinabadilika wakati wameshika remote!!
Sasahivi kuna Tablets za Android zenye infrared port kama Samsung Galaxy Note 10.1 hapa inakuja na inbuilt remote application inaitwa 'peel smart remote' ni nzuri sana, unachagua region yako, unachagua Tv, Decorder, Home Theater, Blue Ray Player, Radio au media player yeyote inayotumia remote alafu unaset remote control yake kwa kuelekezea simu kwenye Tv kama unavyofanya na remote ya kawaida. Brand za Tv zipo karibu zote na ukikosa brand yako kwenye listi unaidownload kupitia net..nta Attatch sample zake below,,

screenshot2013031301373.png


screenshot2013031301233.png


screenshot2013031301224.png


screenshot2013031301223.png
 
Nilikuwa nikiitumia sana Psiloc irRemote kwenye nokia yangu ya zamani S60v2 (Nokia 6260) kipindi hicho wazee wanashangaa channel zinabadilika wakati wameshika remote!!

mwenyewe nimetumia sana Psiloc irRemote nilivyokuwa na N93 na niliumia sana kuwa waliacha kutoa simu na infrared. nilikuwa sina mpango na tablet ila kama sina infrared.. anyway, kuliko kununua hiyo gadget ya Beacon, naona ni bora kununua apple TV as ndo inakuja na native support ya kufanya iPad, iPod na iPhone iwe remote yake plus ina mambo mengi kama streaming kutoka kwenye PC.
 
Hizi remote zinafaa kwenye simu za aina gani? Kwa nokia lumia 920 je?
 
Kiongozi hii nimeikubali amna mautindu zaid juu ya i phone ila isiwe yale ya kujail break ctaki hata kuyasikia maana yalinisumbua mpk nikatamani uza simu yangu na pia nahitaji front face camera kwaajili ya i phone 4 wapi naweza pata
 
Kiongozi hii nimeikubali amna mautindu zaid juu ya i phone ila isiwe yale ya kujail break ctaki hata kuyasikia maana yalinisumbua mpk nikatamani uza simu yangu na pia nahitaji front face camera kwaajili ya i phone 4 wapi naweza pata

Hii haihitaji jailbreak na front face camera iko mbele ya iPhone 4 yako au ya mtu yoyote yule lakini sidhani kama utampata yule ambaye atakuwa tayari kukuuzia front face camera bila ya simu, hata Apple wenyewe hawauzi. Kama unamaanisha umevunjika au kuharibika basi unaweza kupata kwenye ebay kwa chini ya $10, kuwa makini wasije kukuuzia ya kichina.
 
Kwani wadau c tnaotumia android 2.3.6 ndo 2metengwa na hz remote.??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom